Wasomi wahoji ububu wa UKAWA bungeni

Tz ndio nchi pekee ambayo wadomi wake hawatofautiani na wasio wasomi, msomi akikomenti hatofautiani na asiye msomi, wasomi wanatoa comment zao kwa kulinda matumbo yao,
 
Mimi nilishauliza tanzania kuna wasomi? sikupata jibu nilijikita kwenye PHD ya jamaa, aliwezaje kuiwasilisha kwa lugha asiyoimudu hapo chuo kikuu napo jipu hapo. Mleta uzi anasema wasomi wahoji wepi hao, hawa mchana dw anasema hivi jioni bbc anasema sivyo au huyu mtani wangu mhaya mpiga debe wa ccm ana bahati mbaya ya kutopewa cheo. Magu si mumpe dk bana angalau ubalozi mbona kawabeba mpaka basi
 
Bora wakae kimya tu maana hatuna tena uwezo wa kufatilia majadiliano ya bunge.
 
Dokta Bana Kichwa maji kweli, unasema wamegeuka bubu, hapo hapo unajibu hoja zao, hizo hoja zilitolewa ndotoni au makalioni? HOVYO KABISA NA MPUUZI WA MWISHO.

Bashiru na Bana swali langu kwenu, Wananchi wapi hao? Wanawaona kupitia RAMLI? Au Vikao vya Bunge vinafanyikia Uwanja wa Jamuhuri Dodoma hivyo Wananchi wanawaona?
Mnajificha gizani halafu mnasema mnaonekana? Nyie mlitafakari kweli kabla ya maoni haya ya Kipuuzi?

Hakuna excuse yoyote linapokuja suala la Sheria. Sheria ikisema imesema. Unakiuka Sheria lakini unataka waliokiuka Sheria Wakutane na Sheria? Kwa nini watu wanavaa miwani ya mbao na kuishi kwa ushabiki? Kukiuka Sheria katika kuwashughulikia waliokiuka Sheria ni kuwapa nafasi nzuri ya kujitetea na kuishinda serikali mbele ya Sheria maana Sheria inahitaji kufuata Sheria kwa Waovu, hili nalo ni gumu? The current cheap popularity will cost this nation very soon, hapo ndipo mtakapoelewa!
Nchi hii msomi na asiye msomi hawana tofauti wala huwezi kuwatambua kwa kupima michango yao ktk jamii
 
Pole sana ndg najua bado upon kwenye g
Mtu akikuambia jambo la kijinga na ukamwamini atakudharau- by JK Nyerere.
CCM imewaona wajinga sana baada ya kuwalisha uongo nanyi kama mazuzu mkaamini. UKAWA hawajapinga kununua dawati au dawa, wao wanazungumzia taratibu kufuatwa kama sheria inavyosema tatizo likowapi?
Mbona mnaruhusu CCM iwadharau hivyo kwa kusadiki ujinga?
Tafuta hata wa bunge wa CCM wenye kujielewa watakufahamisha kuwa kuna makosa ila kwa vile hawaruhusiwi na chama chao kukosoa wanaumia moyoni tuu na kujiona watumwa
giZa totoro
 
UAMUZI wa Kambi ya Upinzani bungeni kuingia katika vikao vya Bunge na kugeuka bubu wakati wa mjadala wa Hotuba ya Ofisi ya Waziri Mkuu, umechukuliwa kwa hadhari kuwa unaweza kusababisha kambi hiyo ionekane inalinda posho bungeni.

Hadhari hiyo imetolewa na wasomi na viongozi mbalimbali waliozungumza na gazeti hili jana, walipokuwa wakitoa maoni kuhusu uamuzi wa kambi hiyo kususa hotuba hiyo.

Dk Bana

Mhadhiri wa fani ya siasa na utawala katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk Benson Bana, ndiye aliyesema kuwa kama uamuzi huo wa kuwa bubu bungeni hautabadilishwa, kambi hiyo itaonekana inalinda posho na kwamba haipo kwa ajili ya kutetea wananchi.

“Kazi yao ni kuwakilisha wananchi na makundi yote bungeni, sasa kitendo cha kuota ububu na kushindwa kueleza kero za wananchi, ni kutotendea haki wananchi maana ni vema wakae bungeni na kutoa hoja zao la sivyo, itafika wakati watatuomba radhi wananchi,” alisisitiza.

Akizungumzia hoja ya kwanza ya Mwenyekiti wa kambi hiyo, Mbunge wa Hai, Freeman Mbowe (Chadema), kulalamikia muundo wa Serikali kutowekwa gazetini, Dk Bana alihoji kama Mbowe hajui kuwa muundo wa Serikali hautolewi kwa kila mtu.

Kuhusu suala la fedha zilizokatwa katika Mfuko wa Bunge na kuelekezwa katika utengenezaji wa madawati, Dk Bana aliwashangaa wawakilishi hao wa wananchi wanaopingana na uamuzi wa kumuinua mwananchi wa kawaida.

Alisema wananchi wote walipendezwa na hatua hiyo ya Serikali ya kuchukua fedha zilizotoka bungeni baada ya kubana matumizi na kupeleka katika kununua madawati.

“Hatua hii ni kielelezo kuwa Bunge lilikuwa likipangiwa fedha nyingi kuliko matumizi yake hivyo kusababisha kuwepo matumizi ya hovyo, sasa viongozi wa Bunge kuliona hilo na kurejeshwa kwenye jamii ni jambo jema,” alisema.

Alionya kuwa mikakati ya kambi ya upinzani, ni kutetea wananchi lakini kwenye hilo wananchi wenyewe kila kona wanawashangaa kwani inaonesha kutetea maslahi ya wabunge.

Bashiru Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Bashiru Ally alisema wananchi wanaangalia vitendo vya wabunge wao ndani ya Bunge na watawahukumu kwani michango yao ndani ya Bunge ni muhimu na njia ya kutatua tatizo si kususa, bali kufuata taratibu za kisheria.

Alisema uamuzi wa kutozungumza, unaondoa maana ya vyama vya upinzani ndani ya Bunge kwa kuwa watashindwa kujadili masuala yenye manufaa ya wananchi, kwani mawazo ya kiongozi wa upinzani bungeni ni muhimu na yanawekwa kwenye kumbukumbu.

“Kuwekwa kwenye kumbukumbu mawazo hayo ni kwa ajili ya vizazi vijavyo, sasa kitendo cha Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni kutumia vibaya nafasi anayopewa, ni udhaifu wa kimkakati,” alisisitiza Bashiru.

Shehe Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salum, alisema wanavyofanya wapinzani ni jambo lisilopendeza katika kuleta umoja wa kitaifa, kwani wao ni wawakilishi wa wananchi ndani ya Bunge na kususa siyo jambo la kiungwana.
Mlitaka wafanyeje? waongee ili Muwaite FFU? .... Bora wakae kimya waangalie FUTUHI la CCM kwa Raha zao ...
 
Shida kubwa pia ambayo ukawa inawapa shida ni aina ya viongozi wakuu wa chama siyo aina ya viongozi wenye upeo mpana wa kufikiri na kuibua agenda za msaada kwa jamii katika ujenzi wa jamii mpya.
Elimu yako ya Ngumbaro haijakusaidia sana mkuu
 
Back
Top Bottom