Warioba Anamdhalilisha Nyerere!

Warioba Anamdhalilisha Nyerere!

uNAPOSEMA wanaopina Muungano wa serikali tatu ni CCM, CCM PIA NI WANANCHI WA Tanzania. Wananchi wa Tanzania sio CHADEMA au CUF wote ni wananchi wa Tanzania ila wanatofautiana kimtazamo tu.
Mpaka watanzania wanafikia kusema wanautaka au hawautaki Muungano ina maana wanajua faida na hasara zake. Kila mtoa maoni yake anajua ni jinsi gani atafaidika na aina ya Muungano anaoupendekeza, lakini wengine inatokana na uvivu wa kufikiri na kubuni mbinu mpya za kufanya Muungano uimarike zaidi ila wana mbinu za kuudhofisha kwa maslahi duni ya KUPIGIWA MIZINGA 21, Kuwa na bendera yao, wimbo wa Taifa na mambo mengine kama vile kuomba misaada.
Tupe uzuri na ubaya wa serikali mbili pamoja na changamoto zake pia rudi upande wa serikali tatu nazo weka faida na hasara zake ili tujue kama mzee warioba kapotoka,unajua kama sera za mwalimu zilishindwa pia? Unajua kwa nini wakati wa mwiyi aliruhusu soko huria?(ruksa) bs ujue pia kulingana na mda na changamoto za hapa na pale na wimbi la watu wengi kuzidi kuelimika,mwalimu asingekuwa na choice zaidi ya kukubaliana na mawazo ya wengi ya serikali3.
Wanaopinga serikali 3 ni ccm na sio wananchi wote kama unavyojitahidi kupotosha.
 
Ni kwel mwl hakuwa na mawazo mgando,wengi wetu ndio tuna mawazo mgando.
Mwl alifariki 1998 leo 2014 isiwe Nyerere awe mwisho wa upeo wetu kufikiri na kujadli mustakabali wa Taifa letu.
Muungano uliozaa Tanzania ni kt ya Tanganyika na Zanzibar iwaje tukatae nchi yetu ya asili,huu ni utumwa.
Yatubidi tubadilike,kuhusu gharama kwa sasa ni kumbwa kuliko kukiwa na hizo serikali tatu.

Sahihisha hapo.
 
Kwa kuwa wewe ni dictator usiyependa kufuata matakwa ya wananchi walio wengi ndiyo unavyotaka WARIOBA awe?
lahasha..... kajipange vizuri
 
Nyerere aliondoa ushirika baade akaurudisha. alifuta serikali za mitaa akajagundua lilikuwa ni kosa. alipigania mfumo wa chama kimoja akaja kuugeuka. kwa hiyo kusema kuwa hangekubali serikali tatu sasa ni sawa na kutabiri tu.
kimsingi serikali tatu ni muhimu kulingana na mazingira ya sasa. kwamba Zanzibar hawataki serikali moja lakini bara hawaoni tatizo. Zanzibar hawaoni shida sana ya serikali mbili laakini ni mfumo wa kimagumashi. sasa inabaki serikali tatu. no other option!
Fikiria serikali tatu katika ngazi ya chini kama ilivyo jiji la Dar ambapo kuna halmashauri ya jiji na halmashauri tatu za Ilala. Temeke na Kinondoni.
fikiria serikali tatu kama vyombo vinavyoongozwa na katiba na sheria ambazo kila kitu kimeelezwa waziwazi. Watu ni wale wale lakini wanafanya shughuli zao zilezile za kawaida kwa kufuta taratibu zilizopo. maswala ya muungano yatafanyika kwa taratibu zilizowekwa na ya serikali za bara na visiwani hivohivo. unaishi tanganyika unasafiri kwenda Zanz. na zanziba unaenda Tang. kwa kufuta taratibu zilizopo
Kuwepo kwa serikali tatu ni sawa na kugawa majukumu ya kiutekelezaji na kiuendeshaji tu chini ya serikali ya muungano jiografia ya nchi ni ileile. Ikiwa kiongozi wa upande mmoja ataingiwa na tamaa hilo sasa ni suala la uasi na katiba itaeleza nini kifanyike. Jua kuwa Serikali ya muugano ndiyo yenye mamlaka ya nchi.
WATU WAACHE KUENDESHWA KWA HISIA NA USHABIKI
 
Tanzania bara (Watanganyika) tunajifanya tunathamini na kuuheshimu muungano,wakati Zanzibar hawautaki. Angalia katiba yao,kuna cha muungano pale? Wimbo wao wa Taifa,bendera yao,wanaye Rais ambaye ni amiri jeshi wao,kwa hiyo wana vikosi vyao vya majeshi,bendera ya Rais wao,nk.Tanzania bara/Tanganyika tuna nini?Wazanzibar wanajisikia dhalili kutambulishwa kama Watanzania,wanapenda zaidi Uzanzibar(wasisahau ni ndani ya muungano).Tanganyika/Tanzania bara tunatambulishana kama Watanzania. Serikali tatu ikipita,Tanganyika itarudi,lakini Pemba nao watadai serikali yao,au hata Jamhuri ya Pemba ili waungane na Mombasa Republic.Huu ubaguzi unalelewa na serikali iliyo madarakani.Wanasheria wengi walipinga katiba ya Zanzibar,kwamba imeingilia madaraka ya Muungano,ila hakuna hatua iliyochukuliwa. Leo hii wana CCM wanadai kuwa baadhi ya vyama vya siasa ni vya kidini\kikabila(wanapanda mbegu ya ubaguzi),jambo ambalo ni kinyume cha katiba. Hakuna tamko lolote kukemea hali hiyo au kuvichukulia hatua za kisheria vyama hivyo. Hii ni kansa inayolelewa na serikali,sijui kwa faida ya nani.
 
Haka kamkoa kazanzibar katatuponza watanganyika.Kamkoa haka kasumbufu kameshavunja sana katiba malengo yake kawe huru kajiunge na magaidi wenzao.Haka kasomalia katarajiwa kitatupa sana dozi miaka ijayo yani full kujilipua na mauaji ya kustukiza.Ndugu watanganyika wenzangu tuvipe pesa yao ya BOT hivi vijamaa na kuviacha kimpango wao.Tukiendelea kuving'ang'ania vitatujambisha mpaka tushike adabu yetu.Vimeshaweka mamluki wao Tanganyika vinausoma mchezo tu vijalaana hivi.Shauli zenu.
 
K-Boko serikali mbili sio muungano, ni Tanganyika kuikoloni Zanzibar. Wazenj wameishtukia hiyo.

Sent from my GT-I9192 using Tapatalk
 
Last edited by a moderator:
wewe jaribu sana kutumia akiri zako za kuzaliwa kuliko kumfanya Nyerere kama mungu wako. jiulize kwa nini Nyerere alipounganisha Tanu na Afro Shiraz hakuuiacha afro shiraz iwe huru visiwani. Ila alipounganisha Tanganyika na Zanzibar aliiacha zanzibar ijitawale? Muungano wa serikali tatu au mbili zote ni hisia za kipuuzi tupu. Muungano ni serikali moja tuu na raisi mmoja kwisha kazi.

Jaribu kujifunza kumkosoa nyerere ili uijenge nchi! usimfanye Nyerere ni mungu wetu wala eti fikira zake ni bora kupita watanganyika wote.
Mkuu, CCM zipo mbili. Pana CCM (Tanganyika) na CCM (Zanzibar), jaribu kuingia ndani zaidi.
 
So, nani kakwambia na mimi ni CCM?

Mimi ni Mtanzania ndugu. Naitetea Tanzania yangu, na wala siijui Tanganyika na wala sina hamu ya kuijua. Nimezaliwa Tanzania!! Hayo ya faida na hasara--soma tena maandishi yangu! By the way, kuwa CCM ni dhambi ila kutokuwa CCM ndio ushujaa sio?

Wewe ni Mbumbumbu kabisa...
Kama ni kumvua nguo Nyerere,CCM wenyewe ndio walianza tena kitambo tu,
1: Alipinga ubinafsishwaji wa NBC,lakini Mkapa akapitisha..
2:Alikemea Rushwa,lakini ndani ya CCM rushwa ni kama Ibada.
3: Alikemea Undugu,Ukabila na Urafiki ktk kuwapa watu Vyeo/Nyadhifa mbalimbali,lakini leo hii,Jk,Mkewe,Mtoto na Mdogo wa JK ni Wajumbe ndani ya NEC ....
Swali,Angekuepo leo hii ,yanayoendelea ndani ya CCM yangekuapo? Tembo wangefyekwa namna hii!? Madini yange sepeshwa namna hii!? Twiga wangesafirishwa namna hii!? Wawekezaji ucgwara wangeshamiri kama ilivyo sasa!?
Fikiri kabla hujaleta Uzi wako hapa ili ujizolee Umaarufu!!
 
BIG UP mzee Warioba kwa kuwachanachana vilivo wanaokosoa rasimu hii ya katiba. Hawa wanataka machafuko tu nchini kwa kupinga maoni ya wengi.
 
Wewe ni Mbumbumbu kabisa...
Kama ni kumvua nguo Nyerere,CCM wenyewe ndio walianza tena kitambo tu,
1: Alipinga ubinafsishwaji wa NBC,lakini Mkapa akapitisha..
2:Alikemea Rushwa,lakini ndani ya CCM rushwa ni kama Ibada.
3: Alikemea Undugu,Ukabila na Urafiki ktk kuwapa watu Vyeo/Nyadhifa mbalimbali,lakini leo hii,Jk,Mkewe,Mtoto na Mdogo wa JK ni Wajumbe ndani ya NEC ....
Swali,Angekuepo leo hii ,yanayoendelea ndani ya CCM yangekuapo? Tembo wangefyekwa namna hii!? Madini yange sepeshwa namna hii!? Twiga wangesafirishwa namna hii!? Wawekezaji ucgwara wangeshamiri kama ilivyo sasa!?
Fikiri kabla hujaleta Uzi wako hapa ili ujizolee Umaarufu!!
Mkuu, umesahau kitu muhimu sana 'AZIMIO LA ARUSHA'.
 
So, nani kakwambia na mimi ni CCM?

Mimi ni Mtanzania ndugu. Naitetea Tanzania yangu, na wala siijui Tanganyika na wala sina hamu ya kuijua. Nimezaliwa Tanzania!! Hayo ya faida na hasara--soma tena maandishi yangu! By the way, kuwa CCM ni dhambi ila kutokuwa CCM ndio ushujaa sio?

Nani kakuambia Tanzania haitakuwepo chini ya mfumo wa serikali Tartu?! Unjustified terror!
 
serikali 3 ndoto za kipuuzi zenye malengo ovu ya kisiasa,
haitafikiwa kamwe, take it or choke with it
 
Nani kakuambia Tanzania haitakuwepo chini ya mfumo wa serikali Tartu?! Unjustified terror!

Msipotoshe watanzania kwamba eti kuna faida ya serikali tatu, faida ni neno TANGANYIKA tu, hasara ni jyiiingi mno, huyo Mkiti anataka ulaji tu ili apewe pia kuunda katiba ya Tanganykka, na hata hivyo watanzania walioitaka 3 ni wale wazito na maarufu lus nje, maskini kumuongezea neno serikali ya 3 ni upuuzi, mambo ni meengi mno, wakati wa kutoa maoni walikuja 88, hapa Ddm wakasema tuandike kwenye karatasi na kutuma siku hiyohiyo, hali mahali pa kukaa hakuna pale viwanjani, ilikuwa tu ni janja tu, na watu wengi wakashindwa.wamesema waliotoa maoni ni 4m, ndani yake wapo wasioitaka.jiulize hiyo serikali inakuja kwa ajili ya nani, kama ni ya wananchi basi ni serikali mbili kama Mwl.NYERERE alivyotaka.Mziki ni Bungeni naamini haipiti, labda tu...
 
Kwanza mtoa mada kakosa uzalendo, pili ni wa chama chakavu, tatu hoja haina mashiko
 
Nimemsikia Mwenyekiti wa Tume ya Katiba Jaji Mstaafu Warioba akidai kupitia ITV leo kuwa Mwalimu Nyerere hakuwa na mawazo mgando, na kwa maana yake, anataka kuhalalisha kuwa kama angekuwepo, Mwalimu angeunga mkono mawazo yao ya kuibuka na serikali tatu.

Amedai kuwa endapo angekuwepo Mwalimu leo angekuwa amekasirika mno kutokana na Katiba iliyopo ilivyochezewa. Naweza kumuunga mkono kwa hilo lakini ni ukweli ulio wazi Mwalimu asingeunga mkono muungano wa serikali tatu kamwe!

Ni udhalilishaji mkubwa wa mtazamo wa Mwalimu kudai kuwa Mwalimu angeunga mkono serikali tatu!! Sote tulikuwa hai wakati Mwalimu alipoingilia kati, tena kwa nguvu zake zote, na kuziua juhudi za kikundi cha 45 cha kuanzisha harakati za kuunda muungano wa serikali tatu, harakati zilizokuwa tayari zimeshaungwa mkono na Mzee Malecela akiwa Waziri Mkuu na Makamu wa Kwanza wa Rais chini ya utawala wa Mzee Mwinyi na aliyekuwa Katibu Mkuu wa CCM, marehemu Horace Kolimba.

Huu anaoutangaza hivi sasa Warioba ni udhalilishaji mkubwa wa mawazo na msimamo wa Mwalimu kuhusu muungano. Ukweli ni kwamba muungano chini ya serikali tatu sio muungano.

Hauna mashiko na ni rahiusi mno kuuvunja akitokea kiongozi mkorofi kutoka upande wa Tanganyika au Zanzibar kuliko muungano katika mtindo uliopo sasa.

Na Warioba pamoja na heshima zake, asiwadhalilishe wananchi wanaopinga mawazo ya kuwa na serikali tatu kwa kuwaita ni "wenye mawazo mgando"--kama anavyoupigia yeye debe muungano wa serikali tatu pia hao wana haki ya msingi na ya kikatiba kuupinga muungano wa serikali tatu.

Akae akijua sio suala la gharama tu linalopigiwa kelele, ila ni suala la mashiko katika muungano wenyewe. Kwa mtazamo wangu anayeupigia upatu muungano wa serikali tatu, hautaki muungano!

Ukweli ni kwamba pamoja na juhudi zote hizo za kuutetea muungano wa serikali tatu, lakini Warioba hayuko wazi kuhusu ni wananchi wangapi wanaoutaka muungano huo.

In fact, katika wananchi wapatao laki 3 waliohojiwa na tume yake kutoka bara na Visiwani, ni watu wapatao 19,000 tu waliounga mkono muungano wa serikali tatu--hakuna uhalali wowote wa kimahesabu na kimantiki unaoweza kusema kwa kujiamini kuwa Watanzania sasa wanaulilia muungano wa serikali tatu.

Kwa kuanzisha muungano wa serikali tatu, ni wazi kabisa tutadhoofisha mno uzalendo wa Utanzania, ambao miaka ya hivi karibuni umeanza kuimarika sana ndani na nje ya nchi.

Hivi sasa bendera ya Tanzania inapepea...

SIJUI NIFANYEJE WATU Waelewe juu ya Ubaya wa Serikali tatu hasa sie wa Bara, Gharama za kuihudumia hiyo serikali ya 3 Zanz wanauwezo?Nani mwenye nguvu zaidi kwenye Serikali hizo, Tanganyika au Tanzania? Bunge la Tanganyika nalo litaundwa je tupo tayari kubeba gharama? Gharama tena za Katiba ya Tanganyika tupo tayari kuzibeba? Maraisi kibao na viongozi wastaafu kuhudumiwa hadi kufa tupo tayari? Je, tupo tayari kulipa kodi MARA 3 ili kujenga nchi kwa nguvu zetu chininya serikali hizo? Nani mwenye mamlaka ikiwa kuna tatizo upande wa muungano mmoja hasa Tanganyika.Je Zanzibar wakigawanyika na ndipo wanachotaka kuwa Pemba na Zanz tumejiandaa kuwa na SERIKALI NNE?Tunajiunga kuwa jumuia ya EAC, ambapo tunaelekea kuwa na sarafu moja na Rais mmoja, je Kuigawa nchi tutaingia Muungano huu kwa nguvu.MIMI NAWAASA WATANZANIA WOTE...TUSIPOTOSHWE TUSIWAPE NAFASI MTU KUJITENGENEZEA SIFA KUTUMIA LEGACY YA NYERERE, KUONYESHA YA NYERERE ILISHINDWA.TANZANIA NI MOJA WOTE NI WAMOJA NA SERIKALI NI MBILI ILI ZANZIBA WAJUE KUWA WAPO HURU KWA MASWALA FULANI..TUWE WAZALENDO SIO KUFIKIRIA...NITAPATAJE URAIS...KUPITIA CHAMA CHANGU..HASA UPINZANI...HILI SWALA TULIJADILI KWA NGUVU ZOTE, KWA kina.
 
NI mwalimu Nyerere pia aliyefuta mfumo wa vyama vingi miaka ya 60, ni mwalimu Nyerere huyo huyo aliyemshauri Ali Hassani Mwinyi enzi hizo akiwa ndio rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kua aridhie mfumo wa vyama vingi! Tusikariri mambo, mzee/mwalimu alikua ni mtu anaye kwenda na wakati sana. Sababu mojawapo iliyosababisha mwalimu alazimishe mungano na Zanzibar ilikua ni usalama, harakati za mwalimu juu ya nchi zingine kujikomboa zilikua kubwa sana (wa umri wetu tunawakumbuka vizuri sana makaburu wa Africa kusini) aliweza kuzishawishi nchi majirani kuto kua na mahusiano na South Africa, ingawa Zaire (sasa Congo) na Malawi ilishindikana, tunajua nini kilichokua kikitokea (big up kwa usalama wa taifa wa enzi zile, akiwepo na mzee Marando). Ka-nchi kama Zanzibar, nadhani ingekua rahisi tu kurubuniwa na kua kituo cha hao jamaa, leo tunasababu gani ya kuendelea na mungano? Nakubalina kabisa na Warioba kwenye hili!
 
Back
Top Bottom