Wangapi washaisikia hii ya marehemu Hemed Maneti?

Wangapi washaisikia hii ya marehemu Hemed Maneti?

Bingwaman

JF-Expert Member
Joined
Oct 22, 2010
Posts
548
Reaction score
288


Marehemu Hemed Maneti alirekodi kibao hiki jijini Nairobi mwaka 1981 akishirikiana na mwanamuziki Mtanzania aliyekuwa na makao yake katika jiji hilo wakati huo, marehemu Charles Ray Kasembe. Santuri inaonyesha kuwa wimbo huu umepigwa na Vijana Jazz, lakini hii si sahihi. Hii ilikuwa ni jitihada binafsi ya Maneti nje ya Vijana Jazz.
 
Last edited by a moderator:
Charles Ray Kasembe alikuwa ni mpiga rhythm katika bendi ya Super Volcano ya marehemu Mbaraka Mwinshehe. Alibaki nchini Kenya na kuanzisha bendi ya Les Volcano baada ya kifo cha Mbaraka mwaka 1979. Alikuwa ni kiongozi, mpiga solo na mwimbaji katika Les Volcano. Katika wimbo huu, Kasembe amepiga solo huku akishirikiana na Maneti kuimba. Kasembe alirudi nyumbani mwaka 1989 na kujiunga na bendi iliyokuwa ikimilikiwa na Muungano Cultural Troupe. Alifariki dunia miaka michache baadaye.
 
Sahihi kabisa, unatukumbusha mengi, isitoshe ni kama waliwahi kupiga pamoja katika bendi moja, walipishana kidogo sana (Maneti na Charles) wakati Maneti anakaribia kutoka TK Lumpopo mwishoni mwa 1973 ndipo Charles Ray Kasembe naye alipokuwa akijiunga na bendi hiyo. Huenda kufahamiana huko japo kwa muda mfupi ndipo kulipojenga mashirikiano kutengeneza kibao hiki. Charles Ray Kasembe hatimaye naye alitoka TK Lumpopo na kujiunga na Super Volcano (jambo adimu sana wkati huo yaani kutoka kwa Kilaza kwenda kwa Mbaraka ama kinyume chake lilikuwa jambo gumu).
 
Juma Kilaza RIP
Sahihi kabisa, unatukumbusha mengi, isitoshe ni kama waliwahi kupiga pamoja katika bendi moja, walipishana kidogo sana (Maneti na Charles) wakati Maneti anakaribia kutoka TK Lumpopo mwishoni mwa 1973 ndipo Charles Ray Kasembe naye alipokuwa akijiunga na bendi hiyo. Huenda kufahamiana huko japo kwa muda mfupi ndipo kulipojenga mashirikiano kutengeneza kibao hiki. Charles Ray Kasembe hatimaye naye alitoka TK Lumpopo na kujiunga na Super Volcano (jambo adimu sana wkati huo yaani kutoka kwa Kilaza kwenda kwa Mbaraka ama kinyume chake lilikuwa jambo gumu).
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom