Master J: 99% ya wasanii wa bongo ni 'mateja'

tpaul

JF-Expert Member
Feb 3, 2008
21,838
18,250
Mtayarishaji maarufu wa muziki nchini Tanzania ambaye pia ni mchambuzi wa muziki kupitia show ya Bongo Star Search, ndugu Joakim Kimaro, maarufu kama Master J, amekiri kuwa 99% ya wasanii hapa nchini wanatumia bangi ndio maana wanapenda kuimba nyimbo zinazohamasisha ngono, uhalifu na matumizi ya bangi.

Amesema bila kuficha kuwa karibu wasanii wote wanaorekodi nyimbo kwenye studio yake ya utayarishaji wa muziki wanavuta bangi, cocaine, mirungi na dawa nyingine za kulevya. Hata hivyo ameishauri serikali kuwachukulia hatua wasanii hawa kwani inaonekana kama vile serikali inawaogopa. Pamoja na kuvuta bangi hadharani na hata kwenye video wanazorekodi na pia kuvaa nguo zenye picha za majani ya bangi, serikali haijawahi kuwachukulia hatua hata moja.

Chanzo: Said Fella, Master Jay wafunguka msako wa wasanii ‘mateja’

MAONI YANGU
Tatizo la wasanii kula bangi waziwazi limekuwa sugu hapa nchini. Kuna msanii mmoja (jina nimelisahau) amekuwa teja kabisa kwa sababu ya matumizi ya bangi na dawa za kulevya. Nilifikiri serikali ingeweza kumakamata huyu mtu na kumhoji anakaopata dawa ili kuwabaini wauzaji lakini imekaa kimya kana kwamba hakuna kinachoendelea hapa nchini.


Ikiwa mamlaka za serikali zitaendelea kuwaogopa hawa mateja kwa sababu wanawatumia kwenye kampeni za kisiasa, miaka michache ijayo vijana wengi watakuwa mateja kwa kuwa vijana hupenda kuiga kila kitu kutoka kwa wasanii kuanzia mavazi nyimbo za ngono na uvutaji bangi.

Nawasilisha.
 
Mtayarishaji maarufu wa muziki nchini Tanzania ambaye pia ni mchambuzi wa muziki kupitia show ya Bongo Star Search, ndugu Joakim Kimaro, maarufu kama Master J, amekiri kuwa 99% ya wasanii hapa nchini wanatumia bangi ndio maana wanapenda kuimba nyimbo zinazohamasisha ngono, uhalifu na matumizi ya bangi.

Amesema bila kuficha kuwa karibu wasanii wote wanaorekodi nyimbo kwenye studio yake ya utayarishaji wa muziki wanavuta bangi, cocaine, mirungi na dawa nyingine za kulevya. Hata hivyo ameishauri serikali kuwachukulia hatua wasanii hawa kwani inaonekana kama vile serikali inawaogopa. Pamoja na kuvuta bangi hadharani na hata kwenye video wanazorekodi na pia kuvaa nguo zenye picha za majani ya bangi, serikali haijawahi kuwachukulia hatua hata moja.

Chanzo: Said Fella, Master Jay wafunguka msako wa wasanii ‘mateja’

MAONI YANGU
Tatizo la wasanii kula bangi waziwazi limekuwa sugu hapa nchini. Kuna msanii mmoja (jina nimelisahau) amekuwa teja kabisa kwa sababu ya matumizi ya bangi na dawa za kulevya. Nilifikiri serikali ingeweza kumakamata huyu mtu na kumhoji anakaopata dawa ili kuwabaini wauzaji lakini imekaa kimya kana kwamba hakuna kinachoendelea hapa nchini.

Ikiwa mamlaka za serikali zitaendelea kuwaogopa hawa mateja kwa sababu wanawatumia kwenye kampeni za kisiasa, miaka michache ijayo vijana wengi watakuwa mateja kwa kuwa vijana hupenda kuiga kila kitu kutoka kwa wasanii kuanzia mavazi nyimbo za ngono na uvutaji bangi.

Nawasilisha.
haya matendo wanayoyafanya wakiwa kwenye stage /wakati wa maonesho yao, huwezi kuyafanya ukiwa na akili timamu. Lazima uwe umelewa pombe au madawa ya kulevya
 
haya matendo wanayoyafanya wakiwa kwenye stage /wakati wa maonesho yao, huwezi kuyafanya ukiwa na akili timamu. Lazima uwe umelewa pombe au madawa ya kulevya
Ni kweli kabisa mkuu. Kuna baadhi ya nyimbo za ngono ambazo mabinti huzirekodi wakiwa uchi. Mtu mwenye akili isiyokuwa ya bengi hawezi kufanya matendo kama yale abadani.
 
Wasanii toka zamani walikuwa wanavuta bangi..
Msanii wa mziki na bangi ni kawaida sana hiyo haikwepeki kabisa

Ova
Nikujiendekeza tu wala usanii hauna uhusiano na mibangi. Hawa jamaa ni mateja kweli ndio maana yanaimba nyimbo za hovyo ambazo hazisikiliziki kwa mtu mwenye kujielewa.

Tatizo serikali yetu na basata nao ni mateja kama hao wasanii ndio maana wanaruhusu huo uharo utamalaki kila siku halafu mtu akiimba vitu vinavyo make sense kama Nay wa Mitego anaitwa Oysterbay na nyimbo yake inapigwa kufuli.

Ujinga mwingi sana hii nchi. Ila sihami.
 
Umemuona 20% na Dullayo? Inasikitisha sana.
Wako na hali gani mkuu? Ndio maana sober houses zinazidi kuongezeka ktk nchi hii.

Kuna siku nilidamka kwenda Muhimbili nikakutana na kijiji kizima cha mateja wanaenda kupigwa sindano za kuondoa bangi mwilini. Nilishangaa sana. Siku zote bangi inaonekana kuwa ni kitu kibaya kwanini sasa wasanii wanalazimisha kula bangi? Haya masanii yana akili ndogo sana.
 
Nikujiendekeza tu wala usanii hauna uhusiano na mibangi. Hawa jamaa ni mateja kweli ndio maana yanaimba nyimbo za hovyo ambazo hazisikiliziki kwa mtu mwenye kujielewa.

Tatizo serikali yetu na basata nao ni mateja kama hao wasanii ndio maana wanaruhusu huo uharo utamalaki kila siku halafu mtu akiimba vitu vinavyo make sense kama Nay wa Mitego anaitwa Oysterbay na nyimbo yake inapigwa kufuli.

Ujinga mwingi sana hii nchi. Ila sihami.
 
Back
Top Bottom