Wasomi wa Malawi waandika Kitabu kumhusu Magufuli

Trable

JF-Expert Member
Jan 3, 2023
1,783
3,281
Wasomi na viongozi wa Tanzania wakati wao wakichagua kukaa kimya juu ya mambo mengi mazuri ya Pombe Magufuli yanayohusu uongozi wake, wakati wao wakiruhusu watu wajinga kuendelea kuuchafua uongozi wake, wasomi wa nchi Jirani ya Malawi, wao wameonyesha kwamba, wasomi wa Tanzania ni watu wanafiki na ambao wamekumbatia ufisadi pamoja na kujipendekeza kwa watawala ili kulinda mkate wao

Kila kizuri alichonacho mtu, iwapo atakitumia kwa uaminifu kwa ajili ya wengine, hubaki kumbukumbu kwa walioguswa na hicho, na kitu kizuri alichonacho mtu kuihusu jamii, huwa vigumu sana kwa jamii yake iliyomzunguka kukiona uthamani wake, japokuwa haikuwa hivyo kwa John Pombe Magufuli , aliendelea kugusa maisha ya wengi sana nchini na kuzidi sana kuaminiwa saana na jamii aliyokuwa akiiongoza kwamba, sasa tunamtetezi wa dhati na asiyona haya kuwatetea popote pale awapo!

Wakati jamii yake ikiona hivyo na kujivunia kwa uongozi wake makini, sifa zake tayari zilivuka mipaka, na sasa tunaanza kuona jinsi ambavyo haikuwa jamii tu ya watanzania walioguswa na uongozi wa hayati Magufuli, Malawi pia kwa namna yao waliguswa na uongozi wake na hata sasa wasomi nguli wa nchi hiyo wameandika kitabu kinachoeleza umahili wa uongozi wa Magufuli katika kushughurikia matatizo na kero sugu za wananchi

Sifa za mwanaume na ama kiongozi yeyote zisipovuka mipaka kwa utendaji wake bora na kuwa kielelezo cha watu wengine, itoshe kusema kwamba, huyo ni kiongozi ambaye hana ushawishi wowote nje na jamii yake anayoiongoza na ndiyo hao hata wakifa, siku hiyo hiyo watu wanasahau kama naye alikuwepo katika ulingo wa kisiasa!

Sifa za kiongozi yeyote Duniani, ili awe maarufu na wa kuigwa katika kuifikia jamii na Dunia kwa ujumla, shariti asiwe mbinafsi, ni sharti aonyeshe uwezo wake wa jinsi yeye yuko sahihi na smart katika kushughurikia kero za watu wake na hatimaye Watu na viongozi wengine waige namna yake ya anavyotatua na kushughurikia matatizo ya watu wake tena bila hofu yoyote

Huyo ndo alikuwa Magufuli !

Kunakipindi kitafika ambapo ninauhakika kwamba, watu wataulizwa kutaja Maraisi waliowahi kuiongoza Tanzania, kunahatari ya kutajwa Maraisi wawili

Hii ni kwa sababu ya mambo makubwa waliyowahi kuyafanya nayo yakawa alama ya kudumu

Staki maswali mengi kuwahusu wasomi wa Malawi walioona kitu ndani ya uongozi wa Magufuli hadi wao wakaona anastahili awekwe kwenye kumbukumbu ya kitabu ili Africa na Dunia Wajuwe kwamba hata Africa wenye akili kubwa wapo!
 
Mimi siyo msomi lakini hata kama ningekuwa siwezi kufanya upuuzi wa namna hiyo.

Katika safari yangu ya kimaisha nina mashujaa ambao walikuwa watu wangu wa karibu (ndugu) walinifanyia mengi lkn sijawahi kuandika hata ukurasa mmoja kuwahusu wao ndo aje kuwa mtu asiye kuwa na undugu na mimi hata chembe!
 
Halafu kuna wajinga wajinga fulani humu,ngoja waje na uharo wao wa vyeti fake uwasikie!

Wajinga wajinga kama wabunge wa vijiweni wa chadomo wanaoendekeza propaganda za visasi kama majuha,as if ni lazima wao kuwa bungeni.
 
JPM ni kama maji.
Hakuna mtu anayeweza kumzungumzia vizuri JPM zaidi ya waTanzania wenyewe. Huyo Mmalawi anasoma tu magazeti na kusikiliza hotuba ndio anaandika ila hajaishi kabisa Tanzania so haelewi tuliyopitia kama nchi.

Mtu aliua uchumi, Aliua sekta binafsi, alikataa kuajiri, Aliua demokrasia, aliliweka bunge mfukoni, bajeti za maendeleo hazijawahi kutekelezwa hata kwa 70% mpaka anafariki. Alichojifichia ni miundombinu ambayo mingi alijenga kwa mikopo na kutuachia matrillion ya riba!!

So huyo msomi is irrelevant maana Hana facts kuliko waTanzania.
 
Halafu kuna wajinga wajinga fulani humu,ngoja waje na uharo wao wa vyeti fake uwasikie!
Wajinga wajinga kama wabunge wa vijiweni wa chadomo wanaoendekeza propaganda za visasi kama majuha,as if ni lazima wao kuwa bungeni.
Huwezi lazimisha watu wasifie kama hamna!! Kama ni makusanyo mbona Samia kamzidi JPM ilihali humu mlisema watu watakwepa Kodi maana mama ni dhaifu.

Kama ni bajeti imekua mara dufu kuliko JPM. Kama ni miradi mikubwa Bado inaendelezwa hakuna uliosimama, kama ni ajira Mama Samia ametoa ajira nyingi ndani ya miaka 2 kuliko miaka 6 ya JPM!! Sasa what was so special kwa JPM?
 
Hakuna mtu anayeweza kumzungumzia vizuri JPM zaidi ya waTanzania wenyewe. Huyo Mmalawi anasoma tu magazeti na kusikiliza hotuba ndio anaandika ila hajaishi kabisa Tanzania so haelewi tuliyopitia kama nchi...
Mzee wetu, Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi aliweza sema kwa uhakika na bila kumumunya.
Alisema haya wakati wa msiba Chato....na nitamnukuu

"...Nilipata matatizo sana ya fikra, utadhani Kijana hafi...."

"...Miongoni ya mambo aliyotuachia:Jambo la kwanza, nalo ni kubwa ni pale alipofanya kijana huyu, alipoamua kutekeleza maagizo ya Baba wetu wa Taifa Marehemu Mzee Nyerere..."

'...amewaza na kuamua tuhamie Dodoma, nakutekeleza hilo kwa miaka miwili, jambo ambalo sisi wengine tulichukua miaka arobaini, bado hatujatekeleza, amefanya jambo kubwa sana!..."


"...sio hilo tu, ndugu yetu huyu amefanya mambo mengi sana yenye maslahi....Tanzania..."
 
Back
Top Bottom