Alloyce PR
JF-Expert Member
- Nov 15, 2020
- 704
- 801
"Heela! Itafakari nchi inayoinua mkono na kumwaga damu ya Mwafrika mwenzake, kwa kisingizio dhaifu kuwa mgeni anachuma matunda ya ardhi ambayo wao wameshindwa kuituliza. Ni fedheha kuona ubaguzi ukigeuzwa kuwa vazi la sifa.
Afrika Kusini imevaa kilemba cha ujinga kilichofunika macho ya utu wao. Sisi tubaki tukiipenda Tanzania yetu kwa dhati; tuache majivuno ya dharau yanayotokana na kutembea miji ya ughaibuni. Huko mlikokuwa mkibeba maboksi na kufanya kazi za suluba kwa wakoloni. Inasikitisha unaporejea nyumbani na kumwaga maneno ya hovyo, ukiwa umening'iniza hereni masikioni kama ndama aliyepotea zizini." — Alloyce, P.R.
Afrika Kusini imevaa kilemba cha ujinga kilichofunika macho ya utu wao. Sisi tubaki tukiipenda Tanzania yetu kwa dhati; tuache majivuno ya dharau yanayotokana na kutembea miji ya ughaibuni. Huko mlikokuwa mkibeba maboksi na kufanya kazi za suluba kwa wakoloni. Inasikitisha unaporejea nyumbani na kumwaga maneno ya hovyo, ukiwa umening'iniza hereni masikioni kama ndama aliyepotea zizini." — Alloyce, P.R.