Watanzania tuungane kupinga mabaya haya ya awamu ya sita

Abraham Lincolnn

JF-Expert Member
Apr 12, 2018
2,533
4,317
Kwa umoja wetu, Tukiamini sauti ya wengi ni sauti ya Mungu, Na kamwe watawala hawajawahi kuishinda nguvu ya umoja wa umma ambao ndiyo sisi watanzania, Tuungane kukemea, Kupinga na kuchukua hatua ikibidi kuwalazimisha kung'atuka au kutokurudia makosa kuwarudisha katika viti vyao wakati wa uchaguzi ili kama taifa tuweze kusonga mbele.

1. Viongozi wanaosisitiza na kutamka hadharani kwamba kila mmoja ale kwa urefu wa kamba yake. Hii ni hatari na inapelekea viongozi kujihalalishia vitendo vya wizi wa mali ya umma

2. Viongozi wanaoendekeza ziara zisizokuwa na tija wala zisizobeba vipaumbele vya watanzania ambao wengi wanahitaji huduma za msingi za afya, maji, elimu, miundombinu n.k na sio maswala mengine yasiyo vipaumbele kwao. Ziara hizo pamoja na delegation zake zinaigharimu nchi kiwango kikubwa cha fedha zinazotokana na kodi zao.

3.Viongozi wasiojishusha na kufika chini kabisa kujua uhalisia wa maisha ya watanzania walio wengi na ikibidi kushiriki katika kutatua kero zao.

4.Viongozi wasio na uchungu wa mali na rasilimali za watanzania.Viongozi walio tayari kufukuza wamaasai katika makazi yao ya asili kwa ushawishi wa mwekezaji. Kiongozi ambaye yupo tayari kutoa bandari zetu ambazo tumeshagharamikia kwa kiasi kikubwa kwa masharti ambayo si rafiki, Ni Kiongozi wa kupingwa kwa nguvu zote.
5.Kukosa maono, kushindwa kuanzisha wala kusimamia miradi mikubwa na ya kimkakati.

Hayo ni machache, Nadhani Kiongozi wa aina hii hatufai hata kidogo!
 
Tanzania hiihii ya vijana wanaokariri mashairi ya nyimbo za Bongofleva na kucheza pool table ndiyo waandamane!

Sisi hatupo serious na maisha Mkuu though I conquer your move!
 
Kwa umoja wetu, Tukiamini sauti ya wengi ni sauti ya Mungu, Na kamwe watawala hawajawahi kuishinda nguvu ya umoja wa umma ambao ndiyo sisi watanzania, Tuungane kukemea...
Sawa.

Ila tu ukae ukijua yupo sana tu till 2030 Mungu akipenda.

Kama vp hamia Burundi
 
Sawa.
Ila tu ukae ukijua yupo sana tu till 2030 Mungu akipenda.
Kama vp hamia Burundi
Kwa hiyo mkuu wewe unaona ni sawa kilo ya sukari kufikia 4000? Unaona ni sawa viongozi wale kwa urefu wa kamba?

Unaona gharama zinazotumika kufanya ziara zisizokuwa na tija ni sawa? Bandari kumilikishwa unaona sawa? Miradi kusuasua, ukosefu wa ajira, kwako ni sawa? Utakuwa na wadudu kichwani
 
Kwa hiyo mkuu wewe unaona ni sawa kilo ya sukari kufikia 4000? Unaona ni sawa viongozi wale kwa urefu wa kamba?

Unaona gharama zinazotumika kufanya ziara zisizokuwa na tija ni sawa? Bandari kumilikishwa unaona sawa? Miradi kusuasua, ukosefu wa ajira, kwako ni sawa? Utakuwa na wadudu kichwani
Madudu unayo wewe unayeteseka kwa jambo ambalo utaishia kupiga kelele tu hapa kama debe tupu. Huna unachoweza kubadili till 2030 that's why ulishauriwa uhamie Burundi
 
3.Viongozi wasiojishusha na kufika chini kabisa kujua uhalisia wa maisha ya watanzania walio wengi na ikibidi kushiriki katika kutatua kero zao.
Huyu wa hivi namjua kabisa. Na huwa namuwazia angalau siku moja aje kushuhudia maisha ya watanganyika wa hali za chini; kabla hajasisitiza utekelezaji wa mikakati inayowatwisha mizigo wananchi wa tabaka la chini!
 
Kwa umoja wetu, Tukiamini sauti ya wengi ni sauti ya Mungu, Na kamwe watawala hawajawahi kuishinda nguvu ya umoja wa umma ambao ndiyo sisi watanzania, Tuungane kukemea, Kupinga na kuchukua hatua ikibidi kuwalazimisha kung'atuka
kwamba mtu makini, mchapakazi na mwenye bidii, aache kazi na shughuli zake za kujitafutia riziki yake ya kila siku, ababaike na kazi za wengine ati hawafanyi kazi zao vizuri, na halafu hata haionyeshi nani atafanya vizuri na kivipi, na halafu yeye alifanya kazi gani vizuri, wap na lini?🐒

Hiyo ni clueless and rudderless motion 🐒
 
Back
Top Bottom