Watanzania walio Msumbiji wadai wana matatizo

Watanzania walio Msumbiji wadai wana matatizo

Duuuu kweli nchi yangu Tanzania ni mahali salama pa kuishi over hakuna uongozi sasa nini maana ya ujirani mwema na sisi tukiamua kuwatimua wamakonde wa huko itakuwaje watu wa ajabu sana hawa
Na hawa watu kama wameanza hivyo tena sio vizur wajue had jeshi lao linafundishwa na makomando kutoka tanzania

Wakizingua mabeyo atume wanaume kule wakafanye mambo huu ni zaid ya uchiro haiwezekan mtu kahiyari mwenyewe arudi then umushushe kwenye gali
 
Hii k2 Mozambique ipo mida mref Sana watz kunyanyaswa saiv imekua too much,ulikua Ni kawaida mbongo kuuawa kwa kosa Tu la kuvuka border Na kuchimba dhahab,kunyang'anywa Mali Na kuchomewa maduka.ifike mahali serikal iingilie Kati hili suala
 
Hilo ni Swala la Histroria watu wa Kaskazini mwa Msumbiji wana hasira sana na TZ Wengi waliunga mkono RENAMO na kama si Tanzania kuipigania FRELIMObleo wangekuwa labda wanatawala Msumbiji au wana nchi yao,
 
Huko Kusini pa kwenda ni Namibia tu ambapo Mtanzania ukitokeza unapokelewa na jina la "Nyerere! Nyerere!" sio kwingine.
 
Kuna taarifa tangu jana zilikuwa zikisambaa katika mitandao ya kijamii, kuhusu watanzania waishio Msumbiji wamekamatwa na serikali ya huko na kuuwawa!ikiwa ni pamoja kuwekwa jela kwa kilichoelezwa kuwa waondoke Msumbiji sikwao!! na hata kama ulikuwa na karatasi halali za kuishi huko na kufanya kazi wametiwa ndani pia ,na hawakuwa na mda wakusoma dokment za mtu yoyote!! hata pasi za kusafiria zimechomwa!! hadi jana watu walikuwa hawatoki ndani!!!Inasadikika watu 4 walipoteza uhai!.Na hilo katika kipindi cha PowerBreakfast cha Clouds amesikika mtu akiojiwa na Clouds kuhusu hali ya huko na alikuwa akiomba msaada.
Hivyo tunaomba serikali kupitia Wizara ya Mambo ya Nje ichunguze hizi tuhuma.
 
Wale jamaa hawa utu kabisa!Hata Maputo ambako ndiko mjini manyanyaso ya kijinga kijinga kwa foreigner huwa yapo.Ajabu wanawahusudu sana watu jamii ya Wareno.
Kaeni kwenu, mbona mnawahusu sana wahindi
 
Hivi kile chama cha ushirikiano kati ya Msumbiji na Tanzania TAMOFA kilikufa?
 
Raia wa Tz hawana samani
Hakuna chochote hapo
Na hakuna kiongozi anaesikia uchungu
Juu ya watz wanaoua nje ya nchi
Ni wengi walisha uawa lakini hakuna kitu

"Ni aibu raia wa nchi hii kuuliwa nje huko"
Na pasipo hatua yoyote kuchukuliwa.
 
Bas polen sana achane kulia lia rudin kwenye nchi yenu mtulizane mbona mimi niriludi niko home tz nakiga mishe zangu

Na kumbuka hizo ambush hazijaanza leo huwa ni kila mwaka na watu tulikua tunashinda polin mfano mimi nilikimbilia namapa baada ya kutulia ndo nikarud nikaendelea kupiga kazi zangu kama kawaida

Afu kitu kingine police wa mozbiqu wanapenda sana hela aka dinyelu kwahiyo wakikubamba watoe umalizane nao bas
Unajua kusoma Kiswahili vizuri wewe?! hebu soma sentensi ya nne kutokea chini kaandika nini!!!!
 
Habari Wanajamvi::

Ujumbe unaotoka kwa binti Mtanzania Aliye Msumbiji Akifahamika kwa jina la Angel(Anna) Peter ukielekezwa Kwa Mwanahabari Maarufu (MILLARD AYO) ili aufikishe kwa Serikali ya Tanzania..

cf9545ed860f08a4218ca86d451773fe.jpg


Kama haya ni kweli na Balozi wa Tanzania Msumbiji yupo,na hajashughulikia jambo hili aangaliwe kwa jicho la tatu..

Na pia kama kuna ukweli Serikali kupitia wizara ya mambo ya nje ishughulikie jambo hili haraka sana.

NB: UNCONFIRMED
Wana vibali vya kuishi huko?kama hawana kosa la kwanza ni lao japo kuwafanyia hivyo si sawa wala utu,zamani nilikuwa nikisikia wamakonde wanakula watu sasa naanza kuamini kwa ukatili huu wanaweza kufanya hivyo!
 
Wapo wa
Wana vibali vya kuishi huko?kama hawana kosa la kwanza ni lao japo kuwafanyia hivyo si sawa wala utu,zamani nilikuwa nikisikia wamakonde wanakula watu sasa naanza kuamini kwa ukatili huu wanaweza kufanya hivyo!
Passport Na wanaishi kihalali jamaa wana wivu Sana coz wagen wanamake Sana hela kuliko wazawa.mtu ameinvest hela nyingi ataishije kimagumashi?
 
Kwa namna tulivyowasaidia hawa Mozambique, jinsi Wanajeshi wetu walivyokufa kwa ajiri ya kuitetea nchi Yao, kwa namna tulivyoisaidia hiyo nchi kupata Uhuru Wao, Na kwa namna tunavyoishi Na Raia Wao vizuri hapa Tanzania tena wakiwa hawana vibari!!!

Kwa kuzingatia Watanzania waliokumbwa Na tatizo hili Ni wengi, ningekua Mimi ndo mwenye Mamlaka, ningemrudisha Balozi wa Mozambique kwao.

Haiwezekani kwa yote tuliyofanya kwao waje Wafanye unyama Kama huu kwa Watanzania, hata Kama ni kuwarudisha makwao watu wanaoishi kinyume cha Sheria, wangewarudisha kwa kutowatesa Na kuwapora Mali zao!
 
Maisha taabu kweli kweli. Sisi tulioamua kutumia rasilimali na muda wetu kusaidia wengine sasa wanatugeuka, sijui ilikuwa ni busara kujijenga wenyewe tukawa imara mapema labda tusingekuwa tunakimbia kwetu kama sasa!
 
Kwa namna tulivyowasaidia hawa Mozambique, jinsi Wanajeshi wetu walivyokufa kwa ajiri ya kuitetea nchi Yao, kwa namna tulivyoisaidia hiyo nchi kupata Uhuru Wao, Na kwa namna tunavyoishi Na Raia Wao vizuri hapa Tanzania tena wakiwa hawana vibari!!!

Kwa kuzingatia Watanzania waliokumbwa Na tatizo hili Ni wengi, ningekua Mimi ndo mwenye Mamlaka, ningemrudisha Balozi wa Mozambique kwao.

Haiwezekani kwa yote tuliyofanya kwao waje Wafanye unyama Kama huu kwa Watanzania, hata Kama ni kuwarudisha makwao watu wanaoishi kinyume cha Sheria, wangewarudisha kwa kutowatesa Na kuwapora Mali zao!

Kwa jinsi nilivyomsikiliza Mh. Waziri jana, Watanzania wale watarudishwa Na kuacha kila walichochuma Mozambique!
 
Back
Top Bottom