Maboso
JF-Expert Member
- Feb 18, 2013
- 5,163
- 5,765
Tuache uwanja wa kampeni uwe huru kwa watu wote wanaopenda kupigia kampeni upande fulani. Wasanii ni watu wanaohudumia jamii sawa na viongozi wa dini, wasanii wana utashi, wafuasi na wapenzi wao sawa na viongozi wa dini. Wasanii wanashawishi wapenzi wao na viongozi wa dini wanashawishi wafuasi wao, lakini mwisho wa siku watu nao huwa wana akili na matakwa yao, wataamua nani watampigia kura.
Haiwezi kuwa sawa wasanii waruhusiwe kufanyia mtu kampeni lakini viongozi wa dini wanyimwe. Kwani shida ni nini hasa Mh. Lubuva?, ruhusu wote au kataza wote (all or none) utaeleweka sana.
Naomba mifano mitano ya nchi ambazo zimeingia katika mapigano ya wenyewe kwa wenyewe kwa sababu tu ya wasanii kushabikia upande fulani wa kisiasa.