Kakende
JF-Expert Member
- Aug 18, 2012
- 2,741
- 1,233
Wadau ukifika Arusha mjini utaona hali ya kusikitisha, wanawake na baadhi ya vijana wamejaa mji mzima, kila kona ya mitaa wanauza Nyanya na mbogamboga mbalimbali katika maeneo ambayo uwezi kudhania kuwa mtu anaweza kuuza mboga za majani.
Kibaya zaidi ukifika pale friends corner(opposite to CRDB bank) utakuta baadhi yao wanauza nyama mbichi ya kuku, yaani kuku anakatwa vipande. Nyama hizo ni fresh kabisa, hazifunikwi, nzi wanarukia, vumbi, watu wanapita nk, bibi afya wamelala.
Kuuza nyanya ni sehemu ya maisha, ni kujishughulisha, lakini inatakiwa iwe katika sehemu iliyo rasmi, lakini hapa utaona wametandika vigunia chini kila eneo. Kuijishghulisha ni muhimu sana, mimi ningeona wako kwenye mashamba ya uzalishaji wa mbogamboga, wanazalisha na kufungasha kupeleka hata kwenye soko la nje hapo sawa, lakini kinachofanyika hapa ni indicator ya umasikini
Anyway, ukifikiria utagundua kuwa watu hawa wamekata tamaa, wanatafuta angalau cha kuingia kinywani, wanatafutia watoto wao. Hakuna viwanda, hawana elimu watafanyaje!. Maisha ya Mtanzania yamekuwa magumu, Mtanzania sasa anaona umaskini ni sehemu ya maisha yake ndiyo maana ukija uchaguzi anapigia chama kilekile kilichojigawia nyumba za umma, kuua viwanda, sasa ni zamu ya meno ya Tembo.
Vipi mikoa mingine, hali ikoje?
Concept yangu iko hivi. Nchi yoyote ambayo umaskini umekithiri utaona mji mzima vijana ni machinga, watu wanauza utumbo wa kuku, wengine wanauza karanga, kila kijana ni dereva pikipiki ili mradi apate jinsi ya kuishi siku hiyo. Lakini kama kungekuwa na mpango mzuri, tungeona wanawake na vijana wamewezeshwa, mfano wangekuwa wanashona nguo kwa wingi na ku export nje. Kwa taarifa yenu hizi nguo tunazoagiza kutoka nje zote zinatengenezwa kwa mikono ya watu waliopewa mafunzo ya hali ya juu. Ninachomanisha ni hiki hapa chini
Hawa wanashona nguo kwa mikono na ku export
Tazama wa huku kwetu Arusha city center, hapa si sokoni kabisa, ni nje ya maduka
Kibaya zaidi ukifika pale friends corner(opposite to CRDB bank) utakuta baadhi yao wanauza nyama mbichi ya kuku, yaani kuku anakatwa vipande. Nyama hizo ni fresh kabisa, hazifunikwi, nzi wanarukia, vumbi, watu wanapita nk, bibi afya wamelala.
Kuuza nyanya ni sehemu ya maisha, ni kujishughulisha, lakini inatakiwa iwe katika sehemu iliyo rasmi, lakini hapa utaona wametandika vigunia chini kila eneo. Kuijishghulisha ni muhimu sana, mimi ningeona wako kwenye mashamba ya uzalishaji wa mbogamboga, wanazalisha na kufungasha kupeleka hata kwenye soko la nje hapo sawa, lakini kinachofanyika hapa ni indicator ya umasikini
Anyway, ukifikiria utagundua kuwa watu hawa wamekata tamaa, wanatafuta angalau cha kuingia kinywani, wanatafutia watoto wao. Hakuna viwanda, hawana elimu watafanyaje!. Maisha ya Mtanzania yamekuwa magumu, Mtanzania sasa anaona umaskini ni sehemu ya maisha yake ndiyo maana ukija uchaguzi anapigia chama kilekile kilichojigawia nyumba za umma, kuua viwanda, sasa ni zamu ya meno ya Tembo.
Vipi mikoa mingine, hali ikoje?
Concept yangu iko hivi. Nchi yoyote ambayo umaskini umekithiri utaona mji mzima vijana ni machinga, watu wanauza utumbo wa kuku, wengine wanauza karanga, kila kijana ni dereva pikipiki ili mradi apate jinsi ya kuishi siku hiyo. Lakini kama kungekuwa na mpango mzuri, tungeona wanawake na vijana wamewezeshwa, mfano wangekuwa wanashona nguo kwa wingi na ku export nje. Kwa taarifa yenu hizi nguo tunazoagiza kutoka nje zote zinatengenezwa kwa mikono ya watu waliopewa mafunzo ya hali ya juu. Ninachomanisha ni hiki hapa chini
Hawa wanashona nguo kwa mikono na ku export
Tazama wa huku kwetu Arusha city center, hapa si sokoni kabisa, ni nje ya maduka