bahati93
JF-Expert Member
- Aug 6, 2015
- 1,234
- 2,233
Macho yanavutia sana. Kupitia macho waweza kuchungulia roho ya mtu, baadhi ya vigezo vinavyofanya macho kuwa yenye mvuto ni; kuwa na umbo la Uduara wenye uwiano, kuchomoza nje ya sura, na kuchukua nafasi zaidi ya asilimia hamsini ya Sura. Nimeweza kutazama kazi za sanaa za uimbaji na kubaini baadhi ya wasanii wa kiume wana Macho yenye mvuto kulinganisha na wenzao.
Wa kwanza ni Mr. Blue, kupitia kazi - Mimi na wewe - Kiss Kiss. Blue ana macho maridadi sana kuna muda mpaka nilizania yanaweza dondoka kutokana na jinsi yalivyochomoka. Kupitia Macho yake nabashiri Blue ni mtu poa sana, anaishi vizuri na watu.
Wa pili ni Bushoke, kupitia kazi kama - Dunia mapito, Usiende mbali, Nalia kwa furaha. Sijachoka kuyatizama muda wote jamaa Macho yake angavu sana, na Ni makubwa. Kupitia Macho yake jamaa namwona ni kama mtu mwenye usiri na hekima kubwa.
Pia, kuna viumbe vingine vyenye Macho mazuri ajabu sijavitaja. Lucky vina mioyo ya damu na sio ya mashine hivyo vitaelewa. Je, nimemaliza wote au unadhani kuna msanii nimemwacha? Una comment gani juu ya hili.
Wa kwanza ni Mr. Blue, kupitia kazi - Mimi na wewe - Kiss Kiss. Blue ana macho maridadi sana kuna muda mpaka nilizania yanaweza dondoka kutokana na jinsi yalivyochomoka. Kupitia Macho yake nabashiri Blue ni mtu poa sana, anaishi vizuri na watu.
Wa pili ni Bushoke, kupitia kazi kama - Dunia mapito, Usiende mbali, Nalia kwa furaha. Sijachoka kuyatizama muda wote jamaa Macho yake angavu sana, na Ni makubwa. Kupitia Macho yake jamaa namwona ni kama mtu mwenye usiri na hekima kubwa.
Pia, kuna viumbe vingine vyenye Macho mazuri ajabu sijavitaja. Lucky vina mioyo ya damu na sio ya mashine hivyo vitaelewa. Je, nimemaliza wote au unadhani kuna msanii nimemwacha? Una comment gani juu ya hili.