Guasa Ambonii
JF-Expert Member
- Aug 13, 2015
- 8,545
- 10,296
Nimesoma bandiko lako kisha nikamfikiria mtunzi namna alivyo kuwa katika mashimo ya Mfalme Suleiman namna watu weupe wale walivyotumia nguvu na akili zao ili haki ipatikane ili kuwaaminisha watu waweza kuwakubali waliwaambia mambo ya kupatwa kwa mwezi na kweli tukio likatokea na watu kuanza kuwakubali tizama namna walivyo mpigania faulata ambae angetolewa kafara usiku ule wa ngoma.Sina sababu ya kupingana na wewe katika hili, ila jambo moja ni dhahiri nalo ni kwamba vilifanya watu wasome sana na kufurahia hadithi hizo...mimi nakumbuka nikiwa darasa la tatu Mwalimu wa Kiswahili alikuwa anatusomea hadhithi kutoka kitabu kile cha Mashimo ya mfalme Suleiman mpaka unajona kuwa labda uko katika nchi ya wakukuana...Yaani kila wakati tulikuwa tunaomba Jumanne ifike haraka tupate kusikia tunavyosomewa hadithi ile, na mwalimu yule alikuwa anasoma kwa mbwembwe mpaka raha....
Kuna mabaya mengi ya wazungu lakini kuna mazuri mengi pia...Sasa whether mabaya yanazidi mazuri au mazuri yanazidi mabaya this is a subject for discussion....
Wakakubali kupigana bega kwa bega na umbopa mpaka akapata haki yake iliyo chukuliwa na mfalme twala alie muua baba yake umbopa.
Kumbe tunaweza kupanua ufahamu wetu na kila mtu akatoa mtizamo wake chanya kuhusu hivi vitabu vya kale.