Wanawake stress nyingine tunazitafuta

Wanawake stress nyingine tunazitafuta

Sio Kuchepuka tu, bali kufanya mambo yako kwa uhuru bila kufatiliana na kuchunguzana kama vile umefuga Li FBI ndani.
Mara nyingi wanawake hua mnaongozwa na hisia, unaweza ukahisi tu jambo bila hata kua na ushahidi wa uhakika halafu ukaleta tafrani ndani ya nyumba mpaka nyumba inageuka kua ni uwanja wa vita.
Sasa jamani si wanaume wenyewe mnakiri kuwa hakuna mwanaume asiyechepuka chini ya jua? Nyie wenyewe ndo mnawajengea wake zenu hiyo mentality kuwa hakuna mwanaume asiyechepuka kwahiyo wanaingia kwenye ndoa wakiwa na mawazo kwamba nina mume anayechepuka sasa hapo haina haja ya ushahidi tena maana mmeshayafanya maneno yenu kuwa ni sheria
 
Mmekaa sitting room mnaangalia taarifa ya habari, simu ya mr inaita, anaamka anachukua simu, ameamua kuongelea chumbani. Baada ya maongezi anarudi anakukuta mwanamke umeumuka kama umetiwa hamira, aliyepiga simu ni nani?

Kama ungetakiwa kumjua au kujua wanayoongea asingeenda chumbani, yeye ni mtu mzima anahitaji privacy yake. Kama anataka kukopa hela je?

Mimi ninaamini kama katika wote amenichagua mimi, hata akitoka wala sina wasiwasi ninajua atarudi. Simu ikipigwa ninampelekea kama yuko mbali, hata kama caller’s name ni Joyce siulizi kwani mwenye pete ya ndoa ni mimi.

Uache kulala usingizi wako mzuri unamsubiri mtu ambae yuko kwenye bata lake huko au ndiyo anashughulikia ada za watoto. Mradi tu awe na adabu ya kunijulisha kuwa atachelewa.
Ujumbe mzuri sana,Mimi nikinyanyuka kwenda kuongea na simu lazima waifu anifuate kwa nyuma,kumbe naongea na ndugu zangu,
 
Hahahahaahhahahahaahahhahahahahahahahahahahahahahahhaahhaha hebu nijitahidi niwe kama hivi uwenda nikadumu kwenye mahusisno lol...


Nilivyo na gubu hivyo simu ipigwe ukaongee chumbani asalaleeeeeeeeee vita ya hapo si ya mchezo
Eeeh afadhali; maana nilijua mimi tu ndo nimebaki kwenye kundi la non-wife material. Eti akapokelee simu wapi? Aaaaaah weeeeeeeeeee
Subiri tuzeeke tutakuelewa.
 
Wanawake kama nyie mnaowapa waume zenu uhuru wa kuchepuka ndo huwa mnahitajika sana na wanaume malaya na ndo huwa mnaitwa 'wife material' hongereni
by nature kila mwanaume ana tamaa
 
Back
Top Bottom