Kilichonikuta kwa wasichana wa bar

Kilichonikuta kwa wasichana wa bar

fired

Senior Member
Joined
Apr 4, 2021
Posts
188
Reaction score
410
Nilimpata mwanadada kwa baa .kabla nikae naye niliongea na bawabu anijulishe kama huyu dada ataweka dawa kwa kinywaji changu nikiondoka.

Nilimwita mwanadada huyo nikamnunulia bia pia mimi nikachukua bia tulizungumza mda mfupi ,alafu nikaondoka nikajifanya niko msalani.nikamuuliza bawabu akanijulisha mwanadada ameweka tembe kwa kinywaji changu niliagiza kinywaji kingine .

Baadaye nikamwambia mwanadada tuende zetu kwangu akakubali. tulitoka tukaingia kwa gari langu tukaanza safari mwanadada alikua na mkoba wake.baada ya mwendo wa kilomita 10 nikajifanya gari lina shida nikaizima nikamshawishi mwanadada ashuke asukume gari.

Pindi tu aliposhuka na kusukuma gari niliwasha na nikaenda kwa mwendo wa kasi .Nilipofika kwangu kilomita 20 niliangalia mkoba wake nikapata tembe hamsini za kufanya watu walale.Hizi ndio anatumia kuwekea watu kwa kinywaji na kuwaibia.Nilifanya makosa kweli
 
Umenikumbusha enzi zangu kabla ya kustaafu hekaheka za ujana nisha-deal nao sana hao. Wikie d moja hivi ilinikuta morogoro samaki samaki. Dada mmoja hivi akajisogeza, sasa katika maongezi nilimtajia jina la uongo.

Tumemaliza hapo tukaenda logde. Wakati wa shughuli anataja sana jina langu lile la uongo nililomtajia kwa kulirudia rudia. Kesho yake nipo tena samaki samaki tukaonana akaniuliza kwanini nilimdanganya jina.

Baada ya kuzoeana na watu wa pale ndio wakaniambia kuna nguvu za giza wanatumia akitajataja jina lako dizaini kama unasinzia halafu anakuibia kila kitu.
Aisee🤔
 
Zile tembea balaa lake sio la kitoto ukiwekewa kwenye kinywaji unaeza kuwa in comma kwa zaidi ya siku mbili( depending on the dosage) na ukizinduka unajikuta umeporwa kila kitu huku hujielewi kbsa
 
Hapo ndipo unapokutana na mstari utakaokambia hii ni hadithi ya uongo ya kutunga. Hata kama hiyo gari yako ni Bajaji, huwezi kumwambia mwanamke shuka usukume gari, hata Mkurya hafanyi hivyo kwa mwanamke
alisaidiwa na wanaume walikuja kwa sababu ya minisketi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom