Watanzania wana uelewa mdogo kuhusu Pension Fund, 25% ni maamuzi sahihi

Nina mashaka na elimu na uelewa wa viongozi wengi Tanzania, inasikitisha sana..
 
tutaweza,

Pole Sana Hizo habari za mwajiri kuchangia sijui 10 per na mwajiriwa 10 per au mwajiri 15 per na muajiriwa 5per ni Kanuni za mfuko husika, Hapa hatuongelei Mada hiyo, Hapa tunaongelea uelewa wa watanzania kuhusu Pension

Story za darasani sijui percent hizo hazituhusu au story Za sijui Nssf au Psssf hizo Kanuni anzisha uzi wako

Tatizo lenu hamjasoma hiyo sheria mnasubiri vipande vipande mtafuniwe

Rudi soma sheria yote na kikokotozi cha pension yaani Formula ya Sasa ikoje
 
Mkuu twende polepole.

Kulingana na kanuni mpya, Endapo Mstaafu atafariki Familia yake italipwa pension ya mwezi kwa miaka 3 mbeleni.Baada ya hapo biashara imeisha.Hapa ndipo kwenye wizi Mkuu.

Mfano umestaafu 2018 ukalipwa 25m toka kwenye 100m, 2020 ukafariki baada ya kupokea pension yako ya mwezi kwa miaka 2 tu..Zaidi ya asilimia 70 ya pesa Zako zinaenda wapi? Hebu tujuze sisi wenye uelewa mdogo.
Madhara ya kusoma Tanzania Mtu akishindwa kujibu hoja huanza kukasirika na kutukana

Serikali haijaanzisha hii mifuko kujaza watu pesa duniani kote, Ipo kutoa Kinga tu

Tatizo hamjasoma hiyo sheria, Pia hamfahamu maana ya Pension

Pension unapewa kwa Kanuni na mahesabu maalum

Serikali kwa Sasa imekuja na Kanuni muafaka wameondokana na Kila mfuko kujifanyia lake
 
Hivi hawa watu wanajua kweli uhalisia wa wananchi wao kule Peramiho, Namtumbo nk kiasi cha kuanzisha mifumo kama hii..
 
Madhara ya kusubiri serikali iwaletee maendeleo kwenye majumba yenu ndio haya mnalilia Bila kuhoji faida zake, soma hitimisho la uzi
Am a qualified Engineer niliyepata Elimu bora ya enzi ya Mwalimu Kambarage Nikianzia Ifunda Tech Sec.School miaka 1983. Sina shida kabisa ya maisha. Lakini haiondoki haki yangu ya kutoshabikia ujinga wa maamuzi yenu kwa haki za Watanzania.
 
Pole Sana Hizo habari za mwajiri kuchangia sijui 10 per na mwajiriwa 10 per au mwajiri 15 per na muajiriwa 5per ni Kanuni za mfuko husika, Hapa hatuongelei Mada hiyo, Hapa tunaongelea uelewa wa watanzania kuhusu Pension

Story za darasani sijui percent hizo hazituhusu au story Za sijui Nssf au Psssf hizo Kanuni anzisha uzi wako

Tatizo lenu hamjasoma hiyo sheria mnasubiri vipande vipande mtafuniwe

Rudi soma sheria yote na kikokotozi cha pension yaani Formula ya Sasa ikoje
Pole wewe. Kwanza kwa kudhani naongelea kwa akili ya darasani tu. Nimekuambia source ili ukajisomee.

Ninachoongelea ni wewe kusema hiyo ni defined benefit plan na wakati ni contribution plan. Unadhani wale walioweka utaratibu wa fao la kujitoa hapo kabla walikuwa mazwazwa na hawajafanya utafiti?

Kwa sasa hiyo 25% na fao la kukosa ajira inaweza ikawa hatua sahihi ili kuhakikisha uhai wa hii mifuko baada ya kukopwa na serikali. Halafu unaposema % kubwa ya investment ya hii mifuko ni gvt bonds unadhani ni sahihi?

Anyway, let's agree to disagree.
 
Ahsante kiongozi kwa kuuliza na kuhoji
Kwenye hizi bima hasa ya NHIF kuna mambo watu hawaambiwi pia, Hii Bima ya NHIF kuna vitu "neno la kiswahili "not covered niseme haitoi Kinga kwa baadhi ya Magonjwa lakini watu hawajaambiwa mpaka yakukute,
Tunapojadili Mtu anachangia na serikali pia inachangia NHIF walichofanya ni kupunguza gharama yaani Cost sharing tu tofauti na zamani

Hebu jaribu kuelewesha kwa ufasaha na kwa lugha iliyonyooka na kueleweka kwa urahisi......

Mfano mimi hapa ninayo bima ya afya (NHIF) ambayo nachangia mwenyewe kama Tshs. 70,000 kila mwezi.....

Unataka kuniambia nikiugua sitaweza kupewa huduma ya afya? Kuna magonjwa selective ya kutibiwa na Bima yangu ya afya? Is that what you mean here? Nini maana ya kuwa na Bima ya afya sasa if that is the case?

Tukirudi nyuma ni kuwa, hoja yako mwanzo ilikuwa ni kutolea mfano wa South Africa kuwa huko waajiriwa serikali yao haishughuliki nao ktk mambo ya bima za afya
jambo ambalo sina hakika kama ni kweli......

Ukasema wao wenyewe ndiyo hujichagulia makampuni ya bima ya afya wanayotaka na kujiunga nayo kwa kuchangia wenyewe......

Mimi nikakuuliza hivi.

Kwani sisi hapa Tanzania kuna raia ambao wanalipiwa bima zao za afya na serikali?

Lakini naona kama hujajibu swali hili kwa ufasaha na badala yake umechanganya sentensi tu za kiingereza na kiswahili pasipo kueleweka vizuri......

Yeah, inawezekana ulikuwa na lengo zuri la kuelewesha. Lakini nasikitika kusema kuwa sijakuelewa kabisa.....

Sasa kwa manufaa ya wengine, hebu rudia tena kujibu swali langu hapo juu kwa utulivu na kwa lugha fasaha ya kueleweka kwa urahisi......
 
Gussie katika bandiko lako unataka kisema ili mstaafu aweze kujiongezea muda wa kuishi anahitaji pesa kidogo kidogo zikiwa nyingi ataishi maisha ya tamaa hivyo kujiongezea vihatarishi. Ushajiuliza hao wastaafu walikuwa na mshahara kiasi gani wakati wakiwa kwenye ajira ndo uone hii pensheni wanayolipwa inaongeza hali hatarishi kwa kulipwa kwa mkupuo wa 75%?

Ikiwa mtumishi huyu wakati wa ajira hakuweza hata kuweka akiba kwa sababu ya mahitaji ya familia mfano elimu, makazi na mahitaji mengine muhimu leo amestaafu unadiriki kusema ndio wakati maisha yake yataboreka? Mshahara wenyewe ulikuwa haumtoshi sembuse hiyo pesa kidogo wastani wa 20% aliyojikusanyia kwa kipindi chote akiwa kwenye ajira.

Nchi zilizoendelea mstaafu akikuambia ni pensioner huyu ndio mwenye maisha mazuri maana hata kodi haikatwi sio hiyo Tanzania unayoiongelea. Unamzungumziaje mstaafu anayeishi mjini ambaye kwa kiwango cha mshahara alichokuwa analipwa hakuwahi kumiliki hata kibamda utarajie aweze kuendelea kuishi kwa pensheni ya 25% huku akiendelea kulipa pango la nyumba?

Nitakuwa na kosa gani kusema wewe ndio unahitaji kuelimishwa kuhusu 25% badsla ya hao wastaafu kwa kuwa uelewa wako ni kdogo? Je unaishi Tanzania? Je wewe ni mtumishi wa umma?

Toa uzoefu wako kulingana na kipato halisi unachopata kwa mwezi. Hii itakuondolea nadharia ulizojiwekea kichwani ukiweka uhalisia wa namna hiyo 25% itakuondolea hivyo vihatarishi unavyosema.
 
Unachagua nini wakati umewekewa sheria?

Kwanza sifa ya hiyo penshion lazima uwe umechangia angalau miaka15 na pia ufiikie umri wakustafu yaani miaka 55 ndio utapata25% kisha utaendealea kupata iyo pensheni.

Lakini, kama sisi ambao tumechangia katika mifuko chini ya miaka 15 hatuna sifa ya pensheni. Utapewa 25% pesa yako tu uliyoyachangia na kama hutakuwa ujapata ajira nyingine kwa sisi ambao hatujafika miaka 55, baada ya kupewa hiyo 25% utasubiri tena miezi6+ kama utakuwa ujapata ajira mpya. Then ndio wakufikirie kama wanakusaidiaje.

Sasa kama mimi nipo sekta binafsi, nipo NGOs nimefanya kazi hapo kama miaka 2 na hilo shirika linaondoka nchini, michango yangu ipo LAPF kama sh3,000,000 tu. Sasa nikipewa 25% ni sawa sh 750,000 sasa hii pesa naifanyia nini? Kodi ya chumba tu ni sh720,000 nakumbuka mi sina sifa ya pensheni kiasi kilichobaki watakuwa wananilipa kidogokidogo kila baada ya miezi 6+ huu si ukatili?
 
Bahati mbaya umeshindwa kufafanua hoja yako kuhusu ubora wa ulipaji huu wa asilimia 25 tofauti na wa awali wa asilimia 50. Umezungumzia kuhusu elimu, kua endapo elimu ingetolewa kuhusu malipo ya pensheni wananchi wangeishukuru sana serikali, lakini kwa bahati mbaya (au makusudi ?) wewe hukutoa elimu hiyo.

Tuanze kuongelea ulichokiita "moral harzad situation". Kwa namna yoyote ile inashangaza kua namna ambavyo mtu anaamua kutumia pesa yake (katika mambo ambayo si kinyume cha sheria) iwe tatizo kwa mtu mwengine, kiasi cha kuamua kumpunguzia kiasi chake cha pesa, eti kwakua anakunywa pombe au kuvuta sigara akijua kua pesa yake ipo hivyo, anaweza kuendelea kuishi vile apendavyo. Ikumbukwe na ifahamike kua pesa hizi si za hisani, ni fedha za akiba ambazo mfanyakazi amekua akikatwa katika mshahara wake halali pamoja na kiasi anachowekewa na muajiri wake. Kwa ufupi pesa hizi ni za mfanyakazi na si hisani anayopewa au asante, na zinakatwa kisheria. Hivyo basi namna atakavyo zitumia, alimradi havunji sheria za nchi haipaswi na inashangaza endapo eti inamkera mtu namna ambavyo mtumishi baada ya kipindi chake kirefu cha utumishi atatumia pesa zake.

Muundo ya uwekezaji. Kuhusu suala la muundo wa uwekezaji kimsingi mifuko hii kwa utaratibu uliopo sasa, ndio ina dhamana ya uwekezaji wa pesa zilizo katika mifuko hii. Ikumbukwe kua kipaumbele cha kwa kwanza cha mifuko hii si uwekezaji badala yake ni usalama wa fedha za watumishi, hivyo mzigo wa uwekezaji mbovu au mfumo mbovu wa uwekezaji si tu hautaki kubebeshwa watumishi lakini hautaki kuonekana kama jambo linaloweza kustahimiliwa tuu na watumishi.

Umri wa kuishi. Hili si jambo linalohitaji mjadala mrefu, kwani takwimu za wastani wa kuishi kwa mtanzania ni umri gani? (Si ndio kazi ya takwimu hii ?)

Mwisho ikumbukwe, hili ni suala nyeti sana kwa maslahi ya mtumishi yoyote anayestaafu na kwa familia yake kwa ujumla, halitakiwi kuletwa kwa watumishi taena katika hali ya kuwakebehi na kuwadharau kua uelewa wao ni mdogo sana. Uelewa wa watumishi ni mdogo katika kutambua maslahi yao? Yaani watumishi ni mbumbumbu kiasi hata hawaelewi kuhusu mambo bora na yanayofaa mustakabi wa maisha yao! Kwa vyovyote hili ni tusi mleta mada umelitoa kwa watumishi, watu hawa ambao wametumia kiasi kikubwa cha umri wao katika utumishi na ustawi wa taifa letu katika nyanja mbalimbali.

Wakatabahu.
 
Alafu ITV wanakuja na kipima joto eti, "je watoto wa kike kupata mimba mashuleni, je mimba hizo wanapewa na wanaume??" Wanaacha trending issues kama hizi...https://jamii.app/JFUserGuide
 
Pls sijui niseme nini lakini nataka kukuambia umeongea uongo kuhusu hali ya kuongezeka kwa maisha, ukiangalia tanzania life expentancy ni miaka 65 peke yake, na ukiangalia taifa la Norway life expectancy ni 84 years, america ni 80 years, hio ni kwa wanaume, sasa hapa ndipo umekosea, ndio matibabu yako juu, utaalamu wa kutibu magojwa uko wa hali ya juu, LAKINI NI KWA MATAIFA TAJIRI PEKEE, tanzania bado watu wanafariki kwa malaria, kifua kukuu, kuhara au cholera, kukosa mlo bora na stress za umasikini, so huwezi kutuambia ati life expectancy ndio inafanya serikali ifanye hii jambo A BIG NO, ile kitu kinafanya ccm ifanye hii jambo ni moja tu, LACK OF POLICY PERIOD.

CCM haina wataalamu amao wanajua vile hali halisi.
 
Note my point: Jiwe akiondoka madarakani akaja mwenye mtazamo tofauti hii sheria itabadilishwa tena. tusubiri na tuombe uzima after 2025
 
Kiongozi ndio maana nimekuambia kuna aina nyingi za kuchangia, Elimu ni ndogo sana ya pension hapa kwetu, Huo mfumo wa ma DC au RC ni ishu ya Wataalamu tu kuamua, wao wanalipwa kwa Mara moja wanaita "Gratuity "

Kikubwa ni kuelimisha Raia mifumo iliyopo halafu tuchague

Akhaa mnakera sana..eti elimu ya mifuko ya jamii, kwa nini awamu hii na sio awamu zilizopita?Poleni watumishi wa nchi hii,Inakera sana, hela za wastaafu zikajenge viwanda? Tupe basi mifano hai wapi kwingineko hapa duniani haya yalitendeka ewe msomi wa Pension funds
 
Tembea uone Mkuu,
Huko Africa kusini hata mambo ya Afya mwajiri hayamuhusu ni wewe mwenyewe unatafuta Insurance upendayo unachangia

Hapa Tanzania uelewa ni mdogo Sana, Watu Kila kitu wanasubiri serikali

Achana na mambo ya serikali utakufa maskini Jifunze
Kumbe hata ulichopost hukijui... Ukiajiriwa serikalini Tz unaingizwa moja kwa moja NHIF sasa hapo mtu akitaka kujiunga na bima nyingine anafanyaje? Na kwa taarifa yako hizo bima nyingine km AAR serikali imeingiza makucha yake...
 
Kuna uwezekano mkubwa wastaafu watakaoanza na sheria hii wakafa mapema kutokana na msongo wa mawazo.

Kwani kisaikolojia walishajiandaa kustaafu na kanuni za kikokotozi cha awali lakini hii imekuja pasipo kutarajia na tayari mda wa kujipanga kimaisha uko ukingoni kama hakujipanga akitegemea pensheni.

Ukitaka kujua hali ikoje, jaribu kuvaa viatu vya wahusika.
Nadhani lengo la serikali ni kutaka hela hii ibaki kwenye mikono yao ili waendelee kuiwekeza kwenye shughuli za maendeleo. Nia ni nzuri lakini sasa inawaumiza wazee hawa. Siilaumu sana serikali lakini nawahurumia sana hawa walioguswa moja kwa moja katika hili pengine kadiri mda utakavyoenda watumishi watajipanga kisaikolojia kuikubali hali hii maana saivi wengi bado wanashangaa hawaamini amini kama ndio imekuwa vile.

Watumishi pigeni moyo konde wala msihuzunike sana badala yake badilisheni mitazamo na mambo yataenda vizuri tu.
ukisoma makala ya mleta uzi inaonyesha kabisa kuwa kuishi miaka mingi kwa mstaafu ni kikwazo na tatizo kwao hao watu wa mifuko ya pensheni,wanapendelea wastaafu wafe mapema.
 
Back
Top Bottom