napenda sana ugali..naweza kuula hata bila mboga..naula mtupu hivihivi na maji na naenjoy..i dont know why!
sasa ikitokea kuna mboga nnayoipenda sana kama vile samaki waloungwa kwa nazi au mlenda na dagaa mchele walokaangwa...aisee hilo pande la ugali ntalobeba wananishangaa
but dona siliwezi kabisaa nkila nawashwa kwenye koo panapopita chakula.
Ugali ndicho chakula nikipendacho...Nakutana na Changamoto nikimwambia wife apike hata usiku Mara nyingine hulazimika kunipikia Mimi huku wao wakila kingine wakipendacho. Wali kwangu nikila mfululizo unanikifu mnoo.
Nipate Ugali Na Mboga Kavuu, pembeni Kachumbari then liwepo Tembele, utalika ugali mkubwa sana.
Ugali dona saiz ya ngumi yangu,pembeni nyama ya kukausha,mchicha/tembele,kachumberi iliokolea ndimu,mango chatne ama pilipili ya kupikwa,kipande cha tikiti na maji yenye ubaridi kwa mbaaali
Mimi ninapenda sana kula ugali, ninaweza kula chakula hiki siku saba za juma mradi tu nibadilishe kitoweo. Kuna wanaume nikiwaeleza mapenzi yangu kwa ugali wananiona mlugaluga.
Imebidi nipunguze ulaji wa ugali kutokana na issue za uzito wa mwili. Siku hizi ninakula ugali Jumamosi tu. Kuna wanawake wanaopenda kula ugali kama mimi?