Watunduru
Senior Member
- Dec 29, 2011
- 170
- 39
nina rafiki yangu wa kawaida tu si kimapenzi, mwanadada mjasiriamali mama wa watoto wawili na kwa sasa ni mbunge pia,ktk bunge letu tukufu.ki maumbile si haba kwani ktk kundi la warembo nae yumo.miezi miwili iliyopita alinieleza jambo ambalo kwake alidai linamkosesha raha ktk maisha na jambo lenyewe ni kukimbiwa na kila mwanaume anaempata.alidai kuna wakati huamka usiku na kulia machozi juu ya hali hiyo kwa kujihisi mwenye balaa,na kwamba ameshazunguka kwa waganga wasio na idadi bila mafanikio.nilipojaribu kumtia moyo ikawa kama nimejipalia mkaa kwani aliongeza ukaribu na mimi mara dufu na kuanza kunichukulia kama mr wake.japo sikuwahi kukutana nae kimwili niliweza kubaini mapungufu yake ktk muda huo nikajiweka pembeni mapema kabla sijamgusa mheshimiwa.kasoro moja kubwa aliyonayo ni kumfanya mwanaume kama house boy wake,yeye ni mtu wa kutoa maagizo,maelekezo na amri hali ambayo mwanaume yoyote anaejitambua hawezi kuvumilia.nimebaini kumbe hayuko peke yake,kuna wimbi kubwa la wanawake wasomi wanaomudu maisha vizuri kutokana na ajira au biashara lakini upande wa ndoa mambo si mazuri,na walio na ndoa utagundua waume zao ni wale wanaume suruali,nikakumbuka au ndio sababu hata bosi wa mjengoni nasikia hana ndoa!?kumbe huko kote mbali,hapa jf tunao kina dada wanajitokeza kutaka waume lakini ukipitia maelezo yao utagundua ndo walewale kutokana na masharti wanayoweka.hebu tujiulize inawezekanaje mwanamke ana zaidi ya miaka 30 hajaolewa na asiwe na kasoro au hila yoyote?mimi nawapa ushauri wa bure dada zangu hawa kwamba njia pekee ya kuondokana na upweke unaowakabili ni wao ndio waoe wasingoje kuolewa.wako wanaume tegezi kwa wanawake bila kujali kama wananyanyasika au la,hawa ndio suluhisho la kudumu.ni mtazamo tu,
Karibuni kuchangia
Karibuni kuchangia