Wapenda ugali mpo?

Wapenda ugali mpo?

Mimi naweza kula ugali mwaka mzima, wali, ndizi huwa naona kama sio chakula..

Naonaga kama ni vitafunwa kwenye breakfast na sio mlo kamili.

Bila kula ugali naona kama sijala chakula kabisa.
Tukiishi nyumba moja tutaelewana sana
 
Yaani b

ila kusahau mboga za majani ninapenda sana kula na majani ya kunde, majani ya maboga, majani ya mihogo au mchunga.
Daaaaa yani mkuu wewe ni mimi kabisa yaani. Majani ya kunde, maboga huniambii kitu.

Na kuna mboga inaitwa mgagani inapatikana Kanda maalumu ila hata dar siku hizi ipo, naikubali sana
 
Naweza kula ugali kwa muda wa mwezi mmoja mkuu napenda sana iyo molo ndugu
 
utamu wa ugali muwe wengi afu upate na mishikak na kachumbari
ugali.jpg
 
Napenda sana ugali..na ukifuatilia sana walaji wa ugali wengi wanakuaga na afya.
Siri moja ya ugali una kupa nguvu nyingi. Kama kazi unayofanya haihitaji nguvu inabidi ufanye mazoezi kuunguza nguvu amasivyo ni kitambi
 
Safi sana,

Mimi napenda ugali na samaki au wali maharage.
 
Siri moja ya ugali una kupa nguvu nyingi. Kama kazi unayofanya haihitaji nguvu inabidi ufanye mazoezi kuunguza nguvu amasivyo ni kitambi
ha ha ha uko sawa kabisa mie nilijaribu kuupunguza kipindi fulani hivi maana nilikua na kakitambi amaizing!! maana kazi zenyewe nafanya za kukaa mda mrefu!!
 
Tukiishi nyumba moja tutaelewana sana
Alafu inaonekana unajali sana afya yako kupitia chakula, nimekusoma kwenye thread mbali mbali.

Mimi hiyo ni tabia ambayo ninayo, nakula chakula kwa sababu kitaniongezea kitu ndani ya mwili, sio kufuata ladha nzuri
 
Nami napenda sana ugali kila siku ila niule mchana tu usiku hapana maana hua naamka na njaa balaaa,pamoja nakupenda ugali usiwe ugali maharage.
 
Back
Top Bottom