qn of sheba
JF-Expert Member
- Sep 13, 2011
- 3,230
- 1,382
Hakika umenena...niliamua kuwa msomaji tu leo lkn umenifanya nijikute nachangia....
Na hapa kwenye chanzo cha bibilia na makanisa ndipo wengi walipojikwaaa..... Pia ni muhimu kuelewa Yesu aliagiza wanafunzi wakafundishe....sio na pia hakutembea na waandishi wa habari/bibilia na pia hakuna alipoagiza iandikwe....Mwinjili Yohana na Kitabu cha matendo ya mitume vinafafanua vizuri mwanzo wa kanisa na uandishi wa hiyo bibilia.
Ningekuomba uwe msomaji tu sio uanze kutuharibia mada yetu! Sisi twajadili uzuri kabisa hapa
www.exadventist.com/../default.asp
jisomee mwenyewe.
Mkuu Naona unaongea vitu via ajabu tu tena bila maandiko!
Mungu ametuagiza kupumzika Siku ya Saba na ni sabato Yake! Wapi Ktk maandiko tumeagizwa kupumzika Siku ya kwanza ya Juma?
Ningekuomba uwe msomaji tu sio uanze kutuharibia mada yetu! Sisi twajadili uzuri kabisa hapa
Hakika umenena...niliamua kuwa msomaji tu leo lkn umenifanya nijikute nachangia....
Na hapa kwenye chanzo cha bibilia na makanisa ndipo wengi walipojikwaaa..... Pia ni muhimu kuelewa Yesu aliagiza wanafunzi wakafundishe....sio na pia hakutembea na waandishi wa habari/bibilia na pia hakuna alipoagiza iandikwe....Mwinjili Yohana na Kitabu cha matendo ya mitume vinafafanua vizuri mwanzo wa kanisa na uandishi wa hiyo bibilia.
Maandiko gani zaidi nimekuambia soma (kutoka 12;16) Mungu amesema"siku ya kwanza kutakuwa kwenu na kusanyiko takatifu, na siku ya saba kutakuwa na kusanyiko takatifu; haitafanywa kazi yoyote katika siku hizo, isipokuwa kwa hiyo ambayo kila mtu hana budi kula,hiyo ifanyike kwenu" pia nimesema soma(matendo 20:7)"hata siku ya kwanza ya juma,tulipokuwa tumekutana ili kumega mkate, Paulo akahutubu...." ina maana mitume wa kwanza walifanya ibada siku ya jumapili kama tunavyoelezwa hapa na Luka,maandiko haya umeshayasoma? Wasabato kwann hamtaki kuwekwa huru kwa agano jipya,soma(yeremia 31:31-33)"angalia siku zinakuja asema bwana nitakapofanya agano jipya na nyumba ya Israeli,na nyumba ya Yuda si kwa mfano wa agano lile nililofanya na baba zao..")soma yote halafu niambie agano lipi mwalifuata?
Asante kwa ufafanuzi mzuri sana,hata mimi kuna wakati uwa nashawishika kubadili dini na kuwa msabato kwani wengi wenu mna misimamo isiyoyumba ya kiimani na honestly wengi ni waadilifu,ila nilikuwa nasita kwa sababu watu walinieleza kuwa hiyo dini sio Wakristu,labda naomba unitoe shaka tena juu ya ili:Ni kwanini mnasoma zaidi agano la kale na kulipa msisitizo kuliko agano jipya?na kwanini sher4ia za Mussa ambazo nyingi zimetenguliwa na agano jipya nyinyi bado mnazikumbatia?ni kwanini ni haramu kula nguruwe.wakati biblia inasema kiingiacho sio haramu bali kitokacho,samaki wasio na magamba nk,nijuavyo mimi sheria za Mussa,almost zote zilikuwa ni za mpito kuwasaidia wanaIsrael kufika nchi ya ahadi ,walisafir kwa miaka mingi kuvuka jangwa,ukiangalia vyakula vingi vilivyozuiwa ni vyakula vya mafuta mafuta,nguruwe,samaki asiye na magamba,wanyama wasio na kwato etc hii ni applicable kila mtu akiwa anasafiri na familia kuwazuia wanafamilia bahadi ya vyakula especially vya mafuta ili wafike salama bila matatizo ya tumbo,na ukifika salama zile sheria kwa familia za usile mishikaki,kuku wa Salanda,vyakula vya mafuta etc zinakuwa sio applicable tena.Pia nisaidie vitu kama Coca cola,majani ya chai, sukari ect vimeandikwa biblia gani kwamba ni haraamu,wakati enzi hizo coca cola haikuwepo?Wakristo ni watu gani hasa?. hebu soma hapa Paulo akimhutubia mfalme Agripa
Acts 26:27-31 King Agrippa, believest thou the prophets? I know that thou believest. Then Agrippa said to Paul, Almost thou persuadest me to be a Christian. And Paul said, I would to God, that not only thou, but also all that hear me this day, were both almost, and altogether such as I am, except these bonds. And when he had thus spoken, the king rose, and the governor, and Bernice, and they that sat with them: And when they had gone aside, they talked between themselves, saying, This man doeth nothing worthy of death, or of bonds.
Kwa hiyo wakristo kwa maana nyepesi na ya haraka ni watu wanaoishi kama alivyoishi kristo. Na Paulo kwa kuwa alikuwa mkiristo aliwaambia watu aliokuwa akiwaandikia mojawapo ya nyaraka maneno haya yafuatayo Niigeni mimi kama mimi ninavyomuiga Kristo. Kumbe mkristo ni yule anayeiga mambo aliyoyaishi kristo mfano.
1. Wanaitunza sabato maana luka 4:16 anasema na siku ya sabato akaingia katika sinagogi kama ilivyokuwa deaturi yake.
2. Wanaonyesha upendo kwa kila mtu anayewanzunguka
3. na mambo mengine mengi aliyoyatenda Yesu kristo.
Kwa hiyo sisi waadventista wa sabato, ni wafuasi sio tu wa kristo bali ni wafuasi watiifu wa kristo. Maana Yesu alisema maneno haya yafuatayo
Mkinipenda mtazishika amri zangu. Sisi ni watiifu kwa kristo maana amri zake tunazishika kama alivyotuomba kufanya hivyo, tofauti na wengine wanaojiita wafuasi wa kristo huku wakibagua amri za kushika, na hata wengine kufuta kabisa baadhi ya amri as waliona zinawabana katika uongo wao.
Asante kwa ufafanuzi mzuri sana,hata mimi kuna wakati uwa nashawishika kubadili dini na kuwa msabato kwani wengi wenu mna misimamo isiyoyumba ya kiimani na honestly wengi ni waadilifu,ila nilikuwa nasita kwa sababu watu walinieleza kuwa hiyo dini sio Wakristu,labda naomba unitoe shaka tena juu ya ili:Ni kwanini mnasoma zaidi agano la kale na kulipa msisitizo kuliko agano jipya?na kwanini sher4ia za Mussa ambazo nyingi zimetenguliwa na agano jipya nyinyi bado mnazikumbatia?ni kwanini ni haramu kula nguruwe.wakati biblia inasema kiingiacho sio haramu bali kitokacho,samaki wasio na magamba nk,nijuavyo mimi sheria za Mussa,almost zote zilikuwa ni za mpito kuwasaidia wanaIsrael kufika nchi ya ahadi ,walisafir kwa miaka mingi kuvuka jangwa,ukiangalia vyakula vingi vilivyozuiwa ni vyakula vya mafuta mafuta,nguruwe,samaki asiye na magamba,wanyama wasio na kwato etc hii ni applicable kila mtu akiwa anasafiri na familia kuwazuia wanafamilia bahadi ya vyakula especially vya mafuta ili wafike salama bila matatizo ya tumbo,na ukifika salama zile sheria kwa familia za usile mishikaki,kuku wa Salanda,vyakula vya mafuta etc zinakuwa sio applicable tena.Pia nisaidie vitu kama Coca cola,majani ya chai, sukari ect vimeandikwa biblia gani kwamba ni haraamu,wakati enzi hizo coca cola haikuwepo?
Sina hata muda wa kusoma mawazo ya mapandikizi(hasa majesuits) walioingizwa kanisani kwa sda ili waliharibu na waliposhindwa wakaondoka na kutoa hizo pumba.
"Anyway! It is lawful to do good in sabbath day!" sijakupata vema mkuu.
swali limejengwa kwa utunzwaji wa Sabato katika mazingira yaliyopita kama kioo cha sasa. Utanisamehe nipo mbali na Biblia.
Tunafahamu,
unatakiwa kupumzika siku ya saba.
Kuwa na sikukuu mwezi wa saba siku ya kwanza.
Kupumzisha ardhi mwaka wa saba.
Kusamehe madeni mwaka wa saba.
Orodha ikiendelea...
Kwa mtazamo huo dhana ya sabato ni pana zaidi ya kwenda kanisani siku ya sabato "jumamosi".
Inajumuisha taratibu nyingi zaidi kwenye mfumo wa maisha ya muumini, hususani inapokuwa sheria ya Mungu ni ngumu kuirahisisha kwa mtazamo wa kibinadamu
Wandugu,nitatoka nje ya mada kidogo.
Nimesoma na kuishi na wasabato sekondari na chuo pia ,kitu nilichogundua kuhusu hawa jamaa, kwanza kabisa ni Wabinafsi,wanajitenga sana na wakristo wa mathehebu mengine,pili wanajisikia kuwa wanajua biblia zaidi ya wakristo wengine. Tatu ukiwauliza Ellen G White ni nani,majibu wanayotoa ni ya mkato mkato.
Kifupi,hawa jamaa mi walikuwa wananikwaza kwa tabia zao hizo za ajabu.
Hapo penye nyekundu, unajisemea wewe na nani? kama umelenga kwa wanadamu wote basi you are wrong. Unapodhani kwamba unamuabudu Mungu ili akupe ya mwilini, unapaswa ujue kuwa kuna wengine walishaamua kukabidhi maisha yao jumla kwa Mungu(ingawa si katika ukamilifu). Vivyo hivyo katika kumtafuta maana anasema mkinitafuta kwa bidii mtanipata kwa hiyo mimi namtafuta Mungu kwa bidii(japo si katika ukamilifu).Sometimes tunalalamikia sana lakin ukweli nikua hatumjui Mungu vzuri kwa sababu hatuna bidii ya kumtafuta, lakin hata tumtafutapo tumelenga zaidi kwa mahitaji ya mwilin kuliko rohoni ndio maana mwisho wa siku tunaishia kusemana na kusengenyana kwasababu hatumjui Mungu vzuri
Ayubu 22:21 Mjue sana Mungu ili uwe na amani.....