Wanawake nao wapaza sauti zao kuhusu uteuzi wa MA -DAS

wakati wa kugawa vitenge ilikuwa wanawake 100% na wanaume 0%. Wasubiri vitenge vichakae, 2020 watapewa vitenge vingine. CCM wanajua hitaji kubwa la wanawake ni vitenge, na wanatimiza hilo kwa juhudi sana kuwaokoa kushindia vimini
 
watu wote washabiki wa ukawa wanaongla ishu za tuzi kama kulipana fadhila, hii ndio inaonyesha jinsi walivyojipanga kulipana fadhila kama wangeshinda chaguzi kwa nafasi ya urais na ndio maana mgombea wao alipewa nafasi za upendeleo za viti maalumu bila kujali demkrasia
 
Kuna malalamiko kwamba uteuzi hauja zingatia jinsia , haiwezekana katika ma DAS 137 walio teuliwa wanawake wawe 21 tu . Wakati dunia inataka 50% kwa 50% jinsia zote katika vyombo vya maamuzi inaonekana kuna mipango ya kurudisha nyuma jitihada hizo. Tuishauri serikali yetu tukufu kwani hao wanawake ni 28.7 % .ya walio teuliwa
Wanawake ndio wapiga kura wazuri kipindi cha uchaguzi tuwakumbuke kwenye vyeo
 
Hii term hatuangalii SURA na CHURA mlizonazo.

Tunaangilia ELIMU na UWEZO wa kwenda na kasi ya HAPA KAZI tu.

Teh! Fanyeni kazi, mlizoea mbeleko za UWT na CCM.
Mkuu hebu fafanua hilo neno "CHURA" linamaanisha nini hasa, maana ninahisi kama kuna kitu kimefichika nyuma yake.
 
Na aendelee kuwatosa hao kina mama maana walizidi kuishabikia ccm
Mlipoambiwa BAWACHA wanapewa viti maalum kwa rushwa mlikuja juu
sasa Mmawia ww unataka DAS wa Rombo au ukampokee Anna Kilango Malecela
Magu alishaumwa na nyoka subirini 2025
 
Mi naona hata hao 21 wamependelewa,kam mtu hana uwezo hamna sababu ya kumteua huu siyo ule wakati wa kujuana zama hizo zilishapita
 
Watu wanataka kutugombanisha tu na wanawake, wenyewe mbona hawana mpango na uongozi ukitaka kuthibisha hilo angalia tu idadi ya waliojitokeza kugombea uraisi halafu linganisha na wanaume utajua ni kwa jinsi gan wanawake wanataka uongozi
 
Na aendelee kuwatosa hao kina mama maana walizidi kuishabikia ccm

Enzi zao zimepita, awamu ya nne alikuwa anawapa tu kwa kigezo cha 50/50. Huyu jamaa anataka kazi tuu. Hivi alipowaambia HAPA KAZI TU hamkuelewa!!! Tatizo mlikuwa mmekazana kuimba mapambio " wacha waisome namba" mnasahau vitu vya msingi.

Na msipochapa kazi hata hao wachache mtapigwa chini. Enzi za reception na bodymass 8 zimekwisha. HAPA KAZI TU, hiyo 50/50 mtasubiri sana.

Ushauri, WANAWAKE jengeni uwezo, sio kusubiri nafasi za upendeleo, hatuwezi kuwa na taifa la upendeleo pendeleo tu, watu wanajipendekeza ili wapte kazi wakati uwezo zero matokeo yake tunaajili na kulipa mishahara kwa VILAZAA
 
Kwanza tunatakiwa kuelewa kuwa Tanzania ni sehemu ya Dunia, lakini Dunia siyo sehemu Tanzania. Hivyo maamuzi ya kiutawala na mengineyo yanafanyika kwa kuzingatia mazingira, dira, dhima, sera na mipango ya Tanzania siyo Dunia. Pili usawa wa kijinsia ni dhana kubwa kuliko U-DAS. Yaani ndani ya usawa wa kijinsia kuna U-DAS na mengineyo lakini katika U-DAS hakuna usawa wa kijinsia.
 
Back
Top Bottom