Wanawake acheni kuvaa mawigi

Kuna wale Team Mawigi sugu hata ukiwaletea habari za google wataona kama unawazingua, labda mpaka wao wenyewe wakutane nazo wenye maombi

Huwa napata shida sana kuwaza unawezaje kusimama na kuanza kumshukuru Mungu kwa uumbaji wake halafu kichwani umemkosoa kwa kuweka vitu ambavyo yeye hakukuumba navyo. Unakuta midude migumu kwa ndani mtu kashonwa na nyuzi kichwani yaani kisa fashion halafu ngoja uzi uachie bahati mbaya huwa nacheka sana kwani wengine niko nao ofisini mara ooo naomba nirekebishie
 
Wamekubali, after all mawig mnavaa mtuvutie, na sis hayatuvutii Tupa Kule, kuwa simpo tu,
 

Duh aise,nimeupenda uzi huu.
 
Wewe Sonko, Jr umeleta mjadala mzuri sana. Kwa kweli wazungu ni 'washenzi' kweli kweli. Yaani wanatuletea mawigi eti tufanane na wao. Nashukuru mke wangu havai mawigi ila mabinti zangu weeee ni shida. Sijui sisi waafrika tukoje. Nikiwaambia mabinti zangu ambao nawamudu majibu yao hunikatisha tama. Yaani utasikia wanasema wewe baba sisi tunakuheshimu na tunakupenda na umetusomesha ila tunakuomba utuache na haya mawigi kwani ndiyo mambo ya kileo...huwa nabaki nashangaa. Angalau nashukuru jambo moja. Mabinti zangu hawajagusa mikorogo. Yaani jamani mikorogo ni shida kuliko mawigi. Mimi niliwaambia mabinti zangu kuwa wakianza mikorogo nachukua panga na kuwashughulikia sitaki ujinga huo.....
 
Mawigi kwa mwanamke ni kerooo kupitiliza,mwanamke hata akinyoa au abaki na vipilipili inavutia zaidi kuliko kuvaa mawigi.
 
bhaaaasss! mie mwenyewe kichuna nipo naturaliiii, staki shida!
 
Mimi kila siku ndo ugomvi wangu na wife, ijapokuwa ana nywele ndefu nzuri na nyeusi lakini bado na mawigi sijui maweaving hata simwelewi hawa wanawake wetu ni shida
 

Mikorogo noma. . Sasa ukute mkorogo umekolea, wig hizo bangs mpaka haoni mbele, utachoka
 

Hahaha my kaka bana, but wifi akinyukaga weaves zake si huwa unamsifia hata kimoyo moyo au?
 
Hata mumwange povu kiasi gani maweaving na wigi zitavaliwa tu na wanawake as long as wana exist on planet. Kama hamjui hata wazungu hutumia weaving
 
Wamekubali, after all mawig mnavaa mtuvutie, na sis hayatuvutii Tupa Kule, kuwa simpo tu,

Nani kakwambia wanawake huvaa au kujiremba kwa akili ya kuvutia wanaume. Hyo perceptions yako ni wrong
 
Hata maua yanapendeza na harufu tamutamu, kuita nyuki, ili uchavushaji a.k.a uzazi uendelee, we unampendezea Nani kama sio sisi?
 
Hahaha my kaka bana, but wifi akinyukaga weaves zake si huwa unamsifia hata kimoyo moyo au?

Siyo kimoyo moyo namsifiaga kiwazi wazi ila ndo hivyo kinafiki, coz mnalazimisha hayo madude wanaume wengi hatuyapendi, hope umeona mwenyewe walivyotiririka humu

Mnayapenda nyie kwa nyie tu kwa kweli
 
Hata mumwange povu kiasi gani maweaving na wigi zitavaliwa tu na wanawake as long as wana exist on planet. Kama hamjui hata wazungu hutumia weaving

Nani kakwambia wanawake huvaa au kujiremba kwa akili ya kuvutia wanaume. Hyo perceptions yako ni wrong

Mmh basi sawa
Ila wengine tulishajiandaa kisaikolojia, so vaeni tu
 
Siyo kimoyo moyo namsifiaga kiwazi wazi ila ndo hivyo kinafiki, coz mnalazimisha hayo madude wanaume wengi hatuyapendi, hope umeona mwenyewe walivyotiririka humu

Mnayapenda nyie kwa nyie tu kwa kweli

Hahaha my kaka buana, kwa nini kusifia wakati roho haipendi teh
 
Mmh basi sawa
Ila wengine tulishajiandaa kisaikolojia, so vaeni tu

Bora tu mjiandae kuwa mwanamke ndiko kunakopelekea hayo yote kupenda kujipamba mionekano yao. Tofauti tofauti
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…