Wasomi wahoji ububu wa UKAWA bungeni

singidadodoma

JF-Expert Member
Nov 11, 2013
4,394
1,531
UAMUZI wa Kambi ya Upinzani bungeni kuingia katika vikao vya Bunge na kugeuka bubu wakati wa mjadala wa Hotuba ya Ofisi ya Waziri Mkuu, umechukuliwa kwa hadhari kuwa unaweza kusababisha kambi hiyo ionekane inalinda posho bungeni.

Hadhari hiyo imetolewa na wasomi na viongozi mbalimbali waliozungumza na gazeti hili jana, walipokuwa wakitoa maoni kuhusu uamuzi wa kambi hiyo kususa hotuba hiyo.

Dk Bana

Mhadhiri wa fani ya siasa na utawala katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk Benson Bana, ndiye aliyesema kuwa kama uamuzi huo wa kuwa bubu bungeni hautabadilishwa, kambi hiyo itaonekana inalinda posho na kwamba haipo kwa ajili ya kutetea wananchi.

“Kazi yao ni kuwakilisha wananchi na makundi yote bungeni, sasa kitendo cha kuota ububu na kushindwa kueleza kero za wananchi, ni kutotendea haki wananchi maana ni vema wakae bungeni na kutoa hoja zao la sivyo, itafika wakati watatuomba radhi wananchi,” alisisitiza.

Akizungumzia hoja ya kwanza ya Mwenyekiti wa kambi hiyo, Mbunge wa Hai, Freeman Mbowe (Chadema), kulalamikia muundo wa Serikali kutowekwa gazetini, Dk Bana alihoji kama Mbowe hajui kuwa muundo wa Serikali hautolewi kwa kila mtu.

Kuhusu suala la fedha zilizokatwa katika Mfuko wa Bunge na kuelekezwa katika utengenezaji wa madawati, Dk Bana aliwashangaa wawakilishi hao wa wananchi wanaopingana na uamuzi wa kumuinua mwananchi wa kawaida.

Alisema wananchi wote walipendezwa na hatua hiyo ya Serikali ya kuchukua fedha zilizotoka bungeni baada ya kubana matumizi na kupeleka katika kununua madawati.

“Hatua hii ni kielelezo kuwa Bunge lilikuwa likipangiwa fedha nyingi kuliko matumizi yake hivyo kusababisha kuwepo matumizi ya hovyo, sasa viongozi wa Bunge kuliona hilo na kurejeshwa kwenye jamii ni jambo jema,” alisema.

Alionya kuwa mikakati ya kambi ya upinzani, ni kutetea wananchi lakini kwenye hilo wananchi wenyewe kila kona wanawashangaa kwani inaonesha kutetea maslahi ya wabunge.

Bashiru Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Bashiru Ally alisema wananchi wanaangalia vitendo vya wabunge wao ndani ya Bunge na watawahukumu kwani michango yao ndani ya Bunge ni muhimu na njia ya kutatua tatizo si kususa, bali kufuata taratibu za kisheria.

Alisema uamuzi wa kutozungumza, unaondoa maana ya vyama vya upinzani ndani ya Bunge kwa kuwa watashindwa kujadili masuala yenye manufaa ya wananchi, kwani mawazo ya kiongozi wa upinzani bungeni ni muhimu na yanawekwa kwenye kumbukumbu.

“Kuwekwa kwenye kumbukumbu mawazo hayo ni kwa ajili ya vizazi vijavyo, sasa kitendo cha Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni kutumia vibaya nafasi anayopewa, ni udhaifu wa kimkakati,” alisisitiza Bashiru.

Shehe Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salum, alisema wanavyofanya wapinzani ni jambo lisilopendeza katika kuleta umoja wa kitaifa, kwani wao ni wawakilishi wa wananchi ndani ya Bunge na kususa siyo jambo la kiungwana.
 
Nimeanza kuona unafiki wa ukawa..unalalamika kwa fedha kupelekwa kwenye maeneo ya kuwajali wananchi...afya, barabara, elimu
Mtu akikuambia jambo la kijinga na ukamwamini atakudharau- by JK Nyerere.
CCM imewaona wajinga sana baada ya kuwalisha uongo nanyi kama mazuzu mkaamini. UKAWA hawajapinga kununua dawati au dawa, wao wanazungumzia taratibu kufuatwa kama sheria inavyosema tatizo likowapi?
Mbona mnaruhusu CCM iwadharau hivyo kwa kusadiki ujinga?
Tafuta hata wa bunge wa CCM wenye kujielewa watakufahamisha kuwa kuna makosa ila kwa vile hawaruhusiwi na chama chao kukosoa wanaumia moyoni tuu na kujiona watumwa
 
Mtu akikuambia jambo la kijinga na ukamwamini atakudharau- by JK Nyerere.
CCM imewaona wajinga sana baada ya kuwalisha uongo nanyi kama mazuzu mkaamini.
Ukawa hawajapinga kununua dawati au dawa, wao wanazungumzia taratibu kufuatwa kama sheria inavyosema tatizo likowapi?
Mbona mnaruhusu ccm iwadharau hivyo kwa kusadiki ujinga?
Tafuta hata wa bunge wa ccm wenye kujielewa watakufahamisha kuwa kuna makosa ila kwa vile hawaruhusiwi na chama chao kukosoa wanaumia moyoni tuu na kujiona watumwa
Wewe ndo jinga kubwa, hujui kucheza na siasa!
Ona sasa mlivyopuuzwa! Yaani mnadhani mnaweza kuubadili mtizamo wa umma kwa hoja hiyo ya kijinga!?

Kwa Mara nyingine tena, UKAWA mmejiingiza kwenye ujinga wa kiwango cha PhD! Mpigieni magoti Dr Slaa ndo alikuwa na akili za kutosha
 
UAMUZI wa Kambi ya Upinzani bungeni kuingia katika vikao vya Bunge na kugeuka bubu wakati wa mjadala wa Hotuba ya Ofisi ya Waziri Mkuu, umechukuliwa kwa hadhari kuwa unaweza kusababisha kambi hiyo ionekane inalinda posho bungeni.

Hadhari hiyo imetolewa na wasomi na viongozi mbalimbali waliozungumza na gazeti hili jana, walipokuwa wakitoa maoni kuhusu uamuzi wa kambi hiyo kususa hotuba hiyo.

Dk Bana

Mhadhiri wa fani ya siasa na utawala katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk Benson Bana, ndiye aliyesema kuwa kama uamuzi huo wa kuwa bubu bungeni hautabadilishwa, kambi hiyo itaonekana inalinda posho na kwamba haipo kwa ajili ya kutetea wananchi.

“Kazi yao ni kuwakilisha wananchi na makundi yote bungeni, sasa kitendo cha kuota ububu na kushindwa kueleza kero za wananchi, ni kutotendea haki wananchi maana ni vema wakae bungeni na kutoa hoja zao la sivyo, itafika wakati watatuomba radhi wananchi,” alisisitiza.

Akizungumzia hoja ya kwanza ya Mwenyekiti wa kambi hiyo, Mbunge wa Hai, Freeman Mbowe (Chadema), kulalamikia muundo wa Serikali kutowekwa gazetini, Dk Bana alihoji kama Mbowe hajui kuwa muundo wa Serikali hautolewi kwa kila mtu.

Kuhusu suala la fedha zilizokatwa katika Mfuko wa Bunge na kuelekezwa katika utengenezaji wa madawati, Dk Bana aliwashangaa wawakilishi hao wa wananchi wanaopingana na uamuzi wa kumuinua mwananchi wa kawaida.

Alisema wananchi wote walipendezwa na hatua hiyo ya Serikali ya kuchukua fedha zilizotoka bungeni baada ya kubana matumizi na kupeleka katika kununua madawati.

“Hatua hii ni kielelezo kuwa Bunge lilikuwa likipangiwa fedha nyingi kuliko matumizi yake hivyo kusababisha kuwepo matumizi ya hovyo, sasa viongozi wa Bunge kuliona hilo na kurejeshwa kwenye jamii ni jambo jema,” alisema.

Alionya kuwa mikakati ya kambi ya upinzani, ni kutetea wananchi lakini kwenye hilo wananchi wenyewe kila kona wanawashangaa kwani inaonesha kutetea maslahi ya wabunge.

Bashiru Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Bashiru Ally alisema wananchi wanaangalia vitendo vya wabunge wao ndani ya Bunge na watawahukumu kwani michango yao ndani ya Bunge ni muhimu na njia ya kutatua tatizo si kususa, bali kufuata taratibu za kisheria.

Alisema uamuzi wa kutozungumza, unaondoa maana ya vyama vya upinzani ndani ya Bunge kwa kuwa watashindwa kujadili masuala yenye manufaa ya wananchi, kwani mawazo ya kiongozi wa upinzani bungeni ni muhimu na yanawekwa kwenye kumbukumbu.

“Kuwekwa kwenye kumbukumbu mawazo hayo ni kwa ajili ya vizazi vijavyo, sasa kitendo cha Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni kutumia vibaya nafasi anayopewa, ni udhaifu wa kimkakati,” alisisitiza Bashiru.

Shehe Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salum, alisema wanavyofanya wapinzani ni jambo lisilopendeza katika kuleta umoja wa kitaifa, kwani wao ni wawakilishi wa wananchi ndani ya Bunge na kususa siyo jambo la kiungwana.
Dokta Bana Kichwa maji kweli, unasema wamegeuka bubu, hapo hapo unajibu hoja zao, hizo hoja zilitolewa ndotoni au makalioni? HOVYO KABISA NA MPUUZI WA MWISHO.

Bashiru na Bana swali langu kwenu, Wananchi wapi hao? Wanawaona kupitia RAMLI? Au Vikao vya Bunge vinafanyikia Uwanja wa Jamuhuri Dodoma hivyo Wananchi wanawaona?
Mnajificha gizani halafu mnasema mnaonekana? Nyie mlitafakari kweli kabla ya maoni haya ya Kipuuzi?

Hakuna excuse yoyote linapokuja suala la Sheria. Sheria ikisema imesema. Unakiuka Sheria lakini unataka waliokiuka Sheria Wakutane na Sheria? Kwa nini watu wanavaa miwani ya mbao na kuishi kwa ushabiki? Kukiuka Sheria katika kuwashughulikia waliokiuka Sheria ni kuwapa nafasi nzuri ya kujitetea na kuishinda serikali mbele ya Sheria maana Sheria inahitaji kufuata Sheria kwa Waovu, hili nalo ni gumu? The current cheap popularity will cost this nation very soon, hapo ndipo mtakapoelewa!
 
Wewe ndo jinga kubwa, hujui kucheza na siasa!
Ona sasa mlivyopuuzwa! Yaani mnadhani mnaweza kuubadili mtizamo wa umma kwa hoja hiyo ya kijinga!?

Kwa Mara nyingine tena, UKAWA mmejiingiza kwenye ujinga wa kiwango cha PhD! Mpigieni magoti Dr Slaa ndo alikuwa na akili za kutosha
Kheri ukweli unaodumu kuliko uongo usio na mashiko. Acha watu wapuuze ukweli kwa muda kwa kutokufahamu lakini sio kusimamia uongo kwa ajili ya kupata support danganyifu.
Hao mnaowadanganya siku wakierevuka itakuwa ni kasheshe
 
Mtu akikuambia jambo la kijinga na ukamwamini atakudharau- by JK Nyerere.
CCM imewaona wajinga sana baada ya kuwalisha uongo nanyi kama mazuzu mkaamini.
Ukawa hawajapinga kununua dawati au dawa, wao wanazungumzia taratibu kufuatwa kama sheria inavyosema tatizo likowapi?
Mbona mnaruhusu ccm iwadharau hivyo kwa kusadiki ujinga?
Tafuta hata wa bunge wa ccm wenye kujielewa watakufahamisha kuwa kuna makosa ila kwa vile hawaruhusiwi na chama chao kukosoa wanaumia moyoni tuu na kujiona watumwa
Umechakazwa yaani unazunguka humu JF kupingana na ukweli?..
 
Kwa mwenendo huu tutakuwa na CCM imara sana na upinzani dhaifu sana! Wanajua fika kuwa kwa sasa CCM imeteka agenda zote na wao kubakia wakitapatapa!

Uchaguzi wa 2020 utakuwa nzuri sana kuanzia Rais, Wabunge na Madiwani.
 
UAMUZI wa Kambi ya Upinzani bungeni kuingia katika vikao vya Bunge na kugeuka bubu wakati wa mjadala wa Hotuba ya Ofisi ya Waziri Mkuu, umechukuliwa kwa hadhari kuwa unaweza kusababisha kambi hiyo ionekane inalinda posho bungeni.

Hadhari hiyo imetolewa na wasomi na viongozi mbalimbali waliozungumza na gazeti hili jana, walipokuwa wakitoa maoni kuhusu uamuzi wa kambi hiyo kususa hotuba hiyo.

Dk Bana

Mhadhiri wa fani ya siasa na utawala katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk Benson Bana, ndiye aliyesema kuwa kama uamuzi huo wa kuwa bubu bungeni hautabadilishwa, kambi hiyo itaonekana inalinda posho na kwamba haipo kwa ajili ya kutetea wananchi.

“Kazi yao ni kuwakilisha wananchi na makundi yote bungeni, sasa kitendo cha kuota ububu na kushindwa kueleza kero za wananchi, ni kutotendea haki wananchi maana ni vema wakae bungeni na kutoa hoja zao la sivyo, itafika wakati watatuomba radhi wananchi,” alisisitiza.

Akizungumzia hoja ya kwanza ya Mwenyekiti wa kambi hiyo, Mbunge wa Hai, Freeman Mbowe (Chadema), kulalamikia muundo wa Serikali kutowekwa gazetini, Dk Bana alihoji kama Mbowe hajui kuwa muundo wa Serikali hautolewi kwa kila mtu.

Kuhusu suala la fedha zilizokatwa katika Mfuko wa Bunge na kuelekezwa katika utengenezaji wa madawati, Dk Bana aliwashangaa wawakilishi hao wa wananchi wanaopingana na uamuzi wa kumuinua mwananchi wa kawaida.

Alisema wananchi wote walipendezwa na hatua hiyo ya Serikali ya kuchukua fedha zilizotoka bungeni baada ya kubana matumizi na kupeleka katika kununua madawati.

“Hatua hii ni kielelezo kuwa Bunge lilikuwa likipangiwa fedha nyingi kuliko matumizi yake hivyo kusababisha kuwepo matumizi ya hovyo, sasa viongozi wa Bunge kuliona hilo na kurejeshwa kwenye jamii ni jambo jema,” alisema.

Alionya kuwa mikakati ya kambi ya upinzani, ni kutetea wananchi lakini kwenye hilo wananchi wenyewe kila kona wanawashangaa kwani inaonesha kutetea maslahi ya wabunge.

Bashiru Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Bashiru Ally alisema wananchi wanaangalia vitendo vya wabunge wao ndani ya Bunge na watawahukumu kwani michango yao ndani ya Bunge ni muhimu na njia ya kutatua tatizo si kususa, bali kufuata taratibu za kisheria.

Alisema uamuzi wa kutozungumza, unaondoa maana ya vyama vya upinzani ndani ya Bunge kwa kuwa watashindwa kujadili masuala yenye manufaa ya wananchi, kwani mawazo ya kiongozi wa upinzani bungeni ni muhimu na yanawekwa kwenye kumbukumbu.

“Kuwekwa kwenye kumbukumbu mawazo hayo ni kwa ajili ya vizazi vijavyo, sasa kitendo cha Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni kutumia vibaya nafasi anayopewa, ni udhaifu wa kimkakati,” alisisitiza Bashiru.

Shehe Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salum, alisema wanavyofanya wapinzani ni jambo lisilopendeza katika kuleta umoja wa kitaifa, kwani wao ni wawakilishi wa wananchi ndani ya Bunge na kususa siyo jambo la kiungwana.
UKAWA kwa sasa hawana hoja....ngoja labda Zitto akirudi ndiye anayeweza kuibua hoja kina Mbowe wakae nyuma yake...vinginevyo ni sarakasi tu.
 
Wabunge wengi wa upinzani mwaka 2020 wataamua kustaafu maana hawatakuwa na mashiko tena kwa serikali!
 
Wasomi pia kama makundi mengine ndani ya jamii huwa na wapuuzi wao - ni vizuri kutafakari yale wayasemayo. Si mlituona bunge la katiba?
 
Kheri ukweli unaodumu kuliko uongo usio na mashiko. Acha watu wapuuze ukweli kwa muda kwa kutokufahamu lakini sio kusimamia uongo kwa ajili ya kupata support danganyifu.
Hao mnaowadanganya siku wakierevuka itakuwa ni kasheshe
Mkuu we bure kabisa ukawa ndiyo mnazidi kujimaliza hiyo ni hoja ya kijinga sana huwezi kumshawishi mtu mwenye akili akakuelewa.
 
Wananchi wanawashangaa sana....hapo ndio wanapoenda kijizika 2020...
katafute bangi huko hakuna mtazania mwenye akili timamu mwenye hamu na CCM. CCM hashindi kwa kura hata siku moja isipokuwa ni kada Lubuva ndio anayewasaidia. ebu ekeeni tume huru ya uchaguzi kama kweli munajiamini
 
UKAWA lazima wakae watafakari upya mbinu zao maana sioni mwanga mwema kwao ifikapo 2020
Shida kubwa pia ambayo ukawa inawapa shida ni aina ya viongozi wakuu wa chama siyo aina ya viongozi wenye upeo mpana wa kufikiri na kuibua agenda za msaada kwa jamii katika ujenzi wa jamii mpya.
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom