Watanzania na Ubaguzi Wa Ujinga!

hayo maswali nalolijua ni Kuwa Vasco Da Gama alikuwa mzungu wa kwanza kupita Pwani ya Africa Mashariki akienda bara Hindi.. Sasa na wewe unaendelea Kuwa mmbaguzi wa Ujinga badala ya kutupa Elmu kuhusu hayo maswala mengine na ufafanuzi unaturingishia Kama unatoa darasa toa sio ujivuni wa kujua kitu halafu husemi, wengine sisi ni walimu na nyuzi za historia Kama hizi zinztufundisha mengi na tunapata challenges mpya za kuwapelekea wanafunzi wetu Sasa ka wewe hutoi majibu wala maelezo afu unatunanga utakuwa hujatusaidia sisi wala wanafunzi wetu. Siku zote najua Dar Es Salaam ni bandari ya salama ka sio hivyo sema ni nini? Na tupe maana ya majina ya Mikoa ili tuelimike sisi na wanafunzi wetu, ni Kama unajua kitu afu unataka ubembeleeezweee! Kufafanua huo pia ni ubaguzi wa ujinga

Kwanza, punguza ghadhab. Pili, umenifurahisha sana kuwa hasira na hamasa yako ni katika kutaka kusoma na kusomesha. Nakupa mkono wa heko kwa hilo.

Tatu twende taratibu, elimu haipatikani kiharaka na kiurahisi ndio maana leo tunaongelea Ubaguzi wa Ujinga. Laiti tungekuwa tunaipata elimu kiurahisi na sahali kama upendavyo basi tusingekuwa na Ubaguzi wa Ujinga. Nachelea kukupeleka haraka usije nibagua kwa ujinga tu. Tuanze na Dar Es Salaam:

Si Kiarabu tu, ni jina linalopatikana ndani ya Qur'an 10:25:

وَاللّهُ يَدْعُو إِلَى دَارِ السَّلاَمِ وَيَهْدِي مَن يَشَاء إِلَى صِرَاطٍ مُّسْتَقِيمٍ

WaAllahu yadAAoo ila dari alssalami wayahdee man yashao ila siratin mustaqeemin

But Allah doth call to the Home of Peace: He doth guide whom He pleaseth to a way that is straight.

Na Mwenyezi Mungu anaita kwendea Nyumba ya Amani, na anamwongoa amtakaye kwenye Njia Iliyo Nyooka.

Utaona kwa tafsiri hizo, jina Dar Es Salaam halihusiani kabisa na neno "bandari". Isitoshe, kuna miji mingine duniani ina jina hilo, hata mji maarufu sana Kihistoria na Kisiasa, uitwao Jerusalem, nao pia ni Dar Es Salaam, nako hakuna bahari kwayo Dar Es Salaam si "bandari" Salama, maana halisi ni hiyo hapo juu.

Pia kuna nchi inaitwa Brunei Darusalaam (Dar Es Salaam) nako mji wao ni wa bandari na unaitwa Bandar Seri Begawan. Ulidhani ingekuwa Dar Es Salaam.

Ukiridhika ni hili tutahamia lingine.
 
Kajipangeeee vizuriiii ndio ujeeeee no evidence, sources huelewekiii naona kama vileeee umepoteaaa jaribuu tena baadaee

Kipi hukukielewa? sitegemei kama unavielewa ni vitu ambavyo hukupewa uliposomeshwa na Waalimu wako waliosomeshwa kukujaza Ubaguzi wa Ujinga.

Huielewi Dar Es Salaam? au Afrika? au labda Arusha?
 
Enhee! Mkuu Zomba tuendelee nachohitaji ni majibu ya maswala tata uliyoiliza hapo juu, na tafadhali ukijibu jibu na evidence,illustration na reference Kama ulivyofanya ktk Hilo la Dar Es Salaam, hapo nimeridhika coz umesuport jibu lako na evidence. Tuendelee na la Majimaji na issue ya Kinjekitile ka unaifahamu ila with references.
Jazba lazima niwe nayo sababu Mtu unaonekana ka unajua kitu afu unazunguusha maneno kama mwanasiasa. Huku vitabu vyenyewe tunavyotumia viko shallow tena siku hizi Mna sera eti vyenye Alama ya EMAC wakati ndo vimejaa upotoshaji vingine hamtaki tuvitumie na wenye kujua ndo mapozi kibao hivi unategemea nisiwe na hasira, huku na Mimi nataka wanafunzi wangu wanione mjuvi wa mambo naejishughulisha na kusoma at least niwainspire kufikia ndoto zao katika usingizi huu wa manag'amung'amu
 
Enhee! Mkuu Zomba tuendelee nachohitaji ni majibu ya maswala tata uliyoiliza hapo juu, na tafadhali ukijibu jibu na evidence,illustration na reference Kama ulivyofanya ktk Hilo la Dar Es Salaam, hapo nimeridhika coz umesuport jibu lako na evidence. Tuendelee na la Majimaji na issue ya Kinjekitile ka unaifahamu ila with references.
Jazba lazima niwe nayo sababu Mtu unaonekana ka unajua kitu afu unazunguusha maneno kama mwanasiasa. Huku vitabu vyenyewe tunavyotumia viko shallow tena siku hizi Mna sera eti vyenye Alama ya EMAC wakati ndo vimejaa upotoshaji vingine hamtaki tuvitumie na wenye kujua ndo mapozi kibao hivi unategemea nisiwe na hasira, huku na Mimi nataka wanafunzi wangu wanione mjuvi wa mambo naejishughulisha na kusoma at least niwainspire kufikia ndoto zao katika usingizi huu wa manag'amung'amu

Watafeli ukiwasomesha nnayokupa mimi, labda wawe wanafanya thesis zao za PhD.

Ntaendelea na Majimaji, vuta subra kidogo, nimtafute mtafiti aliyeelezea vizuri kabisa hicho kisa.
 
Enhee! Mkuu Zomba tuendelee nachohitaji ni majibu ya maswala tata uliyoiliza hapo juu, na tafadhali ukijibu jibu na evidence,illustration na reference Kama ulivyofanya ktk Hilo la Dar Es Salaam, hapo nimeridhika coz umesuport jibu lako na evidence. Tuendelee na la Majimaji na issue ya Kinjekitile ka unaifahamu ila with references.
Jazba lazima niwe nayo sababu Mtu unaonekana ka unajua kitu afu unazunguusha maneno kama mwanasiasa. Huku vitabu vyenyewe tunavyotumia viko shallow tena siku hizi Mna sera eti vyenye Alama ya EMAC wakati ndo vimejaa upotoshaji vingine hamtaki tuvitumie na wenye kujua ndo mapozi kibao hivi unategemea nisiwe na hasira, huku na Mimi nataka wanafunzi wangu wanione mjuvi wa mambo naejishughulisha na kusoma at least niwainspire kufikia ndoto zao katika usingizi huu wa manag'amung'amu

Soma kwa uchache walivyofanywa mashujaa wa Majimaji:

VITA VYA majimaji "MACHINJIO" YA WAISLAMU


Nje kidogo ya mji wa Songea kuna kitongoji kinaitwa Mahenge,hapo kuna sehemu ya kumbukumbu ya vita vya Majimaji.

Jambo kubwa la mahala hapo ni Kaburi kubwa la halaiki ambamo askari zaidi ya sitini na….
walizikwa kwa pomoja.Na kando ya kaburi hilo la pomoja kuna kaburi la Ally Songea Mbano ambae yeye alizikwa peke yake.

Kwa mara ya kwanza nilitembelea makumbusho hayo mwishoni mwa mwaka 2007.

Baada ya kusaini kitabu cha wageni,na kulipa ada ya kituo,muhudumu wa kituo hicho alitupa karatasi yenye orodha ya majina ya wale wote walionyongwa na kuzikwa hapo.

ukiitazama orodha hiyo na hasa ukiwa mwislam jambo moja litakustuwa.Robo tatu ya walionyongwa na kuzikwa hapo ni waislaam .

linaanza jina lake la kiiislam, kisha kwenye mabano kuna jina la Kikristo na mwishoni linaishia jina la kiasili, mfano Abdulrahman[Dominic]Mputa Gama.

Muhudumu akatueleza kuwa hawa mashujaa wa vita vya majimaji kabla ya kunyongwa alikuwako padri ambae aliwabatiza na kuwapa majina ya kikristo na baadae kunyongwa,wengi walibatizwa kwa hadaa kuwa wakibatizwa wataachiwa huru,wote katika hao walionyongwa walikuwa ni waislam.

Uzuri ni kwamba katika orodha hiyo kulikuwa na jina na sahihi ya Yule padri aliyewabatiza, na kwa mkono wake[huyo padri] aliiyaandika hayo majina.

Karatasi yenyewe ilihifadhiwa vizuri kwenye fremu ngumu ya kioo.Tuliomba kwa nguvu zote kupatiwa hiyo karatasi ya majina hata kwa kununua lakini haikuwezekana pamoja na kuwaona wakubwa wa kituo hicho.

Niliporudi kwa mara ya pili mwezi July 2009.nilipata mstuko.

Karatasi iliyohifadhiwa kwenye fremu ngumu ya kioo,iliyokuwa na majina ya Kiislaam ya mashujaa wa vita vya majimaji,haikuwapo,na badala yake imewekwa karatasi nyingine ombayo ndani ya karatasi hiyo majina ya kiislaam ya mashujaa hao wa vita vya majimaji yameondolewa na kuachwa majina ya ubatizo na yale ya kiasili tu,jina la padri,sahihi yake na wadhifa wake katika kanisa katoliki pia vimeondolewa,na karatasi yenyewe haikuwa kwenye fremu ya kioo na ilikuwa katika fotokopi tu.

Nilimuuliza Muhudumu kulikoni? Akasema……. Songea pana mzee mmoja maarufu sana katika historia ya Tanu na historia ya kuasisiwa Bakwata anaitwa kwa kifupi M.S. Mzee huyu ana binti yake ambaye ameolewa na mzungu wa kijerumani.

Binti huyu na na mumewe wa kijerumani walikuja hapa Songea matembezi.

Hivyo kwa shinikizo la huyu mzee M.S. karatasi hiyo alipewa huyu mzungu kwa ahadi kwamba anaipeleka Ujerumani na atairudisha.

Hivyo ndio karatasi ile asilia ilivyotoweka. Kubwa katika karatasi ile ni ule ushahidi wa majina kuwa wote katika wale walionyongwa na kuzikwa hapo ni waislaam,wengi katika hao walihadaiwa kuachwa huru hivyo wakabatzwa ispokuwa wachahe sana waligoma kama shujaa Ally Songea Mbano.

Huyu kwa ushujaa wake wa kupambana na Wajerumani aligoma na akasumbua sana kiasi akanyongwa siku yake na peke yake na ndio sababu akazikwa pia peke yake.

Ukiingia ndani ya kinyumba cha ghorofa,unaanza kuona picha za mashujaa wa majimaji wakiwa wamevaa mavazi ya vita mithili ya mahujaji wanavyovaa Ihraam wakati wa hija.

kinachoongezeka kwao ni vilemba kichwani.Chini ya kila picha kuna jina la mwenye picha.Katika picha hizo majina Ukipanda gorofani utaona silaha za kijadi,mikuki,pinde,mishale,ngao,n.k.

Kinachosisimua zaidi ni mavazi ya vita.mavazi ya vita ya askari wa majimaji wengi walivaa kanzu za kiislaam na vilemba.

Jambo jingine linalosisimua ni kile ambacho watu wa kituo hicho wameandika"Rosary"[hili ni jina la kikristo,hasa la kikatoliki,ni zile shanga ambazo huning'inia msalaba]lakini unapotazama hicho kilichoitwa "Rosary" utaona si Rosary, bali ni Tasbihi hasa ya kiislaam yenye kupangika hasa shanga zake,33,33,34.maneno yaliyoandikwa kuelezea Rosary hizo ambazo ni Tasbihi ni "Hizi ni Rosary ambazo wapiganaji wa majimaji walikuwa wakitumia KUTAMBIKA kabla ya kwenda vitani kwa kuamini kwamba zitawakinga na risasi.

ukweli ni kwamba hawa askari wa majimaji wengi walikuwa ni waislaam hivyo hawakuwa WAKITAMBIKA bali walikuwa wakitumia Tasbihi hizo kufanya Dhikri kwa Allah kabla ya kwenda vitani.

Midhali sisi waislaam hatujawa tayari kuandika historia yetu kama waislaam,wanaotuandikia watapotosha na kupindisha na kutuzulia wanavyotaka.

Hapo gorofani kuna jingine la kasisimua.kuna makopo au magudulia.

Wameandika kuwa,haya ndio makopo ambayo askari wa majimaji walikuwa wakiyatumia KUNAWA kabla ya kwenda vitani[kushika udhu na sio kunawa]pia kwa kuamini kuwa maji hayo yatawakinga na Muhudumu alitueleza kuwa kumbukumbu nzuri na za uhakika ziko Jimbo kuu la Wakatoliki,Peramiho.

Tulikwenda jimboni lakini hatufanikiwa kwa sababu za ki-urasimu tu.Tulitakiwa tupate kibari cha Askofu mkuu.Hatukukipata.

Kwa yale tuliyoyaona na kuyashudia tulijifunza mambo yafuatayo:-

1.Vita vya majimaji havikuwa ni vita vya kizalendo, kwamba wazalendo walikuwa wakipigania nchi yao.La!!!Vilikuwa ni vita vya waislaam wakipigana na wakristo wa kijerumani waliovamia maeneo asilia ya waislaam kwa lengo la kuuwa uislaam na kusimamisha Kanisa.kwani mazingira yote utayoyaona ya mashujaa wa vita vya majimaji ni mazingira ya kiislaam,kingine ni kwamba hukuti mahala yalipo makaburi ya askari wa kijerumani ila katika miji ya waislaam.Kilwa.Bagamoyo.n.k.kwa nini wauliwe maeneo ya waislaam tu?walifuata nini huko?

2.kuna upotoshaji mkubwa sana wa historia ya vita vya majimaji.Vinaoneshwa kama ni vita vya wazalendo wakipigana na wakoloni wa kijerumani,wakati ukweli si hivyo.Ukweli ni kwamba vita vya majimaji vilikuwa ni vita baina ya waislaam na wakrito wa kijerumani,waafrika wakristo wa songea walijiunga na wakristo wenzao wa kijerumani dhidi ya waafrika wenzao wa kiislaam.

3.Wakristo wameitafiti hakika hii na wakaijua kisha wameificha kwa maslahi yao. MWISHO Kuna haja ya wasomi wetu wa kiislaam kufanya juhudi za makusudi za utafiti wa Historia yetu ili kukifanya kizazi hiki cha kiislaam kujitambua zaidi na kujenga ujasiri.Taasisi za kiislaam na watu binafsi[matajiri]wawawezeshe kiuchumi wasomi hawa kufanya kazi hii.

Mwaka 2008 nimetembelea Kilwa kisiwani ,huko nikamkuta mzungu wa kifaransa akiandika historia ya kilwa kisiwani akiitwaThiery,ameweka kambi na majenereta ya umeme,solar power,na makompyuta.kazi nyingine kubwa alokuwa akifanya ni kukarabati yale magofu ambayo mengi ni Misikiti na majumba ya mawe ya wafalme wa kale.

Kilwa kisiwani ni moja kati ya dola kubwa za kiislaam katika mwambao wa Afrika mashariki,ndio dola ya mwanzo kuwa na sarafu yake ambayo iliandikwa jina la Allah.

Tuliposoma kazi ile ya Yule Thiery mfaransa tayari alikwisha ipotosha kwa kiasi kikubwa.sikuwa na la kumfanya.Kizazi cha vijana wa kiislaam hakitopata historia ya kweli ya kiislaam kama tutawaacha akina Thiery waandike,na hivyo vijana wetu hawatajitambua na hawatokuwa na ujasiri katika uislam wao.


Posted by KIWENDU at Source: KIWENDU: October 2012
 
Watafeli ikiwasomesha nnayokupa mimi, labda wawe wanafanya thesis zao za PhD.

Ntaendelea na Majimaji, vuta subra kidogo, nimtafute mtafite aliyeelezea vizuri kabisa hicho kisa.

Hata mi najua lazima nifate syllabus, ktk vipindi vya clubs, kwenye club ya History ndo huwa tunakuwa na history challenging questions na maswali Kama haya huwa ndo tunayajadili na yamekuwa yakivuta wanafunzi wengi kujiunga na History club tatizo ni pale tunapokosa majibu kwa maswali Yao, tunatumia saikolojia kuwajibu though tunaona wazi hawajaridhirika tena haya nafkiri ntayaweka notice board wafanye utafiti na wao ili Alhamisi ktk clubs periods tujadili
 
Je? Kama ni hivyo na Huyo Kinjekitile Ngware anaingiaje? Kwenye story ya MajiMaji je ni kweli alikuwa great Magician? Kuna tetesi Kuwa alikuwa anafuga wanyama wa aina zote? Na je alikamatwa na Wajerumani hata Kabla ya vita? Then it means MajiMaji ilipiganwa Kuanzia sehemu za Pwani, na sio kusini tu Kama tunavyojua? Na source sio forced Labour, Taxation, na German harsh treatment if you don't mind Mkuu Zomba tuendelee.
NB. ITAKUWA NI VIZURI KAMA UKIFASIRI BAADHI YA MISAMIATI YA KIARABU SABABU SIILEWI KAMA IHRAAM!

 
zomba, naona kama umetumia nguvu kuuubwa sana kujenga hoja kwa mambo ambayo hayahitaji nguvu kubwa hivyo. Interestingly, hukusema neno 'shule' linatokana na lugha gani! Umeegemea zaidi upande wa kiarabu.

Your main point hapa ni matumizi ya neno 'kugundua au kuvumbua'. Hivi zomba, nikisema nimegundua bar moja inayochoma nyama vizuri sana ina maana hiyo bar haikuwepo kabla ya mimi kusema hivyo? Kwamba mimi niliyesema nimegundua ndiyo nimeifanya ika-exist? Au nikisema nimegundua njia ya mkato toka Magomeni kwenda Posta ina maana hiyo njia haikuwepo?

Bila 'context' utajikuta uko nje ya mambo all the time! Na shida yako hapa ni wazi iko kwenye translation - unafanya direct translation.

Mtu anaposema amegundua (discovered) inabidi uangalie anaongelea katika context gani. Vasco De Gama aligundua uwepo wa sehemu mbalimbali including what we now call Tanzania. Kwa 'audience' yake yeye Vasco De Gama, ni wazi hawakuwa wanajua uwepo wa sehemu hiyo. Na kugundua sehemu si lazima ukanyage mahali hapo kwa miguu yako! Labda nikuulize, unajuwa kuwa kuna nchi inaitwa Tonga? Uligunduaje?

Kwa kumalizia, I have discovered JF ina member anaitwa zomba!
 
Bado niko na wewe Mkuu Zomba tueendelee,
Vipi kuhusu mji wa Kilwa ningependa kujua haya
1. Kama Kilwa ndo ulikuwa mji wa kwanza kustaarabika Afrika Mashariki?
2. Wageni wa kwanza kufika hapo ni wachina au waarabu ilikuwa Karne ya ngapi?
3. Sababu za kuporomoka dola ya Kilwa ni zipi?
4. Wenyeji wa hapo walikuwa Kabila gani?
5. Role ya Kilwa ktk long distance trade na kwa nini Mjerumani aliopt Bagamoyo instead ya Kilwa
6. Kwa nini kwa Sasa Kilwa iko nyuma? Unafkir Kuwa kwake nyuma kuna sababu za kihistoria?
7. Je uhusiano wa Kilwa na miji mingine ya Pwani ilikuwaje?
 
ikiwezekana na maana ya majina ya miji Kama Mogadishu, Galla, Mombasa,Lamu, Malindi, Kismayu, Zanzibar, Kilwa na Sofala.. Bagamoyo nil ishafika nikiwa chuo nikipata maana yake halisi
 
Nimepoteza muda wangu kufuatilia sentensi moja baada ya nyingine nikitaraji kuona application ya neno 'UBAGUZI' nisiipate.

Sidhani kama zomba unaelewa neno ubaguzi maana yake. Kikubwa nachokiona hapa ni kutaka kwako watu wajue kuwa Muarabu alifanya hiki na kile na naamini hilo lingeujaza moyo wako furaha. Lkn sitaacha kukwambia kuwa umejikanyaga na kuonesha udhaifu wako ktk kila sentesi. Utangulizi usioelewa na mada isiyoendana na kichwa cha habari.

Chukulia mfano huu; 'Mkwawa aliandika kwa Kiarabu japo aliandikiwa'. Sasa sioni haja ya kututukana ikiwa hatukuoneshwa barua hizo au nyaraka alizoandikiwa kwa kiarabu. Na wewe mwenyewe unakiri kuwa ALIANDIKIWA. Sasa sijui huo kwako ni uvumbuzi au ujemedari wa mdomo ulio katika kichwa kisicho na ubongo.

Labda mimi nirukie kwenye kile kilicho moyoni mwako, manake reading between the lines, umeshindwa kukiweka kwenye maandishi kwa kudhani tutaifahamu nia yako ambayo tayari mimi nimeifahamu.

Ili Historia iwekwe, mambo fulani lazima yafanyike. Leo hii, Warusi, Wamarekani, Wajapan, Wachina na wengineo wanaofanya mavumbuzi kwenye anga za juu na sayari nyingine wanapoenda huko, hawaendi na kurudi kisha kuandika magazetini kuwa walienda. Huacha kitu cha kumbukumbu huko, bendera, maandishi n.k na ndio maana hawatumii nguvu kubwa kujitangaza kwa mdomo.

Uwepo wa Mwarabu katika Pwani ya Afrika Mashariki hamna anayeukataa, lkn haukuwa well documented kwa kuwa hakuwa na something remarkable and acknowledge-able kwenye ground. Huna haja ya kututukana ikiwa Historia ya Mpendwa wako imefutika ndani yetu. Binadamu huamini zaidi akionacho, na hicho humkaa moyoni. Ndio maana Mpendwa wako Muarabu tunamuamini kwa Bakaburi ya Bagamoyo (Kaole) kwani tunayaona.

Linapokuja suala la popularity, hakuna kulazimishana. Huyu Mzungu unayeona wewe (kwa mtazamo wako) kuwa ndio katufundisha UJINGA, ndio huyo huyo ametufundisha kusoma na kuandika kwa lugha hii unayopostia matusi juu yetu. Sasa sijui unapata wapi wazimu wa kututukana kuwa hatujui Mkwawa aliandikiwa Kiarabu ilhali hata huyo Mkwawa hakujua Kiarabu.

Labda nipunguze maneno kwa kukwambia kwamba; UMECHEMKA. Unatulazimisha kukumbuka wafu ilhali tunao wazima ambao elimu na mafundisho yao yanatusaidia na kutuongoza mpaka leo. Nitamuonesha mwanangu Shule walizojenga Wajerumani na Waingereza na kuwasimulia juu ya makaburi ya waarabu.

Masimulizi yangu juu ya makaburi ya waarabu yatabaki kuwa hadithi kwao kwani hatuna kazi na makaburi lkn shule walizoacha Wamisionari hazitabakia hadithi, wataingia humo kusoma na hilo litakaa akilini mwao kuliko makaburi, hata uhubiri vipi.

Kwa akili za namna hii, mmoja wenu alisema kuwa ni Waislamu ndio walimnunulia Nyerere suruali yake ya kwanza ndio akaja kupigania Uhuru.

Na naomba nikukumbushe Mkuu zomba, wewe ni mfano mzuri unapozungumziwa UJINGA. Ndani ya wiki hii tu iliyoisha ulituandikia hapa kuwa miaka fulani nyuma Zanzibar iliitawala Oman.
 
Last edited by a moderator:
Nina threads humu nilianzisha nikizungumzia maana ya Daresalaam
i wonder kama umewahi zisoma
 
zomba, siku zote weka akilini mwako kuwa kukielewa kitu hutofautiana baina ya mtu na mtu. Tunatofautiana uelewa kutokana na mambo mengi. Ndio maana wewe kwa akili na uwezo wako wa kufikiri, juzi hapa ulibandika kituko kuwa Zanzibar iliitawala Oman. Kwa mtu mwenye kuelewa hasa kilichotokea, Zanzibar haikuitawala Oman, bali Sultan wa Oman alihamishia HQs zake Zanzibar.

Nimesoma bandiko nukuu lako kuhusu vita vya maji maji na kama nilivyochelea mwanzo kwenye post yangu ya kwanza, harufu ya Udini inanuka kwenye kila unachoandika JF. Kuna ujinga umejificha kwenye udini wako unakufanya unashindwa kuyaelewa mambo na unathubutu kuwa muongo ili tu ufanikiwe kuwashawishi wengine wasiofikiri.

Hebu jiulize hili ndugu yangu uliyeharibika; Kama vita ya Maji Maji ilipiganwa na kuongozwa na watawala wa temi za pwani ambao wameongoza jamii za Waislamu, ulitarajia kuona Wakristo huko? Unataka kuniambia kuwa Maji Maji ingepiganwa Kilimanjaro, ilipaswa kuitwa vita ya Wakristo dhidi ya Wazungu?

Hamna anayebisha kuwa Maji Maji ilipiganwa na Waislamu zaidi kwa kuwa ilipiganwa Pwani ambako kuna waislamu. Sasa hizi habari zingine za kutunga eti kulikuwa na karatasi ikapelekwa Ujerumani n.k ni utoto wa kijinga. Ideology ya Maji Maji War ilifeli kwa mtindo ule ule wa Kuran ya Mbagala na hapo hamna haja ya kulihusisha kanisa Katoliki katika kila kushindwa kwako.

Kila mtu hutafsiri jambo kwa maono yake bwana. Kama kuna sehemu ya Jamii yetu ilijiegemeza kwa Wajerumani basi ilikuwa ni kwa sababu ya yale ambayo waliamini toka kwa Mjerumani huyo. Wao ukiwauliza what was all about Maji Maji war, watasema kuwa kuna watu walianzisha uprising kwa kuwa hawataki shule (mfano).

Sasa wewe umeleta ujinga wako wa dini kwenye kila jambo. Sidhani kama Waafrika wote waliwapenda waarabu ukiweka akilini kuwa walikuwa notorious wa kuwakamata watumwa kuwauza sokoni Zanzibar, lkn kumbuka ni hao hao ndio walileta Uislam ambao wewe unataka kuniaminisha eti ulikuwa ukombozi kwa kuwa ulipingana na Mjerumani.

If that is so, na mimi nita-conclude kuwa, Majimaji haikuwa vita ya kuipigania nchi, bali ilikuwa vita ya watu wa Pwani kupinga Ukristo uliokuwa unaletwa na Mjerumani na mimi nikaandike vitabu vyangu na kuwafundisha watoto otherwise.

Labda unijibu swali hili moja: Ikiwa kiongozi wa Majimaji aliwaambia watu kuwa twendeni tukapigane vita kwa imani kwamba risasi zitageuka maji na baadhi wakagoma wakiamini mawazo hayo ni ya kijinga, kuna haja ya kuwalaumu kutoshiriki kwao?

Jibu swali hilo ukizingatia kuwa ni mambo haya haya ya kijinga yametuletea mtafaruku Mbagala juzi tu hapa
 
Last edited by a moderator:
Mkuu zomba nilikuwa Nafikiri unazungumzia udini nikafungua hii thread kwa kasi nikiwa tayari na jibu la kukupa lakini nimeisoma sijaielewa ulitaka kusema nini Ngoja nitimke nikalinde kura Huku darajani usinipotezee muda na thread yako ili muibe kura vizuri
 
Last edited by a moderator:
Nimepoteza muda wangu kufuatilia sentensi moja baada ya nyingine nikitaraji kuona application ya neno 'UBAGUZI' nisiipate.

Sidhani kama zomba unaelewa neno ubaguzi maana yake. Kikubwa nachokiona hapa ni kutaka kwako watu wajue kuwa Muarabu alifanya hiki na kile na naamini hilo lingeujaza moyo wako furaha. Lkn sitaacha kukwambia kuwa umejikanyaga na kuonesha udhaifu wako ktk kila sentesi. Utangulizi usioelewa na mada isiyoendana na kichwa cha habari.

Chukulia mfano huu; 'Mkwawa aliandika kwa Kiarabu japo aliandikiwa'. Sasa sioni haja ya kututukana ikiwa hatukuoneshwa barua hizo au nyaraka alizoandikiwa kwa kiarabu. Na wewe mwenyewe unakiri kuwa ALIANDIKIWA. Sasa sijui huo kwako ni uvumbuzi au ujemedari wa mdomo ulio katika kichwa kisicho na ubongo.

Labda mimi nirukie kwenye kile kilicho moyoni mwako, manake reading between the lines, umeshindwa kukiweka kwenye maandishi kwa kudhani tutaifahamu nia yako ambayo tayari mimi nimeifahamu.

Ili Historia iwekwe, mambo fulani lazima yafanyike. Leo hii, Warusi, Wamarekani, Wajapan, Wachina na wengineo wanaofanya mavumbuzi kwenye anga za juu na sayari nyingine wanapoenda huko, hawaendi na kurudi kisha kuandika magazetini kuwa walienda. Huacha kitu cha kumbukumbu huko, bendera, maandishi n.k na ndio maana hawatumii nguvu kubwa kujitangaza kwa mdomo.

Uwepo wa Mwarabu katika Pwani ya Afrika Mashariki hamna anayeukataa, lkn haukuwa well documented kwa kuwa hakuwa na something remarkable and acknowledge-able kwenye ground. Huna haja ya kututukana ikiwa Historia ya Mpendwa wako imefutika ndani yetu. Binadamu huamini zaidi akionacho, na hicho humkaa moyoni. Ndio maana Mpendwa wako Muarabu tunamuamini kwa Bakaburi ya Bagamoyo (Kaole) kwani tunayaona.

Linapokuja suala la popularity, hakuna kulazimishana. Huyu Mzungu unayeona wewe (kwa mtazamo wako) kuwa ndio katufundisha UJINGA, ndio huyo huyo ametufundisha kusoma na kuandika kwa lugha hii unayopostia matusi juu yetu. Sasa sijui unapata wapi wazimu wa kututukana kuwa hatujui Mkwawa aliandikiwa Kiarabu ilhali hata huyo Mkwawa hakujua Kiarabu.

Labda nipunguze maneno kwa kukwambia kwamba; UMECHEMKA. Unatulazimisha kukumbuka wafu ilhali tunao wazima ambao elimu na mafundisho yao yanatusaidia na kutuongoza mpaka leo. Nitamuonesha mwanangu Shule walizojenga Wajerumani na Waingereza na kuwasimulia juu ya makaburi ya waarabu.

Masimulizi yangu juu ya makaburi ya waarabu yatabaki kuwa hadithi kwao kwani hatuna kazi na makaburi lkn shule walizoacha Wamisionari hazitabakia hadithi, wataingia humo kusoma na hilo litakaa akilini mwao kuliko makaburi, hata uhubiri vipi.

Kwa akili za namna hii, mmoja wenu alisema kuwa ni Waislamu ndio walimnunulia Nyerere suruali yake ya kwanza ndio akaja kupigania Uhuru.

Na naomba nikukumbushe Mkuu zomba, wewe ni mfano mzuri unapozungumziwa UJINGA. Ndani ya wiki hii tu iliyoisha ulituandikia hapa kuwa miaka fulani nyuma Zanzibar iliitawala Oman.

Umesema mengi lakini yote yanaelekea katika ule ule muondelezo wa Ubaguzi wa ujinga.

Kuhusu Mkwawa, iwe ameadika mwenyewe au ameandikiwa hilo si tatizo. Kwani leo hii hata mimi siyaandikia haya, kompyuta inaniandikia. Upo hapo ulipo, ni mawazo yangu yanahitimishwa na njia ya kiteknolojia, wakati wa uchache wa teknljia kulikuwa kuna watu wanaitwa "scribes" kazi yao ilikuwa ni kuwaandikia wenye mawazo ya kuandika iwe barua au risala. Ndiyo maana nikatumia maneno yote mawili, nikajuwa kuna kina wewe humu watakuja na hoja dhaifu kuhusu hilo.

Kuhusu Zanzibar kutawala Oman, nilikuwekea na ushahidi kuwa jina Zanzibar halikuanzia unapofikiria wewe, sijui umeshasoma kuhusu Zenj Empire? sijui umeshasoma kuhusu utawala wa Mfalme Suleiman, au unausikia tu. Sijui umeshasoma kuhusu watu wa Tembo? sijui hta kama umeshasoma kuhusu Arusha na jina hilo lina maana ipi, licha ya kukupeleka mbali sana. Bado ungali mchanga katika historia na inakubidi usome sana, elimu haina mwisho na haianzii wala kuishia ndani ya kuta nne.

Nadhani historia kwako ni ile nnayoiongelea mimi ya Ubaguzi wa Ujinga.

Nna uhakika hata maana ya sentensi hiyo itakuchanganya sana.

Nakuuliza hivi, unajuwa kuwa baadhi ya bara Asia lilitawaliwa na Malkia wa kutoka Kontinenti hili la Afrika? kwa jina akiitwa Bilqis au Balqis? unajuwa utawala wake ukiitwaje? ukipata jibu, njoo tuongee kuhusu Zanzibar na Oman ni nani alimtawala mwenzake mwanzo.
 
Hapana soma vizuri poat namba moja na zinafoatatia, utaelewa kuwa sikumaanisha "ubaguzi wa kijinga". Nimemaanisha haswa mada "Watanzania na Ubaguzi wa Ujinga".

Utaishia kujibu tusentensi tudogo na kukimbia mada yako mwenyewe. Huyo keshaelewa, jibu hoja zangu nipate kukuelewa pia.
 
Back
Top Bottom