Waraka wangu wa Mwaka Mpya Kwa wana MMU …

HorsePower

JF-Expert Member
Aug 22, 2008
3,612
2,566
Wana MMU, Heri ya Mwaka Mpya 2012!

Nimepata msukumo wa ndani ya Moyo wangu kuwaandikia waraka huu, kwa upendo mwingi sana, ninyi ndugu na rafiki zangu wakubwa wa MMU nikiwashukuru kwa ushauri na ushirikiano mkubwa mliouonyesha kwa mwaka huo tulioupoteza wa 2011.
Binafsi kuingia 2012 kwangu naona kama miujiza mikubwa sana. Leo hii nilikuwa nikitafakari ndugu kadhaa ambao TUMEWAACHA ktk mwaka uliopita. Ni siku chache tu tumewapoteza watangazaji Halima na John Ngayhoma. Siku kadhaa nyuma tuliwapoteza ndg zetu wengi kutoka Zanzibar kwa ajali ya Kuzama Meli. Wapo waliobaki mwaka 2011 kwa vifo vya kikatili mno kama walioteketea kwa moto kwa ajali ya basi huko chalinze! Wapo waliopoteza maisha kwa ajali mbaya za Pikipiki za kupondwa vichwa vyao! Wapo waliobaki mwaka 2011 kwa vifo vy ajali za gari na kukatwa vipande vipande kiasi cha kushindwa kutambulika. Wapo waliobaki kwa vifo vya wenzao kujilipua kwa kujitoa Mhanga. Pia wapo waliomezwa na mafuriko na wakafa vifo vibaya kabisa vya kunywa maji machafu mpaka kifo. Vita na maandamo ya kupinga watawala dhalimu iliwabakiza wengi! Magonjwa nayo hayakubaki nyuma! Vipo vikundi vya nyimbo na burudani ambavyo pia vilibaki kwa namna mbaya ya ajali isiyoelezeka!
Siwezi kutaja kila janga na namna ambavyo wenzetu wameshindwa kuingia 2012, lakini tujiulize sisi ni nani mpaka tupate neema hii ya kuuona mwaka huu mpya? Au tumefanya jambo gani zuri la kutubakiza kwa mwaka 2012? Hebu tafakari, na mshukuru Mungu wako aliyekulinda na mabaya yote ya 2011 na kukupa neema ya kuingia 2012!

Kipindi hiki cha kuanza mwaka mpya ni kizuri sana kutafakali yale ambayo uliyapanga mwaka uliopita ukashindwa kuyatekeleza. Kwa sasa chukua muda huu, kupanga malengo yako mapya na jitahidi kuhakikisha mwaka huu unamudu kuyatimiza, uliyoyapanga mwaka huu na yale yaliyosalia ya mwaka jana.

Waliobahatika kupata ndoa mwaka 2011, mzilinde ndoa zenu. Jiepusheni na watu wanaojifanya kuwapenda angali mna ndoa, hao ni hatari kwa maisha yenu ya sasa na baadaye, waogope kama ukoma. Kamwe msijihushishe na mambo ya kukumbushia enzi na wale wa zamani, mtaumia. Kataeni aina zote za mahusiano machafu na yale yasiyo halali, muogopeni Mungu.
Kwa wale mliopoteza ndoa zenu au wapenzi wenu, poleni sana. Nawaombea Mungu ayaponye majeraha yenu mliyopewa na wenzi wenu. Nawashauri kutulia, mkiyasahau yale ya 2011 na kuanza maisha mapya 2012. Naamini ukimtegemea Mungu, iko siku utampata wa kukufaa maisha yako yote.

Najisikia kuwashauri wale wote wanaofanya kazi, tujipange mwaka huu tufanye kazi kwa bidii. Wanafanyabiashara, Wakulima na waliojiajiri kwa namna yeyote ile tukaze buti, tuweze kuyatimiza malengo yetu.
Kwa wenye familia tukumbuke kuzitunza familia zetu kwa upendo mwingi. Tukumbuke kwenda kwenye ibada mara kwa mara kumuomba Mungu atulinde na kutukinga na mabalaa ya aina zote.

Niwatakie kila namna ya mafaniko katika mwaka huu Mpya. Upendo na amani vitawale maisha yako. Mikosi ya aina zote, ajali, magonjwa, kuchukiwa bila sababu, roho ya uvivu na mateso ya namna zote yakuepuke.

Happy New Year,

HorsePower
 
Wana MMU, Heri ya Mwaka Mpya 2012!

Nimepata msukumo wa ndani ya Moyo wangu kuwaandikia waraka huu, kwa upendo mwingi sana, ninyi ndugu na rafiki zangu wakubwa wa MMU nikiwashukuru kwa ushauri na ushirikiano mkubwa mliouonyesha kwa mwaka huo tulioupoteza wa 2011.
Binafsi kuingia 2012 kwangu naona kama miujiza mikubwa sana. Leo hii nilikuwa nikitafakari ndugu kadhaa ambao TUMEWAACHA ktk mwaka uliopita. Ni siku chache tu tumewapoteza watangazaji Halima na John Ngayhoma. Siku kadhaa nyuma tuliwapoteza ndg zetu wengi kutoka Zanzibar kwa ajali ya Kuzama Meli. Wapo waliobaki mwaka 2011 kwa vifo vya kikatili mno kama walioteketea kwa moto kwa ajali ya basi huko chalinze! Wapo waliopoteza maisha kwa ajali mbaya za Pikipiki za kupondwa vichwa vyao! Wapo waliobaki mwaka 2011 kwa vifo vy ajali za gari na kukatwa vipande vipande kiasi cha kushindwa kutambulika. Wapo waliobaki kwa vifo vya wenzao kujilipua kwa kujitoa Mhanga. Pia wapo waliomezwa na mafuriko na wakafa vifo vibaya kabisa vya kunywa maji machafu mpaka kifo. Vita na maandamo ya kupinga watawala dhalimu iliwabakiza wengi! Magonjwa nayo hayakubaki nyuma! Vipo vikundi vya nyimbo na burudani ambavyo pia vilibaki kwa namna mbaya ya ajali isiyoelezeka!
Siwezi kutaja kila janga na namna ambavyo wenzetu wameshindwa kuingia 2012, lakini tujiulize sisi ni nani mpaka tupate neema hii ya kuuona mwaka huu mpya? Au tumefanya jambo gani zuri la kutubakiza kwa mwaka 2012? Hebu tafakari, na mshukuru Mungu wako aliyekulinda na mabaya yote ya 2011 na kukupa neema ya kuingia 2012!

Kipindi hiki cha kuanza mwaka mpya ni kizuri sana kutafakali yale ambayo uliyapanga mwaka uliopita ukashindwa kuyatekeleza. Kwa sasa chukua muda huu, kupanga malengo yako mapya na jitahidi kuhakikisha mwaka huu unamudu kuyatimiza, uliyoyapanga mwaka huu na yale yaliyosalia ya mwaka jana.

Waliobahatika kupata ndoa mwaka 2011, mzilinde ndoa zenu. Jiepusheni na watu wanaojifanya kuwapenda angali mna ndoa, hao ni hatari kwa maisha yenu ya sasa na baadaye, waogope kama ukoma. Kamwe msijihushishe na mambo ya kukumbushia enzi na wale wa zamani, mtaumia. Kataeni aina zote za mahusiano machafu na yale yasiyo halali, muogopeni Mungu.
Kwa wale mliopoteza ndoa zenu au wapenzi wenu, poleni sana. Nawaombea Mungu ayaponye majeraha yenu mliyopewa na wenzi wenu. Nawashauri kutulia, mkiyasahau yale ya 2011 na kuanza maisha mapya 2012. Naamini ukimtegemea Mungu, iko siku utampata wa kukufaa maisha yako yote.

Najisikia kuwashauri wale wote wanaofanya kazi, tujipange mwaka huu tufanye kazi kwa bidii. Wanafanyabiashara, Wakulima na waliojiajiri kwa namna yeyote ile tukaze buti, tuweze kuyatimiza malengo yetu.
Kwa wenye familia tukumbuke kuzitunza familia zetu kwa upendo mwingi. Tukumbuke kwenda kwenye ibada mara kwa mara kumuomba Mungu atulinde na kutukinga na mabalaa ya aina zote.

Niwatakie kila namna ya mafaniko katika mwaka huu Mpya. Upendo na amani vitawale maisha yako. Mikosi ya aina zote, ajali, magonjwa, kuchukiwa bila sababu, roho ya uvivu na mateso ya namna zote yakuepuke.

Happy New Year,

HorsePower

Tunashukuru saaaaaaaaaaaaana kwa hotuba hii tamu na ya kutuandaa kusafiri salama kwa mwaka 2012 kama tukiishi kulingana na mausia haya!! Lakin pia nipende kusema kuwa Hotuba yako imegusa kila sector isipokuwa tu mambo ya mazingira (haiko environmental friendly kabisa), climate change na madhara mengine yatokanayo na kutothamini mazingira ni janga la dunia......tukumbushane production and consumption energy efficiency based kama mojawapo ya njia kuu ya kukabiliana na tatizo hili kwa mwaka 2012
 
...tumefanya jambo gani zuri la kutubakiza kwa mwaka 2012? Hebu tafakari, na mshukuru Mungu wako aliyekulinda na mabaya yote ya 2011 na kukupa neema ya kuingia 2012!

....dahhh, ahsante kaka....heri ya mwaka mpya na maazimio yote mema tutayojaaliwa nayo kwa mwaka huu.
INSHAALLAH.
 
Asante kwa mawaidha mema na kututaka tujiandae kwa mwaka huu
Heri ya mwaka mpya pia kwako
 
Ni mimi tu sijatoa salamu/waraka wa mwaka mpya.
Ngoja niende library nikaandae....
 
Tunashukuru saaaaaaaaaaaaana kwa hotuba hii tamu na ya kutuandaa kusafiri salama kwa mwaka 2012 kama tukiishi kulingana na mausia haya!! Lakin pia nipende kusema kuwa Hotuba yako imegusa kila sector isipokuwa tu mambo ya mazingira (haiko environmental friendly kabisa), climate change na madhara mengine yatokanayo na kutothamini mazingira ni janga la dunia......tukumbushane production and consumption energy efficiency based kama mojawapo ya njia kuu ya kukabiliana na tatizo hili kwa mwaka 2012

Asante kwa maoni, ujumbe wako automatically umekuwa added kwenye waraka huu.

Many thanks,
HP
 
hapana, mimi siyo Kikwete! Mimi ni HorsePower, nipo kwa kukutakia heri ya Mwaka Mpya, sina la ziada!

Nimekusoma mkuu................nakutakia mwaka mpya mwema 2012, uumalize salama ili mwakani 2013 uje na waraka mwingine, lakini usio na matukio ya kutisha kama haya, naamini inshaallah mwaka huu utakuwa na mengi mema ya kujivunia.
 
Ahsante sana, na ubarikiwe, ni kweli wengi walitamani mioyoni mwao wauone mwaka 2012, lakini hawapo tena dunia hii, sisi ni nani, na tumetenda mazuri gani hata tukauona mwaka huu wa 2012!! tunamshukuru Mungu aliyetuwezesha kuuona mwaka huu, na kwa wale wote waliofikwa na majanga mbalimbali hata hawakuusherehrkea vizuri mwaka, tunawapa pole sana, hata hivyo na wao wanapaswa kumshukuru Mungu kwa kufika mwaka 2012
 
Back
Top Bottom