Warioba hamuwezi Wassira kipenzi cha wanaBunda
Hawakujuwa kuweka misingi bora ya kuiendesha nchi walipopewa dhamana ya kuijenga hii nchi, fikiri miaka yote ya Nyerere madarakani life expectancy ya Mtanzania haijafika miaka 45.
Nyerere anaondoka sisi ni masikini wa mwisho duniani.
Na hawa kina Warioba ndiyo waliokuwa watendaji, wakati wa Mwinyi huyu alikuwa Waziri Mkuu hakuweza kufanya au kubadili lolote. Hajaishia hapo, Mkapa anaondoka maradakani Tanzania bado tupo kwenye tano hoi za umasikini duniani.
Leo eti anataka kuaminisha watu kuwa ule ujinga wake mwenyewe alioujaza kwenye mapendekezo ya katiba ndiyo bora.
tena nililaumu sana Kikwete alipompa huyu mzee ile kazi, nilisema hivi huyu alifanya nini alipokuwa na wadhifa Tanzania hii hata leo aweze kukusanya maoni vyema? sikupata jibu lenye maana, watu wakaishia kuhororoja na kubwabwaja bila mpango.
Kama si kunikosea huko ni nini? wewe hayakuumizi hayo?

Cha kushangaza kuna watu wanapiga simu wanadai eti ni kuchafuana.Mimi naamini kama kweli hukumu hiyo ipo,basi huu ndio uandishi tunaoutaka maana watu wanajinadi kuwa ni wassfi hivyo vyomba vya habari vinapswa kuueleza ummma ukweli kuhusu hawa watu.Jamhuri wamefanya vyema tu wawapitie na wengine kuangalia historia zao
Kuna mtu aliandika hiviii "CCM ni Kamafamilia lazima wawe na DNA za kufanana na hao wote ni familia moja hawaweziwakatofautiana. Ni ngum dada kusema kaka anakomba mboga wakati nae anajuaatasemwa ni kikojozi. Pole zao wanaojiita wasafi na kukaa ndani ya jalala latakataka na kutaka wasichafuke" ni suala la muda tu tutaona mengi! By the way hivi Mako ana msimamo gani na hii katiba yao wanayotaka ipiteGazeti la JAMUHURI limeripoti kuwa Wassira ni mla rushwa na Mhariri wa gazeti hilo, bwana Manyerere amedai kuwa alipatikana na hatia hiyo Mahakama Kuu na hata alipokata rufaa,rufaa yake ilitupwa na Mahakama ya Rufaa na Mhariri huyo akihojiwa na Channel 10 asubuhi hii akiwa nje ya nchi, amesema nakala ya hukumu ipo.Kichwa cha habari katika gazeti hilo kinasomeka "Wasira mla rushwa".
Hiyo ilikuwa ni kesi iliyotokana na maswala ya uchaguzi miaka ya 90.
Fuatilia Channel 10 mjadala unaendelea.
My take;
Kama sikosei,mtu yoyote aliepatikana na hatia mahakamani kwa kosa lolote la jinai, bssi anapoteza sifa ya kugombea uraisi wa Jamuhuri wa Muungano wa Tanzania.
Kama kweli hukumu hiyo ipo kama gazeti linavyodai,huyu mh. imekula kwake.
Kazi imeanza.
Hahaaa toipic inanusu saa kuwa closednitarudi baadaye