Wanawake wenzangu, je ulivyo ndivyo upendavyo?

Wanawake wenzangu, je ulivyo ndivyo upendavyo?

Karibu sana bi dada. Nafurahi kusoma uzi kama hizi za kuonyesha watu waliomo kwenye ndoa na wanaishi kwa maelewano hata kwenye afya zao wanashirikiana kwa faida zao binafsi na familia husika. Ni nadra sana kukuta habari kama hizi hapa JF, ni kuponda tu mahusiano na ndoa wanaume hivi wanaume vile, wanawake hivi wanawake vile lakini kuna Watanzania chungu nzima wanafurahia mahusiano yao ndoa zao pamoja na majaribuni chungu nzima yaliyokuwepo.
Mawasiliano ni kitu cha msingi sana katika ndoa, lucky me i married my best friend kwahiyo mambo yetu tunashirikishana.
Changamoto hazikosekani kama binadamu, ila kwa msaada wa Mungu tunajitahidi kuzitatua.
 
Yaani Mungu ni mwema kitambi kimenipita kushoto, ila ningekuwa nacho ningepambana tu maana hamna namna
Hongera yako mama, kitambi kinakera asikuambie mtu, nilikuwa nachelewa kazini kisa kuchagua nguo ya kuvaa, kila nivaayo naona haifai navua navaa nyingine, sio siri kinakera.
 
Hongereni sana. Changamoto katika mahusiano/ndoa KAMWE hazikosekani kikubwa ni mawasiliano na kukaa chini kuamua nini cha kufanya ili muweze kuendelea na mahusiano yenu ndoa yenu badala ya kununiana mume anaingilia huku na mke anaingilia kule full kununa.. Hata vikombe viwili ukiviweka pamoja lazima vitagongana sembuse binadamu.

Mawasiliano ni kitu cha msingi sana katika ndoa, lucky me i married my best friend kwahiyo mambo yetu tunashirikishana.
Changamoto hazikosekani kama binadamu, ila kwa msaada wa Mungu tunajitahidi kuzitatua.
 
Karibu sana bi dada. Nafurahi kusoma uzi kama hizi za kuonyesha watu waliomo kwenye ndoa na wanaishi kwa maelewano hata kwenye afya zao wanashirikiana kwa faida zao binafsi na familia husika. Ni nadra sana kukuta habari kama hizi hapa JF, ni kuponda tu mahusiano na ndoa wanaume hivi wanaume vile, wanawake hivi wanawake vile lakini kuna Watanzania chungu nzima wanafurahia mahusiano yao ndoa zao pamoja na majaribuni chungu nzima yaliyokuwepo.
Hahahaaaa!! Yaani ni ponda nikuponde. Kwakweli inatia moyo.
 
Msiache mazoezi kiukweli unaweza kudhani ni kupambana na vitambi tu lakini ukweli ni kwamba pia mnakimbiza magonjwa mbali mbali yanayosababishwa na kufutuka kupita kiasi ikiwemo magonjwa ya moyo, blood pressure etc.

Hongera yako mama, kitambi kinakera asikuambie mtu, nilikuwa nachelewa kazini kisa kuchagua nguo ya kuvaa, kila nivaayo naona haifai navua navaa nyingine, sio siri kinakera.
 
Hongereni sana. Changamoto katika mahusiano/ndoa KAMWE hazikosekani kikubwa ni mawasiliano na kukaa chini kuamua nini cha kufanya ili muweze kuendelea na mahusiano yenu ndoa yenu badala ya kununiana mume anaingilia huku na mke anaingilia kule full kununa.. Hata vikombe viwili ukiviweka pamoja lazima vitagongana sembuse binadamu.
Ni kweli mkuu, alafu haya mambo bwana lazima mmoja ajifanye boya wakati mwingine ili mambo yakwende. Wote mkiwa juu mambo hayasongi.
Upendo wa dhati,mawasiliano,kuheshimiana,kuwa na shukrani,kila mmoja atambue nafasi yake, kubwa zaidi kumshirikisha Mungu(kwa waaminio).
 
Mawasiliano ni kitu cha msingi sana katika ndoa, lucky me i married my best friend kwahiyo mambo yetu tunashirikishana.
Changamoto hazikosekani kama binadamu, ila kwa msaada wa Mungu tunajitahidi kuzitatua.
Aisee nimekupenda bure wa dada yaani ulivyo proud na mume wako!
Sio hawa wanawake wengine pasua kichwa hadi basi!
anyway mungu anifanyie wepesi muda ukifika
Hongera sana
 
Aisee nimekupenda bure wa dada yaani ulivyo proud na mume wako!
Sio hawa wanawake wengine pasua kichwa hadi basi!
anyway mungu anifanyie wepesi muda ukifika
Hongera sana
Nilimchagua awe mume wangu kati ya wooote niliowaona sasa kwanini nisiwe proud nae!! Nampenda,namthamini na kumheshimu sana mume wangu. Sikukosea kumchagua, namuomba Mungu azidi kutupigania.
 
Safi sana, ndoa ni tamu sana hasa pale mwanaume anapopata msaidizi na sio mke pekee. Wewe ni moja ya wanawake wenye hekima wanaojenga nyumba zao na kuzifanya imara zaidi
 
Hongera sana. Huu uzi uliojaa mazuri kuhusu ndoa wengi huukimbia hutawaona humu lakini ungekuwa umekuja kuandika mabaya kuhusu ndoa saa hizi ungekuwa umeshafika page 30.

Nilimchagua awe mume wangu kati ya wooote niliowaona sasa kwanini nisiwe proud nae!! Nampenda,namthamini na kumheshimu sana mume wangu. Sikukosea kumchagua, namuomba Mungu azidi kutupigania.
 
Safi sana, ndoa ni tamu sana hasa pale mwanaume anapopata msaidizi na sio mke pekee. Wewe ni moja ya wanawake wenye hekima wanaojenga nyumba zao na kuzifanya imara zaidi
Nashukuru mkuu, pia namshukuru Mungu na mama yangu pia.
 
Back
Top Bottom