Wanawake stress nyingine tunazitafuta

Wanawake stress nyingine tunazitafuta

Kwa hilo wanawake wengi sana tunafeli,binafsi sihangaikagi na simu ya Mpenzi wangu, aongee wapi achati sijui afanye nini wala sijipi presha, maisha mafupi kwann niteseke kwa vitua ambavyo naweza kuvihandle???Unakuta wamama wanafundishana kuhack simu za wanaume wao, nawaangaliaga nawaona wajinga fulani hivi, unahack unapata presha unakufa unamuacha anaendelea na maisha, ya nini bwana, mie nnachojali ananipa haki yangu vzr ananitimiza vyote nnavyopata basiiii,nampa uhuru wake na maisha yanasonga,na hatujawahi gombana eti kisa simu
Wanawake kama nyie mnaowapa waume zenu uhuru wa kuchepuka ndo huwa mnahitajika sana na wanaume malaya na ndo huwa mnaitwa 'wife material' hongereni
 
Hahahahaahhahahahaahahhahahahahahahahahahahahahahahhaahhaha hebu nijitahidi niwe kama hivi uwenda nikadumu kwenye mahusisno lol...


Nilivyo na gubu hivyo simu ipigwe ukaongee chumbani asalaleeeeeeeeee vita ya hapo si ya mchezo
Hebu utulie tutafute ada ya watoto.
 
Na katika huo uhuru ndiyo anapata na dili ya buashara na wewe na watoto mkapelekwa Zanzibar weekend
You are such an optimist my sister congratulations because being positive in everything is a talent
 
Mmekaa sitting room mnaangalia taarifa ya habari, simu ya mr inaita, anaamka anachukua simu, ameamua kuongelea chumbani. Baada ya maongezi anarudi anakukuta mwanamke umeumuka kama umetiwa hamira, aliyepiga simu ni nani?

Kama ungetakiwa kumjua au kujua wanayoongea asingeenda chumbani, yeye ni mtu mzima anahitaji privacy yake. Kama anataka kukopa hela je?

Mimi ninaamini kama katika wote amenichagua mimi, hata akitoka wala sina wasiwasi ninajua atarudi. Simu ikipigwa ninampelekea kama yuko mbali, hata kama caller’s name ni Joyce siulizi kwani mwenye pete ya ndoa ni mimi.

Uache kulala usingizi wako mzuri unamsubiri mtu ambae yuko kwenye bata lake huko au ndiyo anashughulikia ada za watoto. Mradi tu awe na adabu ya kunijulisha kuwa atachelewa.
Aiseee una akili saaana.
 
Mmekaa sitting room mnaangalia taarifa ya habari, simu ya mr inaita, anaamka anachukua simu, ameamua kuongelea chumbani. Baada ya maongezi anarudi anakukuta mwanamke umeumuka kama umetiwa hamira, aliyepiga simu ni nani?

Kama ungetakiwa kumjua au kujua wanayoongea asingeenda chumbani, yeye ni mtu mzima anahitaji privacy yake. Kama anataka kukopa hela je?

Mimi ninaamini kama katika wote amenichagua mimi, hata akitoka wala sina wasiwasi ninajua atarudi. Simu ikipigwa ninampelekea kama yuko mbali, hata kama caller’s name ni Joyce siulizi kwani mwenye pete ya ndoa ni mimi.

Uache kulala usingizi wako mzuri unamsubiri mtu ambae yuko kwenye bata lake huko au ndiyo anashughulikia ada za watoto. Mradi tu awe na adabu ya kunijulisha kuwa atachelewa.
Nitampa mke wangu huu ujumbe asome.
 
Mimi nadhani bado hatujaelewana hakuna anayetaka mume wa kumsujudia bali ninachojaribu kusema ni kwamba kama wewe mume kufuatiliwa na mkeo hautaki kwanini na wewe umfuatile mkeo? Kama wewe hautaki mkeo akufuatilie halafu wewe unamfuatilia mkeo hiyo ina maana gani?

Ina maana hayo makosa unayotaka kuyakuta kwenye simu yake unataka uyafanye wewe tu ila yeye asiyafanye? Unajua wanaume mnashindwa kukikubali hiki kitu kimoja kinaitwa KARMA yaani 'what goes around comes around' kila unalolifanya haijalishi liwe ni zuri au baya lazima likurudie kwa namna yoyote ile na wakati wowote ule hauwezi kuizuia hiyo hali

Yaani ukichapa wake au watoto wa kike wa wenzio na wewe wako lazima watachapwa tu sasa hauwezi kulazimisha wewe uwe malaya halafu upate mwanamke muaminifu wapo wanaopata wake wa hivyo lakini wajuvi wa mambo wanasemaga "in every general rule there is always an exception"

Kwahiyo katika hiyo general rule ya KARMA hao ambao wanayofanya hayawarudii basi ndo exception yenyewe lakini ni asilimia chache sana sasa nyie wanaume mnataka mfanye hayo kwa wanawake wengine halafu yasijirudie kwa wake zenu na yakijirudia ndo mnaanza kusema wanawake tunafanya makusudi ili kuwalipizia sijui tunashindana na nyie hizo kauli mnatoa wapi jamani?

Halafu kwani shetani huwaga anawatendesha dhambi wanaume tu? Yaani hiyo dunia mnayoitaka ambayo wanaume wanafanya makosa halafu wanawake hawafanyi makosa haipo haijawahi kuwepo na haitakuja kuwepo mtu akipata mke au mume pasua kichwa ndo wake huyo

Anatakiwa akumbuke tu mambo aliyofanya kwa wenzie huko nyuma halafu Mungu alivyo wa ajabu sasa mara nyingi watu wanapata wenza wa kufanana nao tabia with the the exception ya baadhi ya watu sasa whether you are among or not among the exceptions wewe shukuru tu Mungu yaani shukuru kwa yote

Sasa cha kuomba ni kupata mume muaminifu ila sio kulazimisha mume wako awe muaminifu. Kama hujabahatika kupata jamaa anayeheshimu hisia zako to an extent asiwe ana cheat ukapata kichaa ujue utateseka sana.

Piga sana dua, wanaume tunatofautiana sana. And from a closer look you seem to be so controlling. Hio sio character nzuri try to change.
 
Wanawake kama nyie mnaowapa waume zenu uhuru wa kuchepuka ndo huwa mnahitajika sana na wanaume malaya na ndo huwa mnaitwa 'wife material' hongereni
Nikwambie kitu hata ukimbana mwanamme akiamua kuchepuka atachepuka tu,atafanya yake mchana wa jua kali halafu saa kum na mbili yuko home, pia nadhani hadi mtu kuchepuka anakuwa kadhamiria toka moyoni mwake, hivyo bwana mie sihangaikagi kwa kweli
 
Back
Top Bottom