Wanyama hawa hutabiri vifo vya wanadamu

Wanyama hawa hutabiri vifo vya wanadamu

UMASIKINI BWANA

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2013
Posts
942
Reaction score
567
Habari wana Jf.
Naandika bandiko hili baada ya kufanya utafiti Kwa muda mrefu.

Mbwa, paka, bundi wanapolia usiku Kwa sauti ya ajabu kama sauti za wanadamu wanaolia Kwa uchungu hutabiri kitu.

Utafiti umenithibitishia juzi mbwa na bundi walilia sana usiku Kwa mfululizo Jana tumezika MTU mtaani kwetu. Hali hii imekuwa ikitokea Mara Kwa Mara wanyama na ndege huyo wanapolia.

Mbwa hulia Kwa kuweka mdomo juu.Paka hutoa sauti isiyo ya kawaida Kwa kubana koo lake. Bundi hutoa mlio Kwa sauti nene yaani bass.

Mwenye zaidi karibuni [emoji250] [emoji240] [emoji211]
 
Habari wana Jf.Naandika bandiko hili baada ya kufanya utafiti Kwa muda mrefu.Mbwa,paka,bundi wanapolia usiku Kwa sauti ya ajabu kama sauti za wanadamu wanaolia Kwa uchungu hutabiri kitu.Utafiti umenithibitishia juzi mbwa na bundi walilia sana usiku Kwa mfululizo Jana tumezika MTU mtaani kwetu.Hali hii imekuwa ikitokea Mara Kwa Mara wanyama na ndege huyo wanapolia.Mbwa hulia Kwa kuweka mdomo juu.Paka hutoa sauti isiyo ya kawaida Kwa kubana koo lake.Bundi hutoa mlio Kwa sauti nene yaani bass.Mwenye zaidi karibuni[emoji250] [emoji240] [emoji211]
Imani za Kimasikini hizi Bwana!!
 
Kitambo ulikuwa ukimuona njiwa kasimama mguu mmoja pia walisema uchuro.
 
Habari wana Jf.
Naandika bandiko hili baada ya kufanya utafiti Kwa muda mrefu.

Mbwa, paka, bundi wanapolia usiku Kwa sauti ya ajabu kama sauti za wanadamu wanaolia Kwa uchungu hutabiri kitu.

Utafiti umenithibitishia juzi mbwa na bundi walilia sana usiku Kwa mfululizo Jana tumezika MTU mtaani kwetu. Hali hii imekuwa ikitokea Mara Kwa Mara wanyama na ndege huyo wanapolia.

Mbwa hulia Kwa kuweka mdomo juu.Paka hutoa sauti isiyo ya kawaida Kwa kubana koo lake. Bundi hutoa mlio Kwa sauti nene yaani bass.

Mwenye zaidi karibuni [emoji250] [emoji240] [emoji211]
imani tu hizo. kuna siku bundi lilikuja likalia mlangoni kwangu usiku, likatoka likapanda juu ya paa likaendelea kulia, likatoka likaenda kwenye mti fulani mbele ya nyumba yangu likaendelea kulia,
Dadek! nikaona linanizoea nikatoka na boonge la jiwe nikalitupia na kulikemea likakimbia zake sikuumwa na kichwa wala kalio mwaka wa pili sasa!
 
Nikiwa naishi Mbeya, kulikuwa na mzee mmoja, alikuwa na matatizo ya akili, alikuwa na ngómbe wengi, siku anafariki hospitali [ni mbali na nyumbani kwake] ngómbe walilia usiku kucha.

Tukio kama hilo likajirudia tena mwaka huu nikiwa Magu, Mwanza, jamaa wana ngómbe nyumbani kwao, yeye ni dereva wa bodaboda, akpata abiria akampeleka mbali na mji, kule wakamuua na kumtupa porini, ngómbe wao walilia usiku kucha, kesho yake asubuhi maiti ikaokotwa.
 
Inawezekana wana uwezo ambao unawawezesha kuona mambo mabaya yanapokuwa yanatufuatilia binadamu,ila sina uhakika kwani sina ushahidi wowote juu ya hili,ingawa nakumbuka wakati nikiwa mdogo kuna ndugu yetu alikuwa mgonjwa sana,na wiki moja kabla ya kufariki kwake bundi walikuwa wanalia sana,ingawa pia eneo tulilokuwa tunaishi wakati huo lilikuwa ni pori mabundi yalikuwa mengi sana kwahiyo sijui ilikuwa ni coincidence au yawezekena hiyo myth ina kaukweli flani..?
 
Haina uhalisia wowote labda kiidogo ungeniambia njiwa ningekuolewa huku wetu mbwa paka bundi wanalia hiyo miliyo kila leo lakini hamna lolote linalotokea
 
Habari wana Jf.
Naandika bandiko hili baada ya kufanya utafiti Kwa muda mrefu.

Mbwa, paka, bundi wanapolia usiku Kwa sauti ya ajabu kama sauti za wanadamu wanaolia Kwa uchungu hutabiri kitu.

Utafiti umenithibitishia juzi mbwa na bundi walilia sana usiku Kwa mfululizo Jana tumezika MTU mtaani kwetu. Hali hii imekuwa ikitokea Mara Kwa Mara wanyama na ndege huyo wanapolia.

Mbwa hulia Kwa kuweka mdomo juu.Paka hutoa sauti isiyo ya kawaida Kwa kubana koo lake. Bundi hutoa mlio Kwa sauti nene yaani bass.

Mwenye zaidi karibuni [emoji250] [emoji240] [emoji211]
Hapa napoishi paka wanalia daily na wanakufa wao wanatuacha sisi...
 
Siku baba yangu mzazi anafariki usiku mbwa walikua wanalia sana mpaka mdogo wangu akawa analalamika kua hawa mbwa c kawaida kulia hivyo usiku huohuo baba yangu alifariki Rip my dady
 
Back
Top Bottom