Hakuna ubishi kuhusu elimu ya juu, uelewa mkubwa na uzalendo wa Jenerali Ulimwengu. Na mara nyingi ni mkweli. Lakini ni binadamu, naye huongozwa na hisia binafsi wakati mwingine. Kwa mfano, kumsakama sana Mkapa (ambaye alikuwa na upungufu wa ujeuri kama wa Jenerali) ni kwa kuwa hakuzawadiwa cheo alichokitaka serikalini baada ya kushiriki kampeni vyema. Alipoendelea kumsakama, ndipo wabaya katika system wakaleta hoja ya uraia wake. Technically, kwa sheria ya uraia wa wakati ule, Jenerali, Bandora na wengine hawakuwa raia kwa kuwa hawakuzaliwa Tanganyika. Walizaliwa Rwanda, wakaja nchini wakiwa wadogo. Watu wengi wa mipakani, hata wa ndani sana kama maeneo ya Tabora (kwao Bandora) kulikokuwa na wahamiaji wengi, hasa wakimbizi wa nyakati za ukoloni, hawakuwa raia technically. Ilitakiwa warasimishe kwa kupata uraia wa kujiandikisha. Familia za kisomi mijini zenye utata huu huenda zilirekebisha haya, lakini haikuwa rahisi kwa familia ya kawaida kufanya hivyo, matokeo yake kwenye siku mbaya yakatokea ya akina Jenerali na Bandora. Wenye umri mkubwa mtakumbuka kuwa kwa sheria ile, ili kupata pasipoti ilibidi uonyeshe uraia wa Tanzania wa wazazi wako au upate mzee wa kula kiapo kuwa alishuhudia wazazi wako WAKIZALIWA. Sijui kama mnakumbuka jinsi Azim Premji alivyokosa uraia na kuvuliwa ubunge kwa sababu tu baba yake hakuwahi kukana uraia wa India, shitaka aliloshinda Dr. Walid Aman Kaborou wa CHADEMA. Ukisumbua, watu wa system, lakini hata washindani wako wengine kama wa kisiasa wa Premji, wanakupiga pale ulipo na kasoro hata usiyoijua. Jenerali, Bandora, Premji walirekebisha kilichotakiwa, na sheria ile pia imerekebishwa kiasi. Wote wapo nchini na ni raia.