Wasomi hawa wafuatao, wafikishwe mahakamani haraka sana!

Nsanzagee

JF-Expert Member
Jun 28, 2023
1,940
4,127
Heko Hayati JPM kwa uamzi huu ambao hukusikiliza kelele za wachumia tumbo na wanasiasa wajaza tumbo, kwao nchi badaye ila tumbo ndio kipaombele chao.

Miongoni mwao mwa wanaohitajika kufika kwa pilato ni, Waziri Nape na Waziri January Makamba, hawa ndio walikuwa msitari wa mbele kama wanasiasa kupinga mradi huu ambao ndio mwarobaini wa mgao wa Umeme nchini

Na wote waliokaa kitako kuitishia serikali ya awamu ya tano kwamba, iachane na ujenzi wa Bwawa la Umeme huko Rufiji kwa sababu kutasababisha madhara makubwa, moja wapo ni kutokunyesha mvua nchini, kwani miti itakayokatwa, inatosha kabisa kuifanya nchi yetu isiwe inapata mvua.

Kama utafiti wao ni kweli, Hizi mvua zinatokana na nini?

Naishauri Serikali, kama kweli tumedhamiria kupiga hatua za kimaendeleo, wasomi aina hii ya watu waongo kiasi kile, wachukuliwe hatua kali ili iwe fundisho kwa wasomi wengine wenye nia ya kupotosha.

Poleni watu wa Dar kwa mafuriko, watu wa Hanang'i, kule Morogoro, Geita, Mwanza n.k, Pole na hongera pia kwa Serikali kwa kuwajali wahanga wa mafuriko na kuwapatia mahitaji na vitu kadha wa kadha vya kibinadamu.

Hongera nyingi zimwendee Hayati Magufuli kwa kuwapuuza hawa wasomi njaa na kuendelea kujenga hiki kituo kikubwa kabisa nchini cha kuzalishia Umeme, si ajabu hata hao wasomi watanufaika na umeme huo

Shida yoote hii huwenda inasababishwa na wasomi waongo, wachumia tumbo, kwa kuwa wamekuwa wakifanya tafiti za kiulaghai bila kizingatia masilahi ya nchi yetu kwanza.

Mungu ibariki TANZANIA
 
Elimu ya mzungu haipo sawa 100% zaidi ya assumption ambazo tumekariri na kuaminishwa.

Unakuta mtu anachambua mambo ambayo yameandikwa na binadamu mwenzake. Inawezekana miaka ijayo watu wakaja na hoja nyingine.

Ndio maana inaitwa elimu ya mazingira.
 
Elimu ya mzungu haipo sawa 100% zaidi ya assumption ambazo tumekariri na kuaminishwa..

Unakuta mtu anachambua mambo ambayo yameandikwa na binadamu mwenzake... Inawezekana miaka ijayo watu wakaja na hoja nyingine.

Ndio maana inaitwa elimu ya mazingira.
Naanza kukuelewa mkuu, na hii ni hoja mhimu sana
 
Elimu ya mzungu haipo sawa 100% zaidi ya assumption ambazo tumekariri na kuaminishwa..

Unakuta mtu anachambua mambo ambayo yameandikwa na binadamu mwenzake... Inawezekana miaka ijayo watu wakaja na hoja nyingine.

Ndio maana inaitwa elimu ya mazingira.
Hiyo CM sijui laptop au tablet unatumia now ni elimu ya mzungu, why na sisi tusibuni yetu?
 
Hiyo CM sijui laptop au tablet unatumia now ni elimu ya mzungu, why na sisi tusibuni yetu?
Una hakika miaka 100 mbele zitakuwepo kweny chat,unaelewa elimu ya mazingira zile assumption za kina Einstein zipo wapi?

Wamekufa hawakuwa na wazo hata la kuwepo kwa artificial intelligence...wengine wamekufa wakipinga uwepo wa simu za mkononi ..
 
Wafunguliwe kesi
Mbona jangwani kuna mvua au hawajui hilo?
Tena na mafuriko kabisa
Inasikitisha sana mkuu, hao watu walipiga kelele nyingi sana, wakaungwa mkono na wazungu, ilikuwa kidogo tu bwawa lisijengwe iwapo Magufuli angeliwasikiliza
 
Elimu ya mzungu haipo sawa 100% zaidi ya assumption ambazo tumekariri na kuaminishwa.

Unakuta mtu anachambua mambo ambayo yameandikwa na binadamu mwenzake. Inawezekana miaka ijayo watu wakaja na hoja nyingine.

Ndio maana inaitwa elimu ya mazingira.
Sayansi ya kweli ilikufa na akina Archimedes na akina Newton huko. Siku hizi anayefadhili utafiti ndiye anayeamua matokeo ya utafiti huo yaweje. Ndiyo maana siku hizi unakuta utafiti unahusu kitu kile kile lakini matokeo yake yanakinzana.

Majuzi hapa ukatoka utafiti huko US eti watu wanaokula kitimoto wanaishi maisha marefu, wakati inajulikana kwamba ulaji wa nyama nyekundu unaweza kuleta matatizo lukuki ya afya yakiwemo lehemu mbaya, magonjwa ya moyo, unene n.k. Kuja kufuatilia kumbe utafiti ulikuwa umefadhiliwa na chama cha umoja wa wafuga nguruwe! 😁😁😁😁

Tumefika mahali hata kwenye sayansi inakubidi akili za kuambiwa uchanganye na zako!
 
Sayansi ya kweli ilikufa na akina Archimedes na akina Newton huko. Siku hizi anayefadhili utafiti ndiye anayeamua matokeo ya utafiti huo yaweje. Ndiyo maana siku hizi unakuta utafiti unahusu kitu kile kile lakini matokeo yake yanakinzana.

Majuzi hapa ukatoka utafiti huko US eti watu wanaokula kitimoto wanaishi maisha marefu, wakati inajulikana kwamba ulaji wa nyama nyekundu unaweza kuleta matatizo lukuki ya afya yakiwemo lehemu mbaya, magonjwa ya moyo, unene n.k. Kuja kufuatilia kumbe utafiti ulikuwa umefadhiliwa na chama cha umoja wa wafuga nguruwe! 😁😁😁😁

Tumefika mahali hata kwenye sayansi inakubidi akili za kuambiwa uchanganye na zako!
😂😂😂😂😂😂
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom