Wild Flower
JF-Expert Member
- Jul 20, 2023
- 962
- 1,909
Bajeti Kuu ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2026/27 inatarajiwa kusomwa bungeni jijini Dodoma, na kila mmoja wetu anasubiri kwa hamu kujua mwelekeo wa maisha yetu kwa mwaka ujao.
Ni bajeti ya kwanza kusomwa inayoanza kutekeleza Dira Mpya ya Taifa ya Maendeleo ya Mwaka 2050 (Vision 2050).
Akitoa mwelekeo wa dhamira ya Serikali kuelekea mwaka huu wa fedha, Waziri wa Fedha, Dkt. Mwigulu Nchemba, alisisitiza:
Wewe binafsi una matarajio gani makubwa kutoka kwenye bajeti ya kesho?
Vipaumbele vyako ni vipi?
Unadhani Serikali inapaswa kuelekeza nguvu na mabilioni ya fedha kwenye maeneo gani zaidi kati ya haya:
Ni bajeti ya kwanza kusomwa inayoanza kutekeleza Dira Mpya ya Taifa ya Maendeleo ya Mwaka 2050 (Vision 2050).
Akitoa mwelekeo wa dhamira ya Serikali kuelekea mwaka huu wa fedha, Waziri wa Fedha, Dkt. Mwigulu Nchemba, alisisitiza:
"Bajeti ya mwaka 2026/27 ni ya kihistoria kwa kuwa ndiyo inayoanza kutafsiri kwa vitendo Dira mpya ya Taifa ya Maendeleo ya 2050. Tumejipanga kuhakikisha sekta za uzalishaji zinachochewa kwa kasi ili kupanua wigo wa ajira kwa vijana, kuimarisha uchumi wa kidijitali, na kupunguza ukali wa maisha kwa mwananchi wa kawaida chini ya msingi wa kujitegemea zaidi."
Wewe binafsi una matarajio gani makubwa kutoka kwenye bajeti ya kesho?
Vipaumbele vyako ni vipi?
Unadhani Serikali inapaswa kuelekeza nguvu na mabilioni ya fedha kwenye maeneo gani zaidi kati ya haya:
- Elimu na Mikopo ya Elimu ya Juu
- Afya na Bima kwa Wote
- Kilimo, Mifugo na Ruzuku za Pembejeo
- Kodi, Biashara, na Fursa za Ajira kwa Vijana