Warioba Anamdhalilisha Nyerere!

Warioba Anamdhalilisha Nyerere!

Mleta mada umepatia sana. Mungu akubariki. Jaji warioba nampenda, lakini kwa serikali tatu kaweka utashi wake. Njelu kasaka, muumini wa serikali tatu hakubaliani naye. Stay tune! Tanzania yangu maskini inakufa
. Tutaipigania hadi mwisho.

Kweli kabisa 'Mpiganaji Wangu'!
 
Muungano ni wa kupigiwa kura kama ni:
A) Serikali mbili,
B) Serikali tatu, au
C) Serikali moja
Halafu utafutwe wastani wa asilimia za kura za bara na zile za visiwani ili kuamua ni muungano gani wananchi wanataka! NJE YA HAPO NI KUEDELEA KULEA TATIZO! HONGERA KWA KULIONA HILO BABA YETU WARIOBA!
 
Bwana Mashakaa, wacha klalamika hovyo,
kama yamekushinda...
 
Tanzania for tanzanians.sikuzaliwa tanganyika. Siijui tanganyika. Nchi yangu ni tanzania!!!
 
Nimemsikia Mwenyekiti wa Tume ya Katiba Jaji Mstaafu Warioba akidai kupitia ITV leo kuwa Mwalimu Nyerere hakuwa na mawazo mgando, na kwa maana yake, anataka kuhalalisha kuwa kama angekuwepo, Mwalimu angeunga mkono mawazo yao ya kuibuka na serikali tatu. Amedai kuwa endapo angekuwepo Mwalimu leo angekuwa amekasirika mno kutokana na Katiba iliyopo ilivyochezewa. Naweza kumuunga mkono kwa hilo lakini ni ukweli ulio wazi Mwalimu asingeunga mkono muungano wa serikali tatu kamwe! Ni udhalilishaji mkubwa wa mtazamo wa Mwalimu kudai kuwa Mwalimu angeunga mkono serikali tatu!! Sote tulikuwa hai wakati Mwalimu alipoingilia kati, tena kwa nguvu zake zote, na kuziua juhudi za kikundi cha 45 cha kuanzisha harakati za kuunda muungano wa serikali tatu, harakati zilizokuwa tayari zimeshaungwa mkono na Mzee Malecela akiwa Waziri Mkuu na Makamu wa Kwanza wa Rais chini ya utawala wa Mzee Mwinyi na aliyekuwa Katibu Mkuu wa CCM, marehemu Horace Kolimba. Huu anaoutangaza hivi sasa Warioba ni udhalilishaji mkubwa wa mawazo na msimamo wa Mwalimu kuhusu muungano. Ukweli ni kwamba muungano chini ya serikali tatu sio muungano. Hauna mashiko na ni rahiusi mno kuuvunja akitokea kiongozi mkorofi kutoka upande wa Tanganyika au Zanzibar kuliko muungano katika mtindo uliopo sasa. Na Warioba pamoja na heshima zake, asiwadhalilishe wananchi wanaopinga mawazo ya kuwa na serikali tatu kwa kuwaita ni "wenye mawazo mgando"--kama anavyoupigia yeye debe muungano wa serikali tatu pia hao wana haki ya msingi na ya kikatiba kuupinga muungano wa serikali tatu. Akae akijua sio suala la gharama tu linalopigiwa kelele, ila ni suala la mashiko katika muungano wenyewe. Kwa mtazamo wangu anayeupigia upatu muungano wa serikali tatu, hautaki muungano! Ukweli ni kwamba pamoja na juhudi zote hizo za kuutetea muungano wa serikali tatu, lakini Warioba hayuko wazi kuhusu ni wananchi wangapi wanaoutaka muungano huo. In fact, katika wananchi wapatao laki 3 waliohojiwa na tume yake kutoka bara na Visiwani, ni watu wapatao 19,000 tu waliounga mkono muungano wa serikali tatu--hakuna uhalali wowote wa kimahesabu na kimantiki unaoweza kusema kwa kujiamini kuwa Watanzania sasa wanaulilia muungano wa serikali tatu. Kwa kuanzisha muungano wa serikali tatu, ni wazi kabisa tutadhoofisha mno uzalendo wa Utanzania, ambao miaka ya hivi karibuni umeanza kuimarika sana ndani na nje ya nchi. Hivi sasa bendera ya Tanzania inapepea katika madaladala, bodaboda, viwanjani na vitu vyenye alama ama bendera ya Tanzania vimeanza kutapakaa nje ya nchi!! Watanzania tuwe makini sana katika suala hilo--mvi sio hekima!!

Nyerere alijenga viwanda ccm mkauza, Nyere alihifadhi maliasili zetu ccm mnagawa, alitunza tembo ,faru. ccm mnauwa kwakasi, ni ktk awamu hii tunashudia biashara ya madawa ya kulevya ikishamiri, kati yenu na warioba nani anamsaliti nyerere?
 
Wanaopinga mfumo serekali 3 ni CCM na wanaotaka mfumo wa serekali 2 uendelee ni CCM kutokana na sababu wanazozijua wenyewe.Walioleta muungano wa ajabu ajabu ambao haujawahi kutokea dunia ni CCM.Ni muungano wa ajabu kwa sababu huwezi ukaunganisha vitu viwili halafu vikapatikana vitu viwili.Vitu viwili vinapounganika ni lazima kitokee kitu kimoja.Kama TANU na ASP zilivyounganishwa ikapatikana CCM moja kwanini kwenye muungano wa serekali ya Tanganyika na ya Zanzibar zikazaliwa serekali 2 badala ya moja?kama CCM ilivyo moja.Wanao taka serekali 3 ni wananchi wala siyo Waryoba ili pawepo na usawa huwezi ukasema kuwa kunamuungano wa usawa wakati kuna nchi moja pamoja na serekali yake haipo halafu upande mmoja una sekali yake na nchi.Pia hakuna sehemu yoyote iliyoandikwa kuwa kile kilichofanywa na Nyerere hakiruhusiwi kubadilishwa hata kuboreshwa hakiruhusiwi hata Nyerere mwenyewe hajawahi kusema kuwa hiki ninacho kifanya kiendelee kuwa hivi hivi milele na milele.Wananchi nao wanataka kufanya chakwao endapo Nyerere angetokea akafufuka wawe na cha kumuonyesha kuwa wewe ulituachia hiki lakini sisi tumefanya hiki na kile.

Okay, lakini wasiibuke watu kwa kuwa Nyerere amefariki dunia, kudai kuwa Nyerere hakuwa na mawazo mgando, kwa maana ya kutaka kuhalalisha kuwa eti labda Nyerere angeliunga mkono wazo la serikali tatu! Hilo nalipinga hadi kaburini--msimamo wa Nyerere katika muungano hakuwa na mswalie mtume! Angeweza kukubali jambo lolote jingine libadilishwe kama alivyorelax katika suala la kubehuliwa kwa Ujamaa na mengine kadhaa (hata Azimio la Arusha) lakini sio katika muungano huu uliopo--hakutaka mchezo nalo kabisa akiamini kuwa ni suala la Msingi wa Taifa. Ninaposema hivyo sina maana kwamba ni dhambi kumkosoa Nyerere (coz hakuwa malaika), lakini ni dhambi kumpachika msimamo ambao aliupinga hadi mwisho wa maisha yake!! Baadhi yetu tulipata bahati ya kumfahamu vyema Mwalimu, tusidanganyane mchana kweupe!!
 
Binafsi Tanzania haijanisaidia lolote, zaidi ya kuishi miaka yote nikiwa nimesahaulika na kukandamizwa kama Tanganyika.
Acha uvunjike tuu huo muungano, kwanza kwetu wengine umelete gundu tu.
 
Siku zote kikwete hafanani na hao ccm katika maamuzi yake siunakumbuka ya serikali ya umoja wa kitaifa, kwa hili serikali tatu ndio litapita lakini naomba unijuze kwanini sisi wabara tunaing'an'gania zanzibar? Tunafaidika na nini na tuna the best army na strategic areas za kuweka kambi za jeshi

Uko right kabisa mkuu,kikwete kapigana na mawazo mengi sana ya wanaccm wenzake,tutamkumbuka kwa machache yake.
Navyojua mimi tanganyika inajitosheleza kwa kila kitu na sababu kubwa za kuing'ang'ania zanzibar ni sababu za kiusalama tu plus uwepo wa gesi na mafuta ila tofauti na hapo hatuna tunachokipata wala kufaidika na zenji,labda wakuu wa nchi wanasababu zao za msingi ambazo wananchi wa kawaida hatuzijui.
 
Binafsi Tanzania haijanisaidia lolote, zaidi ya kuishi miaka yote nikiwa nimesahaulika na kukandamizwa kama Tanganyika.
Muungano wenyewe gundu kibao.
 
Nyerere alijenga viwanda ccm mkauza, Nyere alihifadhi maliasili zetu ccm mnagawa, alitunza tembo ,faru. ccm mnauwa kwakasi, ni ktk awamu hii tunashudia biashara ya madawa ya kulevya ikishamiri, kati yenu na warioba nani anamsaliti nyerere?

Lete ushahidi usio na mashaka kuwa tiba ya madhambi hayo ni serikali tatu!
 
Binafsi Tanzania haijanisaidia lolote, zaidi ya kuishi miaka yote nikiwa nimesahaulika na kukandamizwa kama Tanganyika.
Muungano webyewe gundu kibao.

Wanakudanganya kuwa Tanganyika ndio itakupa kula ukishinda kijiweni?
 
Someni kitabu cha mwalimu "uongozi wetu na hatima ya tanzania". Mwalimu hakuacha kitu. Nawaomba sana msome hicho kitabu. Hata jaji warioba na kina butiku hawakipendi maana kinawaumbua. Haki ya MUngu hicho kitabu kimemaliza yote. Warioba team watajuta kusaliti hekima za mwalimu. Wameanza kuwa wakali, why? Nafsi zinawasuta. Wanajua dhambi yao. Eeh mwalimu, lala salama ukijua tanzania inakata roho. Umepuuzwa, lakini ukweli haupo mbali.
 
Wanakudanganya kuwa Tanganyika ndio itakupa kula ukishinda kijiweni?

Potelea mbali nikidanganywa sasa, maana tulipo toka nimeshadanganywa sana kuhusu faida za muungano wa serikali mbili.
Uongo huo ndiyo umenifikisha hapa kijiweni nilipo sasa.
 
Usitokwe povu sana kwa kuetetea serikali 2, je na tunaotaka serikali 1, mbona hatutoi matamko? Muungano siyo mali ya wanasiasa kama wananchi wakiamu hawautaki hakuna mwanasiasa atakayelazimisha juo hilo.
Nakushauri uwashawishi viongozi wako wa CCM kuwa kwanini wasiitishe kura ya maoni kuhusu muungano kaka tunautaka au hatuutaki? na kama tunautaka je tunautaka wa serikali ngapi?
Note: Tusitetee serikali ngapi tunazotaka badala ya kuulizwa hayo maswali hapo juu.

Ndugu, hata kama una hoja lakini kwa kuwa umetumia lugha ya mitaani wakati hii ni mada nyeti, nakuacha!
 
K-BoKO: naomba kujua ni watu gani waliomba muungano? Kama ni wazanzibari kwa sasa wanataka serikali tatu sasa ulipotoa mawazo yako ulikuwa unalijua hilo, muungano wa serikali tatu unawekwa kwa masilahi ya wazanzibari watu ambao tumekuwa tukilazimisha kuwanao kwa sababu wanazojua wachache, kikwete atakumbukwa kwa lile la serikali ya umoja wa kitaifa na hili kama litapita na.wazanzibari, azimio la arusha lilikufa wakati wa mwalimu wakati.akiwepo mbona hakusema kadhalilishwa?

Hivi kumbe hata azimio la arusha nalo lilikuwa ni kero kwako? Haya basi, muungano nao ni kero ya mwisho kwako; serikali 3 ni ubinafsi tu uliokomaa, kama bado tunautaka muungano ni bora tume ingelijikita kuhoji wananchi ni kwa nini sasa tusiende kwenye serikali moja. Ujinga wa sasa wa serikali tatu ni kurudi nyuma tu na kuendekeza utengano na ubinafsi!
 
Endapo utaona vyema message yangu, nimeunga mkono la kuchezewa kwa katiba iliyopo--na hasa upande wa Zanzibar--ila kama ilivyokuwa kwa Mwalimu--siamini kabisa kwamba solution ni serikali tatu. Mbona suala hilo liliibuliwa wakati Mwalimu akiwa hai, tena kwa hoja hizo hizo za kuchezewa kwa katiba, hasa upande wa Zanzibar na kwa kutumia uwezo wake kama Jeshi la Mtu Mmoja akaiua hoja ya serikali tatu iliyokuwa ikiasisiwa na akina Njelu Kasaka na kundi lao la watu 45? Tuzungumze tatizo halisi hapa badala ya kulikwepa! Kama viongozi wetu wameshindwa kumfunga paka kengele, naamini Watanzania wa kweli watamfunga katika kura ya maoni ijayo!! Na pia naamini iko siku ataibuka kiongozi Mtanzania atakayemdhibiti vyema 'paka' asiichezee katiba ya TANZANIA.

Ufumbuzi siyo kuendelea na serekali 2 ufumbuzi ni serekali 1.
 
K-BoKO: naomba kujua ni watu gani waliomba muungano? Kama ni wazanzibari kwa sasa wanataka serikali tatu sasa ulipotoa mawazo yako ulikuwa unalijua hilo, muungano wa serikali tatu unawekwa kwa masilahi ya wazanzibari watu ambao tumekuwa tukilazimisha kuwanao kwa sababu wanazojua wachache, kikwete atakumbukwa kwa lile la serikali ya umoja wa kitaifa na hili kama litapita na.wazanzibari, azimio la arusha lilikufa wakati wa mwalimu wakati.akiwepo mbona hakusema kadhalilishwa?

Nadhani umejichanganya mno kiasi kwamba nashindwa kukupata sawasawa, sorry sana!
 
Ufumbuzi siyo kuendelea na serekali 2 ufumbuzi ni serekali 1.

Ukweli ni kwamba huo ndio msimamo wa Watanzania wengi, mimi nikiwemo. Ila sote twajua kuwa hilo halikuwepo tangu day one ya kuundwa kwa muungano na limeendelea kupingwa, hasa na Wazanzibar kwa kuogopa kumezwa. Muungano wa serikali mbili tumekuwa nao kwa miaka 50 na wengi wetu tumezaliwa Watanzania na tumeishi ndani ya Tanzania kwa miaka yote hiyo 50--waswahili wanasema heri zimwi likujualo! hatupingi kubadili au kuandika katiba mpya, lakini tunapinga mabadiliko for the sake of mabadiliko--tunataka mabadiliko yenye tija sio yatakayovunja nchi tuliyozaliwa na kuipigania kwa miaka 50!!
 
Back
Top Bottom