zomba
JF-Expert Member
- Nov 27, 2007
- 17,240
- 3,910
Naamini na nnadiriki kuandika kuwa Watanzania ni wabaguzi, ubaguzi wao si wa kidini au wa kijinsia au wa kikabila au wa rangi. Hizo ndio njia kuu zijulikanazo za ubaguzi duniani.
Watanzania, wengi wao, hawana kabisa ubaguzi huo. Ubaguzi wa Watanzania ni wakijinga au wa ujinga. Naamini kabisa kuwa ubaguzi wa Watanzania ni wa ujinga zaidi ya wakijinga. Ujinga hawana ila wana ubaguzi wa ujinga.
Ikiwa Watanzania hawana ujinga, huu ubaguzi wa ujinga wameutowa wapi? nna uhakika kuwa huu ubaguzi wamepachikwa na Waalimu wao na Waalimu wao walipachikwa na Waalimu wao na hao Waalimu wao walipachikwa huu ujinga walipojengewa mashule na kusomeshwa na kufundishwa cha kuja kuwafundisha hao waliotarajiwa kuwa ndio watakuja kufundisha, matokeo wamewajaza Watanzania ubaguzi wa ujinga.
Mara kadhaa humu JF nimekuwa nikitumia sentensi "uneducated fool from an uneducated school", nna uhakika wanaonisoma humu JF wameshaisoma sentensi hiyo, si mara moja wala mbili, wako walioielewa wakakaa kimya na wako walioielewa wakashindwa kuielewa na wakaanza kung'aka kuwa hilo si neno la kueleweka. Sina haja ya kulielewesha kwani, muelewa huelewa haeleweshwi. Asiyeelewa hutaka kuelewa na huuliza ili aelewe wala hataharuki na kujifanya anajuwa asichokijuwa, moja ya ubaguzi wa ujinga.
Ubaguzi mwengine wa ujinga tuliokuwa nao na uliojazwa vichwani mwa wengi ni kuwa Vasco Da Gama ndio kaivumbuwa hii Tanzania au Tanganyika wakati ukweli ni kuwa wakati wa Vasco Da Gama jina Tanzania halikuwepo wala Tanganyika halikuwepo. Kuna anaelipinga hili? Anza.
Isitoshe, Vasco Da Gama hajawahi kuikanyaga ardhi ya nchi hii, ambayo leo inaitwa Tanzania (jina aliloipa Muhindi wa Tanga). Vasco Da Gama aliishia baharini alipotia nanga manuwari zake, hajashuka wala kuigusa hii ardhi ambayo wengi wanajazwa ujinga wa kusema kuwa Vasco Da Gama ndio mvumbuzi. Swali la kujiuliza, Jee, Vasco Da Gama alivumbuwa kipi? alimkuta nani hapo Kilwa? (Naomba wajuzi wanipe maana ya neno "Kilwa") labda hilo ni neno la Kireno? kwa kuwa umeaminishwa kuwa Vasco Da Gama kapavumbuwa? au maana ya jina (au neno) Sofala, zilipotuwa kwanza manowari zake, ambako alipewa nahodha kipofu akamuongoza hadi Kilwa. Ndio kipofu. Ni ajabu lakini kweli.
Jee, hayo mmeyasoma huko mnakojazwa ujinga? Ni wangapi leo hii wanaojuwa kuwa hapa katika Ardhi hii kulikuwa kuna mji, kama si nchi, inayoitwa Raptha? Hii Raptha iko wapi? ilianza lini na nani walikuwa Watawala? na imeshia wapi? Maweee!
Nani leo hii anaejuwa kuwa Majimaji ilikuwa ni vita isiyokubalika na wengi leo hii?
Nani anaejuwa kuwa Mkwawa alikuwa anaandika Kiarabu, japo kuandikiwa?
Nani leo hii anaekiri kuwa nchi hii ina mbegu na si shina au tawi tu la Uarabu, la hasha, si nchi hii, Kontinenti hili? Nakuhakikishia hakuna. Kwanini hakuna? ni Ubaguzi wa ujinga.
"Afrika" ni lugha gani, au neno? tuseme jina hilo? vyovyote, iwavyo na iwe, limetokana na lugha gani uijuwayo wewe? zaidi ya neno au jina "Afrit"? kama huna zaidi ya hapo basi ujuwe umejazwa ujinga.
Dar Es Salaam. ni lugha ipi na neno hilo linatoka wapi? anaekuambia ni "Bandari Salama" basi huyo kakujaza ujinga kwani si maana yake ya ukweli.
Arusha, unajuwa maana yake? na neno hilo limetoka wapi? hali kadhalika Tanga? Tabora? Morogoro? Ruaha? Mbeya? Shinyanga? Zanzibar?
Kama huyajui yote hayo basi ujuwe umejazwa ujinga wa ubaguzi wa ujinga. Hakuna zaidi.
Tujadiliane.
Watanzania, wengi wao, hawana kabisa ubaguzi huo. Ubaguzi wa Watanzania ni wakijinga au wa ujinga. Naamini kabisa kuwa ubaguzi wa Watanzania ni wa ujinga zaidi ya wakijinga. Ujinga hawana ila wana ubaguzi wa ujinga.
Ikiwa Watanzania hawana ujinga, huu ubaguzi wa ujinga wameutowa wapi? nna uhakika kuwa huu ubaguzi wamepachikwa na Waalimu wao na Waalimu wao walipachikwa na Waalimu wao na hao Waalimu wao walipachikwa huu ujinga walipojengewa mashule na kusomeshwa na kufundishwa cha kuja kuwafundisha hao waliotarajiwa kuwa ndio watakuja kufundisha, matokeo wamewajaza Watanzania ubaguzi wa ujinga.
Mara kadhaa humu JF nimekuwa nikitumia sentensi "uneducated fool from an uneducated school", nna uhakika wanaonisoma humu JF wameshaisoma sentensi hiyo, si mara moja wala mbili, wako walioielewa wakakaa kimya na wako walioielewa wakashindwa kuielewa na wakaanza kung'aka kuwa hilo si neno la kueleweka. Sina haja ya kulielewesha kwani, muelewa huelewa haeleweshwi. Asiyeelewa hutaka kuelewa na huuliza ili aelewe wala hataharuki na kujifanya anajuwa asichokijuwa, moja ya ubaguzi wa ujinga.
Ubaguzi mwengine wa ujinga tuliokuwa nao na uliojazwa vichwani mwa wengi ni kuwa Vasco Da Gama ndio kaivumbuwa hii Tanzania au Tanganyika wakati ukweli ni kuwa wakati wa Vasco Da Gama jina Tanzania halikuwepo wala Tanganyika halikuwepo. Kuna anaelipinga hili? Anza.
Isitoshe, Vasco Da Gama hajawahi kuikanyaga ardhi ya nchi hii, ambayo leo inaitwa Tanzania (jina aliloipa Muhindi wa Tanga). Vasco Da Gama aliishia baharini alipotia nanga manuwari zake, hajashuka wala kuigusa hii ardhi ambayo wengi wanajazwa ujinga wa kusema kuwa Vasco Da Gama ndio mvumbuzi. Swali la kujiuliza, Jee, Vasco Da Gama alivumbuwa kipi? alimkuta nani hapo Kilwa? (Naomba wajuzi wanipe maana ya neno "Kilwa") labda hilo ni neno la Kireno? kwa kuwa umeaminishwa kuwa Vasco Da Gama kapavumbuwa? au maana ya jina (au neno) Sofala, zilipotuwa kwanza manowari zake, ambako alipewa nahodha kipofu akamuongoza hadi Kilwa. Ndio kipofu. Ni ajabu lakini kweli.
Jee, hayo mmeyasoma huko mnakojazwa ujinga? Ni wangapi leo hii wanaojuwa kuwa hapa katika Ardhi hii kulikuwa kuna mji, kama si nchi, inayoitwa Raptha? Hii Raptha iko wapi? ilianza lini na nani walikuwa Watawala? na imeshia wapi? Maweee!
Nani leo hii anaejuwa kuwa Majimaji ilikuwa ni vita isiyokubalika na wengi leo hii?
Nani anaejuwa kuwa Mkwawa alikuwa anaandika Kiarabu, japo kuandikiwa?
Nani leo hii anaekiri kuwa nchi hii ina mbegu na si shina au tawi tu la Uarabu, la hasha, si nchi hii, Kontinenti hili? Nakuhakikishia hakuna. Kwanini hakuna? ni Ubaguzi wa ujinga.
"Afrika" ni lugha gani, au neno? tuseme jina hilo? vyovyote, iwavyo na iwe, limetokana na lugha gani uijuwayo wewe? zaidi ya neno au jina "Afrit"? kama huna zaidi ya hapo basi ujuwe umejazwa ujinga.
Dar Es Salaam. ni lugha ipi na neno hilo linatoka wapi? anaekuambia ni "Bandari Salama" basi huyo kakujaza ujinga kwani si maana yake ya ukweli.
Arusha, unajuwa maana yake? na neno hilo limetoka wapi? hali kadhalika Tanga? Tabora? Morogoro? Ruaha? Mbeya? Shinyanga? Zanzibar?
Kama huyajui yote hayo basi ujuwe umejazwa ujinga wa ubaguzi wa ujinga. Hakuna zaidi.
Tujadiliane.