MwanaFalsafa1
JF-Expert Member
- Feb 26, 2008
- 5,565
- 836
Na Mwandishi Wetu, Iringa
WAZIRI wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk. Diodorus Kamala, amewataka wasomi nchini kujiamini na kujiandaa kufanya kazi katika nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC).
Dk. Kamala alitoa kauli hiyo juzi katika Chuo Kikuu cha Tumaini mjini Iringa, wakati akizindua maonyesho ya Siku ya Waajiri Kukutana na Wahitimu Tarajiwa (Careers Day).
Alisema, mwakani milango ya soko la pamoja katika EAC itafunguliwa, hivyo Watanzania wanapaswa kujiandaa kwa ushindani.
Alisema, Watanzania wanayo maarifa ya kutosha, hivyo hawapaswi kuwa na wasiwasi juu ya kinachodaiwa kuwa Wakenya wanafahamu Kiingereza vyema kuliko Watanzania.
"Nawahakikishia kuwa Wakenya wanazungumza Kiingereza cha kienyeji, lakini sisi Watanzania tunazungumza Kiingereza cha Oxford (Uingereza)," alisema Dk. Kamala na kushangiliwa.
Alisisitiza kuwa, Watanzania wanapaswa kujifunza somo la Maendeleo ya Jamii (Development Studies), Mawasiliano ya Umma (Communication Skills), Maadili (Ethics) na Technolojia ya Mawasiliano ya Umma (ICT) kwa nia ya kujiweka katika nafasi nzuri zaidi kiushindani.
Alionya kuwa, wakati umefika kwa Watanzania kuanza kujifunza Kifaransa, kwani soko likifunguliwa nchi za Rwanda na Burundi zinazungumza Kifaransa, lakini zinajifunza Kiingereza kwa kasi kubwa, hivyo kama Watanzania watakuwa hawajui Kifaransa, itawawia vigumu kufanya kazi katika nchi hizo.
Waziri huyo alisema, faida za kuingia katika soko la Afrika Mashariki ni nyingi, kwani ukubwa wa soko utapanuka na gharama za uzalisjaji zinazidi kupungua.
Alitoa mfano wa mauzo ya Tanzania kwenda Kenya kuwa, tangu ushuru wa pamoja uanze kutekelezwa 2007, Tanzania imeongeza mauzo nchini humo kutoka wastani wa Sh bilioni 94.5 kufikia Sh bilioni 275.5.
Dk. Kamala alizitaka nchi wanachama wa Afrika Mashariki kuruhusu wananchi wa nchi hizo kufanya kazi katika nchi zao, kwa maelezo kuwa Tanzania imeshaonyesha njia.
"Leo hii Tanzania inaajiri wana-Afrika Mashariki wengi kuliko nchi nyingine yoyote, wapo kwenye hoteli na kila mahala," alisema.
Aliongeza kuwa serikali ya Tanzania imejenga misingi mizuri ya uchumi, na hadi sasa imedhibti mfumko wa bei kuliko nchi zote wanachama wa EAC.
"Mfumko wa beki kwa Kenya ni asilimia 26, Rwanda ni asilimi 19, Burundi ni asilimia 19, Uganda ni asilimia 13.4 na Tanzania ni asilimia 13.
Hii inamaanisha kwamba kama kuna mtu anataka kuwekeza dola zake, atanona ni hasara kuwekeza katika hizi nchi nyingine, hivyo atakimbilia Tanzania na ndivyo inavyokuwa," alisema na kushangiliwa.
Chuo Kikuu cha Tumaini kimekuwa cha kwanza kukutanisha waajiri na wahitimu tarajiwa, suala ambalo ni kawaida kwa nchi za Ulaya.
I agree with some of the things this guy has said. Tanzanians shouldn't be scared to compete and have more confidence with themselves. Some parts I don't agree with is e.g Tanzanians(I'm assuming he meant the majority) speak English from Oxford. Smatta my Kenyan bro, I am more curious to hear your opinions on this. I'm sure this is one piece both me and you will agree upon.
WAZIRI wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk. Diodorus Kamala, amewataka wasomi nchini kujiamini na kujiandaa kufanya kazi katika nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC).
Dk. Kamala alitoa kauli hiyo juzi katika Chuo Kikuu cha Tumaini mjini Iringa, wakati akizindua maonyesho ya Siku ya Waajiri Kukutana na Wahitimu Tarajiwa (Careers Day).
Alisema, mwakani milango ya soko la pamoja katika EAC itafunguliwa, hivyo Watanzania wanapaswa kujiandaa kwa ushindani.
Alisema, Watanzania wanayo maarifa ya kutosha, hivyo hawapaswi kuwa na wasiwasi juu ya kinachodaiwa kuwa Wakenya wanafahamu Kiingereza vyema kuliko Watanzania.
"Nawahakikishia kuwa Wakenya wanazungumza Kiingereza cha kienyeji, lakini sisi Watanzania tunazungumza Kiingereza cha Oxford (Uingereza)," alisema Dk. Kamala na kushangiliwa.
Alisisitiza kuwa, Watanzania wanapaswa kujifunza somo la Maendeleo ya Jamii (Development Studies), Mawasiliano ya Umma (Communication Skills), Maadili (Ethics) na Technolojia ya Mawasiliano ya Umma (ICT) kwa nia ya kujiweka katika nafasi nzuri zaidi kiushindani.
Alionya kuwa, wakati umefika kwa Watanzania kuanza kujifunza Kifaransa, kwani soko likifunguliwa nchi za Rwanda na Burundi zinazungumza Kifaransa, lakini zinajifunza Kiingereza kwa kasi kubwa, hivyo kama Watanzania watakuwa hawajui Kifaransa, itawawia vigumu kufanya kazi katika nchi hizo.
Waziri huyo alisema, faida za kuingia katika soko la Afrika Mashariki ni nyingi, kwani ukubwa wa soko utapanuka na gharama za uzalisjaji zinazidi kupungua.
Alitoa mfano wa mauzo ya Tanzania kwenda Kenya kuwa, tangu ushuru wa pamoja uanze kutekelezwa 2007, Tanzania imeongeza mauzo nchini humo kutoka wastani wa Sh bilioni 94.5 kufikia Sh bilioni 275.5.
Dk. Kamala alizitaka nchi wanachama wa Afrika Mashariki kuruhusu wananchi wa nchi hizo kufanya kazi katika nchi zao, kwa maelezo kuwa Tanzania imeshaonyesha njia.
"Leo hii Tanzania inaajiri wana-Afrika Mashariki wengi kuliko nchi nyingine yoyote, wapo kwenye hoteli na kila mahala," alisema.
Aliongeza kuwa serikali ya Tanzania imejenga misingi mizuri ya uchumi, na hadi sasa imedhibti mfumko wa bei kuliko nchi zote wanachama wa EAC.
"Mfumko wa beki kwa Kenya ni asilimia 26, Rwanda ni asilimi 19, Burundi ni asilimia 19, Uganda ni asilimia 13.4 na Tanzania ni asilimia 13.
Hii inamaanisha kwamba kama kuna mtu anataka kuwekeza dola zake, atanona ni hasara kuwekeza katika hizi nchi nyingine, hivyo atakimbilia Tanzania na ndivyo inavyokuwa," alisema na kushangiliwa.
Chuo Kikuu cha Tumaini kimekuwa cha kwanza kukutanisha waajiri na wahitimu tarajiwa, suala ambalo ni kawaida kwa nchi za Ulaya.
I agree with some of the things this guy has said. Tanzanians shouldn't be scared to compete and have more confidence with themselves. Some parts I don't agree with is e.g Tanzanians(I'm assuming he meant the majority) speak English from Oxford. Smatta my Kenyan bro, I am more curious to hear your opinions on this. I'm sure this is one piece both me and you will agree upon.