Lady Mwali
Senior Member
- Nov 15, 2018
- 147
- 332
Jamii yetu inapotosha maana ya kuandaa na kutoa futari ktk jamii.
Kwa kawaida futari inabidi itolewe kwa Waislam waliofunga wasiojiweza.
Leo unasikia futari inaandaliwa kwa matajiri wenye uwezo huku
wakiachwa masikini wahitaji.
Mathalani jana Wasafi Media imefuturisha bungeni Dodoma
huu ni zaidi ya unafiki.
Wabunge hawahitaji kufuturishwa kwani wanajiweza
wanapokea posho lak 3 kila siku na mshahara milioni 12 kwa mwezi.
Ingependeza zaidi Wasafi Media wangefuturisha masikini na makundi maalumu kama yatima,walemavu na wenye ukoma.
Nakumbuka marehemu Mengi alikuwa tajiri sana lakini mara nyingi alikutana na walemavu na kula nao chakula,sijawahi kusikia Reginard Mengi ameandalia chakula wabunge.
Jamii yapaswa ibadilike, iache unafiki na kufake maisha.
Kwa kawaida futari inabidi itolewe kwa Waislam waliofunga wasiojiweza.
Leo unasikia futari inaandaliwa kwa matajiri wenye uwezo huku
wakiachwa masikini wahitaji.
Mathalani jana Wasafi Media imefuturisha bungeni Dodoma
huu ni zaidi ya unafiki.
Wabunge hawahitaji kufuturishwa kwani wanajiweza
wanapokea posho lak 3 kila siku na mshahara milioni 12 kwa mwezi.
Ingependeza zaidi Wasafi Media wangefuturisha masikini na makundi maalumu kama yatima,walemavu na wenye ukoma.
Nakumbuka marehemu Mengi alikuwa tajiri sana lakini mara nyingi alikutana na walemavu na kula nao chakula,sijawahi kusikia Reginard Mengi ameandalia chakula wabunge.
Jamii yapaswa ibadilike, iache unafiki na kufake maisha.