Elungata
JF-Expert Member
- Jan 28, 2011
- 40,205
- 33,224
msemo kuwa mungu wao alitaka utawala uwe katika nyumba ya Daud,hiyo ni power struggle na ilikuwa propaganda ya wayahudi ili waendelea kutawala wao,anyway nilichokielewa mimi nikwamba wengi katika hii hoja hawajui tafsiri ya neno myahudi,msamalia na muisraeli,
Taifa la israeli lilikuwa na makabila 12 ndani yake kwapamoja yanaunda hilo taifa ,baada ya kifo cha mfalme suleimani hili taifa la israeli liligawanyika sehem mbili kabila 10 zilizokuwa zinakaa kaskazini mwa hilo taifa zilikataa kuendelea kutawaliwa na kabila la yuda so wakajitenga wakaweka makao yao makuu kwenye mji wa SAMALIA na taifa lao likawa linaitwa ISRAELI na kabila zingine mbili zilizobaki ilikuwa ni YUDA (JUDAH) na BENJAMINI wao walikuwa wanakaa kusini mwa nchi so wakabaki na taifa lao likawa linaitwa YUDA,na makao yao makuu yakawa Yerusalemu na wakawa wanatawaliwa na watu wa nyumba ya daudi kama Mungu alivyowaagiza,sasa ukianza kusoma 2Wafalme 16 wale waliobakia kusini wakaanza kutambulika kama WAYAHUDI (JEWS) kutokana na jina la taifa lao kuwa YUDA(JUDAH),sasa ukiendelea kusoma mbele zile kabila 10 za kaskazini zilizojitenga na ambazo hazikuwa zinatawaliwa na wazaliwa wa nyumba ya Daudi kama ilivyokuwa desturi badala yake zilitawaliwa na wafalme wasiofuata misingi ya Mungu wa baba zao wakachukuliwa utumwani na Mfalme wa ASSYRIAN wakaenda huko wakaendelea kutawaliwa na kuchangamana na watu wa mataifa wa huko ndio wakaitwa WASAMARIA,sasa kipindi Yesu anakuja alikuta bado huo mgawanyiko upo ule ufalme wa kaskazini (Samaria) na ufalme wa kusini (YUDEA) ambayo ilikuwa chini ya utawala wa WARUMI(ROMAN RULE),so utaona kwanini wayahudi walikuwa hawataki kuchangamana na wenzao tangia awali ,
Yesu na wanafunzi wake waliihubiri injili Judea yote kutafuta kondoo waliopotea kwa muda wa miaka mitatu na nusu then wayahudi wakamkataa Yesu kama Masihi wao wakafanikiwa kuwashawishi waroma kumuua Yesu na wakafanikiwa lakini baada ya siku tatu akafufuka akajionyesha wazi wazi kwa wanafunzi wake kabla ya kupaa kwenda mbinguni kuketi mkono wa kiume wa Mungu mwenye Enzi! ila kabla hajashikwa na kusulubiwa pale msalabani aliwaambia wanafunzi wake kuwa "Adhabu ya Wayahudi kumkaataa (soma kumb la torati 28) Mathayo 21:41,Yerusalemu itatwaliwa kimabavu na hekalu litavunjwa na wayahudi watachukuliwa utumwani kwenye mataifa yoote ya duniani, huu unabii ulitimia mwaka 70 baada ya Yesu ambapo mfalme TITUS aliyafanya hayo aliyoyasema Yesu!
So Waisraeli (zile kabila 10)au wasamalia waliadhibiwa wakatawanywa koote kama adhabu ya kuto kutii maagizo ya Bwana Mungu ,then YUDEA(JUDAH) nao wakatawanywa kama adhabu ya kumkataa masihi Yesu!
kinachofuata baada ya hapa ndio wakristo wengi tunakuja kutofautiana ...............Je hawa waliorudi pale wanaojiita taifa la israeli ndio wale waliotawanywa miaka takribani 2000 iliyopita?? au hawa ni fake na original bado wapo kwenye utumwa,dhiki,mateso na kila aina ya manyanyaso kama neno la Kristo linavyosema?????? kuna thread kama hii niliianzisha unaweza kuisoma pia kupitia hii link
https://www.jamiiforums.com/threads/uhalisia-wa-taifa-la-israeli.
mfano Saul mfalme wa kwanza hakuwa na uhusiano wowote na Daud,
daudi alikuwa mpiga kinanda wa kumfurahisha saul,na inaonekana hata ufalme alupata kwa hadaa,kwani mfalme saul baadae aligundua Daud anashirikiana na wafilist kumuhujumu,na hata wakati anakaribia kufa 'saul alitaka mwanae ndo awe mrithi wake ,Daud akacheza manuva mpaka yeye ndo akawa king,
hata ukijiuliza Daud alifanya kipi cha ajabu hadi iwe lazima ukoo wake ndo utoe mfalme.?
Hicho ndo kilifanya hiyo nchi igawanyike mara mbili,maana solomon mwana wa Daud alilewa madaraka,akaanza kunyanyasa raia,na alipokufa,raia wakamwuliza mrithi wake kama atawalegezea kidogo ama ataendelea kutawala kwa mkono wa chuma kama babake,alipojibu atawabatiza kwa moto,
waisrael wakaamua kujitenga na kuchagua mfalme wao.
Ukirudi kwa wayahudi,hawakuchukuliwa utumwani kwa kumkataa yesu,bali walitekwa na ufalme wa babel na baadhi kwenda utumwani,
ieleweke kuwa enzi hizo sio wayahudi pekee ndo walikuwa wakipelekwa utumwani,
ilikuwa ndo fashion,hata waasyria,waamori etc nao walikuwa wakipelekwa utumwani,na hawakuwa wote,wavamizi walichukua toplayer,
kwa maana ya mafundi,wasomi etc,sio kwamba taifa zima lilibebwa,
wakati wa yesu hakukuwa na judah kingdom,utawala wa Rumi ndo ukitawala,na Herode alikuwa amewekwa hapo na warumi kama Governor,
mwaka 70AD wayahudi wakiwa wamechoshwa na utawala wa kikoloni,waliiasi,
kuna jamaa mmoja akijiita masihi aliekuja kuwakomboa wayahudi ndo aliongoza uasi akijitangazia state kama yule al baghdad,
akapigana na warumi kwa zaidi ya miaka miwili,warumi walipata reinforcement toka Rumi,
wakatuliza uasi na kwa ghadahabu wakaliharibu lile hekalu