SIKU UKIIBIWA NDIYO UTAJUA MWIZI ANATAKIWA KUTENDEWA NINI LAKINI KWA SASA ENDELEA NA POROJO AMBAZO HATA KWENYE HIZO DINI ZETU ZOTE HAKUNA LISEMALO UMWACHE MWIZI HAI ILA KWA DINI ZA MAZINGAOMBWE WANAKUAMBIA SABA MARA SABINI MAANA YAKE UIBIWE MARA MIA NNE TISINI ILE YA TISINI NA MOJA SIJUI NAYO USAMEHE AU?
BADO MMOJA,
Jaribu kidogo kuwa realistic. Usidhani ka ni wewe tu uliyewahi kuibiwa, tena wakati mgumu sana na mahali pabaya saana. Lakini, kama kweli weye ni Mkristo, unayeujua Ukristo, sidhani ka ungelikuwa na mawazo yako. Njoo uwe Mkristo uishi Kikristo, hutayawaza uwazayo.
Wakati usafiri ni shida, nilisafiri na familia yangu kutoka Musoma kuja Arusha. Familia ya watu 8, sintaisahau hiyo safari kwani ilikuwa kuungaunga. Musoma - Mwanza, Mwanza - Nzega, Nzega - Singinda, Singida - Arusha. Ni safari ngumu, ndefu na ya kuchosha. Waweza kuona kuwa ulikuwa ujinga lakini aliyesafiri kipindi hicho cha 80s anajua nilichofanya ni hekima sana.
Nikiwa Singida, nikaibiwa nusu ya hela zangu zote za safari. Tena kwa mtu aliyejifanya msamaria mwema na kunisaidia mizigo na baadhi ya watoto. Ninachomshukuru Mungu ni kuwa, hakuwaumiza watoto wala hakuniumiza mimi ila alinimaliza nguvu kabisa. Nilifedheheka mbele ya familia ka baba waliyemwona ni Tyson asiyetishwa. Lakini siku hiyo, begi langu likachukuliwa vivi hivi tukiangalia likatokomea gizani. Ili kuwafanya wale genge la jambazi waondoke nika walilia kuwa jamani tunaenda mbali na angalieni familia mnihurumie hata nusu ya nauli wakacheka kicheko cha fisi wakatokomea gizani na matisho kuwa watarudi tena. Namshukuru Mungu hawakurudi.
Nikafungua maboksi yangu na kutoa hela niliokuwa nimeificha humo, asubuhi tukapata gari la kufika Arusha. Hebu niambie, ni mimi leo kweli nawatetea wezi?? Namshukuru Mungu aliyewafumba macho wasinivamie tena pale stand Singida hata wakawadhuru watu wangu.