Wanaweza???

yani hili baraza liko weak sana,hivi huyu machemli angeweza kweli bomoabomoa kama ya magufuli! jamani tuache ushabiki hili baraza lisingetufikisha popote yani hapo naona vichwa viwili tuu au nchi ingeongozwa na kina sabodo au maaumuzi magumu kutoka kwa pengo au vatican

Acha udini wewe..........huo ni ukosefu wa fikra na ujinga.........
 
Kaka acha ussumptions hapa. wewe siunawajua walioshinda na walioshindwa ebu tupe list ya mawaziri kwa ufahamu wako

Mak, Mr.

Sina list ya wagombea wote walioshindwa na wenye uwezo wa kuwa mawaziri halisi. My point is, pool ya kuteua ingekuwa kubwa. Na katika wale kumi wa kuteuliwa angeweza kuniweka hapo mimi, sasa si unaona ningepiga kazi vizuri tu (joke)? Au na mimi unanifutilia mbali kama hao hapo juu kamanda?

Siwezi kupinga kwamba mawaziri vivuli wanaweza wasiweze kazi ya uwaziri kamili. Ila tuwapime kwa watakachofanya kama mawaziri vivuli.

Lakini, hao wa CCM miaka nenda rudi ambao wamekuwa sio mawaziri vivuli bali mawaziri halisi wameweza? Najua hawajaweza, kwa hiyo tungalie chanzo cha kushindwa pia.
 
tusiendelee kuwa na fikra mgando. Kuna mfano wa project moja huko India ambako wakulima wa vijijini walibadilishwa na kuadopt kilimo cha kisasa pamoja na mfumo mzuri wa kutunza kumbukumbu na hesabu! Ndipo coordinator wa hiyo project alipo hitimisha kwa kusema kuwa "kumfundisha mtu asiye mwaminifu kutunza pesa ni kumpa njia zaidi za kukuibia". Huoni kuwa hiyo ndiyo tofauti kati ya 'wateule' wa CDM na thi thi emu??
 
bwana mdogo Joseph Kabila (29yrs) aliweza..........

The U.N. Stabilization Mission in the DRC said it was stepping up its presence in the area. At least 8,000 rapes were reported by humanitarian agencies in the DRC in 2010...
 
kaka hujui kama wadhamini wa chadema kama ni hao jamaa aliowataja Kashaga? Na pia akina Pengo wanajicholesha wanapoonekana kifua mbele kukitetea chadema. wao kama viongozi wa kiroho hawatakiwi kuonesha hisia zao dhahiri shahiri.Mnaowashangilia waangalieni sana wasituletee ya rwanda, maana walianza hivohivo.

Evidence!...
 
The U.N. Stabilization Mission in the DRC said it was stepping up its presence in the area. At least 8,000 rapes were reported by humanitarian agencies in the DRC in 2010...

How about unreported rape cases in Tanzania? Kila kiongozi ana changamoto zake. Kwa maana hiyo unataka Nyerere afufuke aje kuongoza nchi? Tunaweza kuiongoza nchi yetu kirahisi tu kama tutawajibika na kuwa waadilifu. Mimi ninaweza kuwa rais, waziri au kiongozi wa ngazi yoyote inayoendana na taaluma yangu katika nchi hii, hali kadhalika wanajf wengine. Kama wewe huwezi, nenda kajitakase.
 
Hilo Baraza lako la ccm linakusaidia nini sasa hivi,mpaka unajadili baraza kivuli la upinzani, mwisho wa siku na baraza lako la ccm ni kilio tu cha maisha yamepanda nk
 
Nililiangalia baraza kivuli la mawaziri lililoundwa na upinzani bungeni.. nikaassume endapo kama Dr. Slaa angepita hili ndilo lingekua baraza lake la mawaziri..

Msemaji ofisi ya Raisi: Freeman Mbowe,
Msaidizi: Silinde David
Uwekezaji na Uwezeshaji: Matiko
Ofisi ya Waziri Mkuu: Vicent Kiboko
Ofisi ya Raisi: Said
Ofisi ya Raisi & Utawala Bora: Mch Nakse wa Karatu
Ofisi ya Makamu wa Raisi: Gekulu
Ofisi ya Raisi & Mazingira: Leticia Nyerere
OFisi ya Fedha: Zitto Kabwe Msaidizi: Christina Lissu
Mambo ya Ndani: Lema
Katiba ya Sheria: Tindu Lissu
Kimataifa: Wenje
Jeshi la Ulinzi: Seladhini
Mawasiliano: prof Kayili
Makazi: Mdee
Maliasili: Mch Peter Msigwa
Nishat na Madini: Mnyika
Ujenzi: Machemli
Uchukuzi: Mhonga Said
Viwanda: Olenywa
Elimu na Mfunzo: Mtinda
Afya: Dr Gilbert Mbasa
Maendeleo ya Jamii: Naomi Kaiula
Vijana na michezo: Mbilinyi Mr Two
Kilimo: Meshack Obulugwa
Maji: Haines Kiwia
NB:- Kama kutakua na changes ni kidogo sana!.

Tujiulize viongozi hawa wangetufikisha tunakoenda?? Manung'uniko, migogoro, majanga, umasikini na kuzorota kwa elimu na mengine kama haya yangeendelea kuwepo au wangefanikiwa kuyakabili??..



Mr Sugu nae si ungempa wizara ya Tamaduni Habari na Michezo ili aifungie Clouds?
 
Jibu gumu swali rahisi.

CHADEMA wangeshinda nafasi ya Uraisi kwa idadi hiy hiyo ya wabunge? Huoni factors ambazo zingewawezesha CDM kushinda uraisi zingewawezesha kushinda nafasi nyingi zaidi ya wabunge hivyo mawaziri wangetoka kwenye pool kubwa zaidi? Na kama Dr. Slaa angeshinda angeteua wabunge kumi kwa mujibu wa Katiba huoni kwamba angeweza kuteua watu wenye uwezo pia kama hao mawaziri vivuli hawawezi?

Maswali mengine ni ya kipuuzi sana. Ni sawa nikuulize ungezaliwa wa kike ungeolewa au ungekuwa msagaji? Hapo unajibu vipi? Yote hayo yanategemea various factors.

Mawaziri Vivuli Chadema unaweza kuwapima kwa utendaji wao kama mawaziri vivuli. Huna haja ya kufanya assumption, wana majukumu yao kama mawaziri vivuli kwa hiyo wapime kwa kutumia utendaji wao na sio assumption.

Karibu.


Ha ha ha.Jamaa uko right
 
Back
Top Bottom