Agosti 8, 2022 watoto huko Nantong mkoani Jiangsu China walijifunza ujuzi kuhusu kilimo katika uwanja wa mazoezi wa “shamba la furaha” katika kijiji cha Hangqiao mjini Rugao. Kwenye mapumziko hayo ya majira ya joto, shamba hilo lilifunguliwa bure kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari, na kuwafundisha wanafunzi ujuzi wa kilimo na ujuzi wa kazi na kuongeza furaha katika maisha yao ya mapumziko ya majira ya joto.