Waraka: Kanisa Katoliki laandaa waumini uchaguzi 2010

Status
Not open for further replies.
Maana yake ni kwamba kabla hajauchana aliusoma, na hivyo ujumbe umemfikia. Atakuwa anaendelea kutafakari taratibu, halafu baadaye atakuja kuwa muhamasishaji na mgawaji mzuri wa waraka huo. Hii ni kama ilivyokuwa habari ya Paulo (Sauli).

Habari ndio hiyooo!!
 
Mwenye waraka aulete jamvini tuusome ili tuyaone hicho kilichomtia hasira Babu akaamua kuchana.
 
mtu mpumbavu na mbishi hata ukimweka kwejye chupa bado atanyoosha kidole!!!

kungunge mpuuzi sana, hebu kaone
 
Mwache auchane, kwani huo waraka ulikuwa mmoja tu? Ukimwona mtu amesimama mbele ya runinga na kuwabishia anaowaona ndani na wanachokiongea, au akaanza kuwatishia kuwachapa bakora wanaopigana ndani ya runinga, utahangaika naye? Hiyo inasaidia kumtafsiri mtu na akili zake. Kama ni kichaa au mtoto mdogo au sijui vipi! Ukipoteza muda kumfikiria mtu wa aina hiyo waliokaa pembeni watashindwa kutofautisha akili zenu.

Hivi mtu akichana msahafu mbele yako, kama una akili timamu utahangaika naye? Maana yake akichana kitabu hicho ndio ameondosha imani yako kabisa? Mjinga anazo njia nyingi za kujitambulisha katikati ya watu. Akielekezwa huwa hajambo. Lakini mpumbavu anajua anachokifanya, mwachie tu ataumbuka mwenyewe. Usimsaidie kuumbuka. Wakatoliki wanasemea ufisadi kwamba marufuku aliyeubeba kupewa uongozi. Sasa yeye kama sio fisadi anaumia nini?

Mwenezi wa CCM kwenye runinga ameonekana akisema serikali ya CCM imeagizwa na CCM yake waende wakaongee na watu wa dini zote kuhusu hizo nyaraka zao na kupata muafaka. Sasa huyo mheshimiwa aliyechana nakala tu, anapingana na chama chake anachokienzi?

Leka
 
Kwa wale ambao hamjapata kuuona huo waraka. Ni huu hapa

Nimeambatanisha na ilani ili uuelewe vizuri
 
Mzee kingunge makuzi yake ya kipagani na siasa za ndio mzee zinampeleka kunakopaswa kuwa mwisho wake sasa. selelii hakuongopa, wamelaaniwa watu hawa.
 
Jamani ule waraka ulimwagwa hapa ama kwenye post gani ? Mwenye direct link kwenye waraka aniwekee hapa tafadhali nimeutafuta sana .Nashukuru kwa msaada
 
Mkuu wangu, usidhani sikuelewi. Nina kuelewa sana tu. Nadhani nakuelewa kuliko ninavyotakiwa kukuelewa. Maelezo mengi hayawezi kunifanya nikuelewe zaidi.

Mkuu wangu labda ni summarize ninachomaanisha:
1. Waislam kama watu wengine wote nchini wanayo haki ya kutimiza sala zao kama inavyoagizwa katika maongozi ya dini. Ikiwa ni pamoja na kuwa na Mahakama ya Kadhi
2. Waraka unaoutumia kujibu hoja hapa si waraka uliotolewa kama ilani, bali ni ujumbe kwa wakatoliki (internal document). Kuna document 2 ambazo najua umeziona zote
3. Serikali haina haja, ulazima wala sababu ya kufuata ushauri kutoka kundi lolote la jamii endapo ikiona hakuna manufaa katika ajenda zake kufanya hivyo
4. Kila mtu anayo haki kikatiba kutoa maoni yake bila kuvunja sheria za nchi
5. Katiba ya nchi ni ya wote. Wenye dini na wasio na dini. Isibadilishwe kwa manufaa ya dini moja au kundi fulani la watu pekee
6. Ushiriki wa maendeleo ya jamii ni wajibu wa kila mtu ndani ya jamii. Mafundisho yoyote yanayoweza kuisaidia jamii si vibaya kutolewa na yeyote bila kujali dini yake, rangi yake, sura yake, jinsia yake, nafasi yake, itikadi yake wala umri wake n.k.
7. Makosa ya jinai yafuate mkondo wa sheria inayohusika
8. Dini zote zina lengo la kumkomboa binadamu na hasa muumini wake. Hakuna Dini bora duniani zaidi ya nyingine

Mkuu hiyo ndio imani yangu kutokana na suala hili.

Mkuu tupo pamoja ktk hili isipokuwa tu umeshindwa kunielemisha mimi sababu hujajibu kitu isipokuwa imani yako wewe.. Hujanambia sababu, malengo na dhumuni la Waraka huo kupelekwa ktk vyombo vya serikali!. pamoja na kwamba nakubaliana sana na imani yako ambayo ni imani ya kila mtu dunaani na sii Hapa JF au Watanzania pekee.. tatizo sio imani yako ama yangu isipokuwa tu ni Upana wa ibada ya vitu vinavyohusiana na imani hiyo ndipo tunapo tofautiana. Waraka wa kanisa sio part ya ilani au ibada ya Wakristu au Wakatoliki. Ni kitu kinachoongezwa kulingana na mtazamo wa watu binafsi iwe wachungaji au Maaskofu kutokana na watu na mazingira.. Ni maoni ya binadamu ambayo hayapo ktk Biblia kama ni part ya Ibada ama sala wa dini ya Kikristu, hivyo sii haki inayo.

Na hakika Lunyungu amezungumza ukweli kwamba hatuwezi kuelewana kwa sababu hata yeye mwenyewe hafahamu kinachozungumzwa hapa zaidi ya kuchukua upande..Tunaweza soma maandishi sawa ukurasa mmoja na tukafikiri tupo ukurasa mmoja lakini kile kinachoingia akilini ktk ufahamu ndio tofauti zinapotokea kutokana na mjengo wa imani zetu..Maana ya kila neno ikawa na uzito tofauti kwa kila mmoja wetu..

Kwa mfano unaposema waislaam wana kila haki ya kutimiza sala zao! hapa sidhani kam waislaam watakuelewa kwani Sala ni nguzo moja tu ya Ibada za Waislaam. Na muhimu uelewe kwamba sala kwa Wakristu huitwa Dua kwa Waislaam. Dua na sala ni vitu viwili tofauti kabisa.. yaani unapoomba Mwenyezi Mungu unafanya dua ambayo kwa wakristu - Kuomba dua ni Sala. Kwa Waislaam, sala ni ibada inayohitaji mfululizo wa vitendo fulani (rakaa) na inafuatwa na waislaam wote duniani bila kuongeza wala kupungua..
Mfano mwingine ni Pepo, Pepo kwa Wakiristu ni shetani wakati kwa waislaam ina maana yaliyopo Peponii..i.e.. Motoni kuna moto - Peponi kuna Pepo. Hivyo unaweza kuona tofauti ziliopo ktk matumizi ya maneno kati ya waislaam na Wakristu. ikiwa hujazielewa tofauti za maneno haya ni vigumu sana watu tukalewana kama ilivyokuwa taabu kwangu kumfahamisha mtu kama Lunyungu...

Yote haya yasingefikia hapa tulipo kama sote tungepata kuelewa ni kitu gani haswa wapinzani wa waraka wanakizungumzia badala ya kufikiria mbele majibu wa kanisa na kile mnachopigania...
Unajua ni jana tu nimesoma Martrydom na jinsi baadhi ya watu walivyoweza kukabiri mateso kwa jina la bwana.Jinsi Yesu, Paul, Petro, na wafuasi wote wa yesu walivyopitia mateso kabla ya kifo chao wakiendelea kuishika dini bila kupingana na serikali tawala..
Kisha nikajiuliza hivi kweli waislaam wangeweza kukubali mateso kama yale bila kuinua kidole wala mkono kujihami..Nikasema haiwezekani! Muslaam inapofikia HAKI yake hawezi kukubali kuteswa bila kuweka Upinzani mkali against the Oppressor. Na ndio maana ni vigumu sana kwa mtu akitumia imani ya dini kuweza kumwelewa Muislaam pamoja na kwamba dunia nzima leo hii hakuna mtu anayekubali mateso kulinda imani yake ila tutapambana na hao wadhalimu kwa ku address issues za haki za binadamu ktk imani zetu sote badala ya kujificha tusi sulubiwe!
 
Watu wengi wanaopinga huu waraka wanapinga tuu kwa sababu umeletwa na wakatoliki , lakini awajawa specific katika kukosoa kilichomo katika huo waraka. Mimi napinga kabisa wale wanaojaribu kufananisha huu waraka na mahakama ya kadhi, huu waraka hauitaji kodi ya walipa kodi ili kuwa implemented ! Mahakama ya kadhi inataka hela za walipa kodi zitumike kitu ambacho sio sahihi .

Nimesoma huu waraka za zaidi ya mara moja , na kusema ukweli sijaona jambo lolote baya. Halafu kitendo cha kusema kwa kuwa serikali wamekabidhiwa huu waraka basi utakuwa sheria that is plainly disingenuous. We all understand that in order to forge a law in Tanzania , the parliament has to pass a bill and then signed by the presidentis. Kila siku vyombo mbali mbali, vya kidini na NGOs, vinawasilisha waraka mbali mbali kwa serikali ili kujaribu kuishawishi serikali kuhusu mambo fulani. kwa hiyo kusema kwa kuwa serikali imepewa huu waraka basi utakuwa sheria ni kuudanganya umma.
 
Rufiji,
Mkuu kuna shughuli yoyote ya serikali ambayo haiambatani na kodi ya wananchi?
Mkuu wangu ebu tazama UNDP election support yao wanatoa kiasi gani cha fedha ktk kufanikisha uchaguzi wa mwaka 2010 ikiwa ni pamoja na elimu ya Uraia. Huo pia ni waraka na hakuna mtu anayepingana na uwakilishi wake..
Tumeandika hadi tunasahau tuliyaandika bado unadai hatujawa specific.. wapi wewe umekuwa specific na madai yako.. Nitarudia kusema kwamba hakuna mtu anayepinga waraka huu isipokuwa uwakilishi wake..na wewe unaporudia maneno hayo hayo kwa maana tofauti inajenga sura nyingine kabisa ya kutofahamu tunachozungumza.. yale yale tukisema Pepo wewe unafikiria tunazungumzia shetani..
 
Last edited:
Mkuu Mkandara, hivi ni kweli kuwa waraka huo umekabidhiwa kwa serikali? Una uhakika na hilo? Maana nijuavyo mimi, waraka uliotolewa una lengo la kuelimisha watu kuhusu uongozi bora baada ya uchaguzi mkuu wa 2010. Sasa serikali ina kazi gani na ujumbe huo? Kwa maana kuna vyama vingi, na chama chochote kinaweza kuona au kisione faida ya waraka huo na kuamua kuutumia au kuachana nao. Kuna shurutisho gani linalotaka waraka huo utumike kama mwongozo wa kuendeshea serikali, zaidi ya kuwa mapendekezo tu?
 
Rufiji,
.. yale yale tukisema Pepo wewe unafikiria tunazungumzia shetani..


Mkandara, nadhani tatizo unafikiri kila mtu anaamini katika hizi dini zilizoletwa na wazungu na waarabu , mimi siamini katika dini yeyote katika hizo! Kwa hiyo kuniweka kwenye kundi hilo uliloniweka ni makosa makubwa. Back to the topic, Sasa wewe unaona ni fair kodi yangu nitakayolipa mimi itumike kuwanufaisha kikundi fulaani cha watu ? This is ridiculous, kama wanataka hiyo mahakama basi waanzishe kwa hela zao wenyewe. Kwa hiyo kesho vipi kama dini nyingine itataka hela za walipa kodi kwa ajili ya shughuli fulani , jamani let us be serious , where are we going to draw a line ?

Mimi nasema mpaka sasa sijaona mtu aliyepinga kilichomo katika huo waraka, zaidi ya kupinga huu waraka kwa sababu tuu umetolewa na kikundi fulani cha dini. Mimi nadhani tatizo sio waraka bali ni nani ametoa waraka !
 
Rufiji,
Mkuu hapa ndipo napochoka na WABONGO yaani wepesi sana wa kugeuza fact na kuzipeleka wanakotaka wao.. Mkuu ebu rejea uloandika mwanzo, ni wewe ulosema
Watu wengi wanaopinga huu waraka wanapinga tuu kwa sababu umeletwa na wakatoliki , lakini awajawa specific katika kukosoa kilichomo katika huo waraka. Mimi napinga kabisa wale wanaojaribu kufananisha huu waraka na mahakama ya kadhi, huu waraka hauitaji kodi ya walipa kodi ili kuwa implemented ! Mahakama ya kadhi inataka hela za walipa kodi zitumike kitu ambacho sio sahihi....
Ukiwa na maana sisi tumesimama upande wa pili tunapinga kanisa katoliki pasipo sababu.. jambo ambalo sii kweli kwa sababu nimekwisha sema wazi kuwa hata kama ningekuwa Mkatoliki, uwakilishi wa waraka huu nisingekubaliana nao...Ungewakilishwa na Msikiti au Sheikh nisingeukubali, hata kama waraka huu ungeandikwa na Pagan au Mkristu ningeukubali lakini ukawakilishwa na chombo cha dini ya Kiislaaam, nisingeupokea.. Ungeandikwa na dini zote mbili sawa lakini sii kwa kutumia aya na sura za dini hizo kama dira ya waraka na mwoingozo kwa society nzima nisingeukubali..Sura na aya hutumika kama kibwagizo cha kufikisha ujumbe lakini sii mwongozo wa ujenzi wa waraka au mkakati wa kile kinachojengwa.

Nadhani unanipata vizuri kwamba nalitazama swala hili bila ushabiki..
Halafu mkuu wangu ni wapi nimesema wewe mkristu au kukupa dini? nilichosema ni kwamba hakuna shughuli ya serikali ambayo fedha za walipa kodi hazitumiki.. Kila project ya serikali ni lazima kodi yetu itumike hata kama ni Party ya kujirusha tu. Nimekuomba wewe uwe specific na kile ulichosoma na hukuona makosa.. Mfano unaposoma kifungu fulani tueleze mazuri yake kama unavyotaka sisi tuorodheshe Ubaya wa hivyo vifungu tunavyovikataa.

Recta,
Mkuu nina uhakika kuwa waraka umekabidhiwa serikalini.. sasa utabadilisha mtazamo wako?.. Labda kwa kukumbusha kidogo rejea kikao cha CCM kilichopita, utakuta kati ya agenda zilizozungumziwa ni pamoja ya waraka wa Kanisa na hata mahakama ya kadhi. Mnaopinga mahakama ya kadhi ni kwa sababu ya Uwakilishi wake serikalini sawa nasi tunaopinga vyote au wale wanaopinga Waraka huu pamoja na kwamba nguvu za vipengele baina ya mada hjzi mbili zinatofautiana.maudhui ni yale yale yakilenga waumini wa dini hizo..

Hivyo, haiwezekani kabisa serikali kujadili waraka wa katoliki na yaliyomo ikiwa Kanisa halijawakilisha waraka huo kwa vyombo vya serikali. tena basi maamuzi yamefikiwa kuwa Viongozi wa serikali watakutana na viongozi wa dini (kanisa) hiyo kujadili zaidi..kama huamini nenda site ya chama utayakuta..

Rufiji,
Mkuu nakurudia tena na kusema kwamba kama wewe huna dini haina maana nitakuelewa tofauti, kwa sababu kinachogomba hapa sii imani ya dini ila ushabiki wa dini..na ndicho nachojaribu kuepusha umma na fikra au propaganda za viongozi fulani wenye malengo msoyajua..

Labda sasa hivi nizungumze kwa herufi kubwa maanake mnashindwa kabisa kunisoma. Mimi naziheshimu dini zote lakini siamini viongozi wala waumini wake kwa ni hawa ni binadamu na wanaweza kabisa kuchuma madhambi wakitumia vyombo vya dini.. Kama tulivyowekwa Utumwani na wazungu na waarabu wakitumia dini, haina maana dini hizo zina mapungufu isipokuwa waumini wake ndio wenye mapungufu.

Hawa viongozi wetu wa dini ikiwa wanashindwa kuwakemea Mafisadi usoni ila wepesi wa kuandika waraka ambao mafunzo yake yatahitaji fedha na mikakati kuwezeshwa zoezi hili na kadhalika naichukulia hii kuwa ni mbinu ya kuchuma zaidi ya makusudio yake.

Jamani TZ watu wakishasikia tu fedha zimewtolewa na UN basi utaona NGOs zinavyojipanga iwe kanisa au Bakwata na nakuhakikishieni Bakwata nao wanajipanga sii kwa sababu wanataka kuwaelemisha wananchi isipokuwa kuna ULAJI period.

Hivyo, mimi sikubaliani kabisa na vyombo haswa hivi vya dini vinapotumiwa ktk maswala ya siasa na rahisi sana kuvuta watu kuchagua viongozi kutokana na mapendekezo ya vyombo hivi..Sijui kama una habari kuwa kuna baadhi ya wabunge huwekewa kabisa kiwango cha kuchangia baadhi ya makanisa na misikiti laa sivyo watapigwa kampeni ya kuangushwa!..Ndio wapambe wa wabunge wote nchini yaani mbunge anajipanga ktk kanisa ikutoa misaada ili akubalike na wananchi... Ni kitu tayari kinafanya kazi.
Yaani vyombo hivi sasa hivi ni mafia, na dnio maana unamwona Rostam kila kona ya wachungaji wote wa wadhehebu yote kununua Royalities zao..
Kiila msomi wa dini siku hizi deal ni kufungua kanisa au msikiti.. tena wakayapa dhehebu majina yao wanyopenda wao.. Hii hatari jamani tuweni macho na hizi imani za kijinga. It may look good lakini tujaribu kufikiria nje ya sanduku laa sivyo tutaendelea kuliwa kama Ule Upatu wa kanisa..

Tukiwaruhusu kutoa elimu ya Uraia badala ya shule zetu, kesho watatuchagulia viongozi wao na hapo sidhani kama tutaweza tena kusimamisha sheria kama tulivyoachia Mafisadi kutumia Takrima kujitangaza.

Leo hii hatuwezi tena kuondoa Takrima kwa elimu ya Uraia isipokuwa dawa ni kupiga marufuku kabisa utumiaji wa Takrima...Na Lobbiest wote ni lazima wajiandikishe, wajulikane na kiwango cha juu cap ni lazima kiwekwe kwa shirika au mtu mmoja kuchagia uchaguzi.
 
Last edited:
Jana "Askofu Mkuu" Kakobe naye akaudandia waraka wa RC na mwongozo wa Waislam kwamba utavuruga amani na utulivu wa Nchi. Akasahau kabisa aliyokuwa akiyafanya na Mrema 1995. Na leo magazeti karibu yote ya kiswahili yamempa coverage kubwa.
 
Ukiangalia historia ya Kanisa Katoliki huwa alionei haya serikali wala haiogopi. Events in the Philippines under President Ferdinand Marcos forced Cardinal Sin, the spiritual leader of all Filipino Catholics, to become involved in the politics of the region. He became witness to corruption, fraud and even murder at the hands of the regime — events that pushed Filipinos on the brink of civil unrest and even war. Sin appealed to Filipinos of all religions to follow the teachings of Jesus in the Gospels and use peaceful means to change the political situation in the Philippines. Kwa hiyo Kardinali Pengo anachofanya kisitushangaze.

Japokuwa alikaribishwa na akaenda nyumbani kwa kiongozi mmoja wa siasa aliehusishwa na RICHMOND miezi michache iliyopita na akamsifia sana. Kwa kuwa anajiona kuwa yeye ni mwakilishi wa Yesu basi alichofanya hakukosea because he is infallible.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom