Wanawake Arusha wanasikitisha, vipi mikoa Mingine?

Wanawake Arusha wanasikitisha, vipi mikoa Mingine?

Tatizo sio wanauza nini tatizo mitaji haikui kwa sababu kila kukicha maandamano na kila maandamano tegemea hasara wataendelea kuuza majani mpaka wafie uko na lema akiendelea kuwachezea kama zombie
 
hivi kii bora kati ya kuuza kuku mbichi barabarani au kuuza mwili?
 
Ukiacha mazingira, wanawake Arusha ni wahangaikaji/watafutaji sana. Kupitia biashara zao halali za kuuza nyanya na mchicha wanalea familia, wanalipa kodi na kusomesha watoto.

NI KWELI KABISA, WAMAMA HAWA WA ARUSHA MJINI WANAJITAHIDI JAMANI. WANASOMESHA WATOTO, WANALISHA FAMILIA, WANALIPA KODI ZA NYUMBA, WANAJENGA NYUMBA ZAO ZA KUISHI, WANATUNZA WABABA( BAADHI YA WABABA HAWAFANYI KAZI YOYOTE YA KUINGIZA KIPATO. KAZI YAO KUBWA KUSHINDA VIJIWENI WAKITEGEMEA JASHO LA WAMAMA HAWA). WAMAMA HAWA HAWALALI JAMANI. NAWAPA POLE SANA, NAWAOMBEA KWA MUNGU JASHO LAO LISIMWAGIKE BURE. Hakika wachacharikaji sana. Saa kumi na moja asubuhi utawaona barabarani, kwenye toyo na kwenye vifodi na mafurushi makubwa ya mboga za majani wanawahi soko kuu, Kilombero na Samunge(soko lililipo uwanja wa NMC) kuuza mboga kwa bei ya jumla. Wengine wana watoto mgongoni. Ukirudi mabustanini kuna wanaolima hizo mboga wanahangaika kunyweshea maji usiku na mchana na kupeleka mboga kuuza au kuwauzia wenzao wanaokwenda kuuza jumla au rejareja. Kukipambazuka ndo utawakuta wanavyochacharika na uuzaji wa mboga, nyanya, vitunguu, n,k katika maeneo hayo yasiyo rasmi. Utawaona na vigunia vyao wametandika chini, watoto migongoni wanahangaika kubembeleza wapita njia wanunue. Ghafla utaona wananyanyua mifuko na vigunia vyao na kukimbia. Kisa? Mgambo katokea anawafukuza wasiuzie bidhaa katika maeneo hayo!!!!!
Shida hii ya kufanya biashara maeneo yasiyo rasmi inatakiwa iangaliwe kwa mapana zaidi. Sababu kubwa ni kuwa watu ni wengi wakati mji ni mdogo. Watu wamejazana sana pale eneo la kuzunguka soko kuu, NMB na CRDB bank hadi uhuru Road wakiuza vitu kwa sababu pia kuna wanunuzi wengi tu. Uwingi wa watu/walaji na mji mdogo ndilo tatizo. Kinachopaswa kufanywa ni kupanua mji na kuhamishia soko kuu na stand ya mabus makubwa nje ya mji kwenye maeneo kama vile Murieti, Moshono, Usa river, Kisongo, Korona, Lengijave, n.k. Kwa kufanya hivyo basi kutakuwa na mtawanyiko wa watafutaji na si kulundikana sehemu moja kiasi hata magari yanakosa pa kupita. Huu ni mtazamo wangu. Naomba kuwasilisha.
 
Wanajitapa na lema wao mbona kabla yalema hayakuwepo hayo kwanza arusha ilikua safi sana but huenda naye lema akawa ni shina la hayoo mambo kutokea.
 
Huuu ulioandika ni ujinga we ulitaka wauze uchi?think big unadhani arusha ni hollywood watu wote waekti muv
 
Huuu ulioandika ni ujinga we ulitaka wauze uchi?think big unadhani arusha ni hollywood watu wote waekti muv

Nadhani hukuelewa namaanisha nini. Nchi yoyote ambayo hali ya umaskini imekidthiri utaona asilimia kubwa ya watu wanakimbilia kazi ya aina moja tena ambayo ni rahisi kufanya. Kitendo cha mji mzima kuona watu wametandika vigunia chini wanauza nyanya, wengine wanauza karanga, wengine utumbo wa kuku, kila kijana machinga, kila kijana dereva pikipiki si jambo la kujivunia. Hapo kuna dalili ya umasikini, inamaanisha kuwa wengi hawana mbinu mbinu mbadala ndiyo maana wanahamua kufanya hivyo.
 
hivi kii bora kati ya kuuza kuku mbichi barabarani au kuuza mwili?

Tatizo nchi haina viwanda, ndiyo maana utaona wanauza utumbo wa kuku, wanaume dereva pikipiki nk. Sasa kama wewe unaona hiyo ni sign nzuri basi
 
Mkuu Kakende nakubaliana nawe kuwa ni indicator ya umaskini na kweli kwamba wanajitutumua japo mkono uende kinywani ila sehemu wanayofanyia biashara hizo haziendani kabisa na sii salama kwa afya ya mlaji na muuzaji pia. Na hii inatokana na kudekezwa kwa kutetewa na mbunge wao. Arusha ni jiji ila kwa hali hiyo hata hadhi ya jiji haipo tena na Mh. Lema anapaswa kuwaelimisha wapiga kura wake ili vitu vitendke kwa utaratibu.
 
Last edited by a moderator:
Hivi nyie si mlisema arusha ndio wasomi na maisha bora ndiomana mnawapenda wa bunge wa cdm sisi tunaowabunge wa missm ndio mnatuita mi masikini mimi naona kwetu huwa wanatengewa soko lao na wanauza mbogamboga na matunda kama kawaida sio kama arusha huko kwenye wasomi kwetu kigoma sivyo wakina mama wanauza nyanya kwenye soko lao la mbogamboga ma matunda waliotengewa nyambafu
 
Back
Top Bottom