Kipenzi Chao
Member
- Oct 12, 2010
- 99
- 4
Mkuu kuna haya yafuatayo;Inashangaza sana, wanaume tukitoka nje ya ndoa huwa tunarudi na nidhamu tu na zawadi kedekede nyumbani na malavidavi ya kutosha kwa mama watoto. Lakini wao wakitiwa nje basi nyodo mtindo mmoja ndani, kwanini lakini???
- Huwa wanasema wanandoa wakiishi pamoja kwa muda mrefu hufanana....! Tafadhali sana, kufanana kwao sio kwa sura, bali kwa tabia....! Hivyo, kama sio mkeo kakuridhisha tabia hiyo, basi uwe makini usije ukamridhisha yeye siku za mbeleni....!
- Uelewe kuwa wanawake wengi huwa wanaadhibu kimyakimya....! Hivyo, kama mkeo atakauwa ameshtukia, basi uanze kujua kuwa kunyamaza kwake si bure, bali ni kwa kuwa anajua ngoma droo...!
- Hayo maneno ya kimadongo unayopewa na wezi wenzio kuhusu nyumba zao lazima kuna moja katika haya; aidha nawe unamkandia mkeo mbele yao, au hawana akili nzuri kabisa, na hivyo unatembea na wajinga, vichaa, malaya, machangu, na wasiofaa kuigwa katika dunia hii....!
- Ninavyoamini mimi ni kwamba kila afanyacho binadamu kwa mwenzie mara nyingi huwa ni kujaribu kufidia guilt ya yale yaliyowahi kumtokea naye kwa kufanyiwa na binadamu wengine...! Hivyo, huenda hata unavyofanya ni kujaribu kubalanzisha uliyofanyiwa nawe huko nyuma...! Na kama ndivyo nikupe pole, lakini nikushauri kuwa hiyo sio tiba ya hasira....!
- Vinginevyo; kumbuka misemo haya; "Asiyesikia la mkuu huvunjika guu" na "Asiyefunzwa na mamaye, hufunzwa na ulimwengu"....! So, angalia usivunjike guu au usije fundishwa na ulimwengu kwa vitendo....! Maana naona kama bado umelala kabisa....!