Linguistic
JF-Expert Member
- Mar 16, 2021
- 3,671
- 8,237
So kutokula Gambe+Nyapuz Ndio Kutoka kimaisha? Hiyo ni sehemu ya kurefreshHii ni sababu moja wapo inayowafanya Watanzania wengi hususani vijana wa siku hizi wanashindwa kutoka kimaisha.
Hebu fikiria mtu ameenda kuzisaka kwa watu alafu anaingia kwenye ulimbukeni na maisha ya starehe kiasi hicho? Starehe ambayo inamgharimu muda (mtu anakesha club mpaka saa kumi na moja alfajiri), hela (unaanza kulipia stahere, machangudoa na kuwalipia kodi yao ya nyumba), uwezekano mkubwa wa kuambukizwa magonjwa ya zinaa (mwisho ni umauti tu) na kibaya zaidi ni uwezekano wa kuingia kwenye mikono ya wahuni wakakumalizia mbali kwa kujifanya mjanja.
Mwisho wa siku jeneza linaporudi Tanzania, utasikia mtoto wetu amerogwa, hakuna mchawi hapo. Ni mfumo wa maisha aliyochagua mtu.
Utapoteza fursa na muda ujanani vibaya mno usipojiangalia, utakuja kulia chooni.