Wanaume wengi ni katili sana kulinganisha na wanawake

Wanaume wengi ni katili sana kulinganisha na wanawake

Lanlady

JF-Expert Member
Joined
Feb 27, 2019
Posts
1,913
Reaction score
6,524
Habari! Ni matumaini yangu mu wazima wa afya, kama kuna wagonjwa poleni sana; nawaombea mpate afya haraka kwa uwezo wa Mola!

Sasa, leo naomba tuzungumze kidogo kuhusu tabia za baadhi ya wanaume. Kama tujuavyo wengi, kwa mila na desturi za kiafrika; mwanaume ndiye huanza kutafuta au kutaka mahusiano na mwanamke. Mwanamke anaweza asiwe tayari kutokana na sababu mbalimbali lakini mwanaume anaweza kutumia mbinu za ushawishi ili awe na huyo mwanamke.

Baada ya muda mwanamke anaamua kukubalia kuwa na mahusiano na huyo mwanaume. Ni jambo la kawaida kwasababu za kimaumbile, si rahisi kuishi peke yako siku zote.

Cha ajabu ni kwamba baada ya muda kupita, mwanaume yule yule aliyetumia kila aina ya ushawishi kumpata mwanamke aliyemhitaji, anaanza kumdharau, kumtesa na pengine hata kumsimanga kwa yale aliyomfanyia. Mfano pesa, mtaji wa biashara nk. Huu ni ukatili.

Mwanaume unapoamua kumshawishi mtu kwa namna yoyote ile, inabidi ujiandae kwa matokeo utakayoyapata! Usianze kulalamikia pesa au mali ulizotumia kwa ajili yake. Huo ni ukatili wa kihisia!
 
Kama naanza kukuelewa vile, ila sijapata kujuwa ukatili wa mwanaume uko wp!! please explain in detail 🙏🙏🙏🙏
 
Habari! Ni matumaini yangu mu wazima wa afya, kama kuna wagonjwa poleni sana; nawaombea mpate afya haraka kwa uwezo wa Mola!

tili wa kihisia!
Mwanamke ukishakuwa na bei watu wakapanda umeisha, Mimi hununua jinsi kali na kuipenda siku ile ile inapokuwa dukani nikivaa mara moja thamani yake inaporomoka kama hela ya malawi.
 
Mwanamke ukishakuwa na bei watu wakapanda umeisha, Mimi hununua jinsi kali na kuipenda siku ile ile inapokuwa dukani nikivaa mara moja thamani yake inaporomoka kama hela ya malawi.
Utakuwa hujaipenda bali uliitamani.
Na ndio maana unapaswa kujihakikishia kama kitu unachohitaji ni kwa matumizi ya muda mrefu au mfupi
 
Hueleweki
Mbona inaeleweka sana!
Yaani kama umeamua kuchumbia au kuoa, inabidi uwe tayari kwa mazuri na mabaya. Na ikitokea mtu uliyemchumbia hakupi matokeo uliyotarajia, haipaswi kumchukia kwasababu hakukulazimisha uwe naye! Kama mnaachana muachane kwa amani na sio kumtafutia visa na kumnyanyasa kisa tu ulimtunza au kumpa mahitaji
 
Na wewe umesahau ukatili wa kijinsia uliomfanyia jamaa yetu hivi majuzi?

Umemuita mpaka ghetto kwako alafu ukaishia kumnyima mbususu? Unajua maumivu aliyoenda nayo jamaa yetu?

Upigwe matukio mpaka ukome.
Hakuitwa. Alijipeleka mwenyewe.
Isitoshe ni mbishi. Anaambiwa kupima afya hataki. Na wakati ni mtu na mke wake na bado ana wengine wengi.
 
Habari! Ni matumaini yangu mu wazima wa afya, kama kuna wagonjwa poleni sana; nawaombea mpate afya haraka kwa uwezo wa Mola!

Sasa, leo naomba tuzungumze kidogo kuhusu tabia za baadhi ya wanaume. Kama tujuavyo wengi, kwa mila na desturi za kiafrika; mwanaume ndiye huanza kutafuta au kutaka mahusiano na mwanamke. Mwanamke anaweza asiwe tayari kutokana na sababu mbalimbali lakini mwanaume anaweza kutumia mbinu za ushawishi ili awe na huyo mwanamke.

Baada ya muda mwanamke anaamua kukubalia kuwa na mahusiano na huyo mwanaume. Ni jambo la kawaida kwasababu za kimaumbile, si rahisi kuishi peke yako siku zote.

Cha ajabu ni kwamba baada ya muda kupita, mwanaume yule yule aliyetumia kila aina ya ushawishi kumpata mwanamke aliyemhitaji, anaanza kumdharau, kumtesa na pengine hata kumsimanga kwa yale aliyomfanyia. Mfano pesa, mtaji wa biashara nk. Huu ni ukatili.

Mwanaume unapoamua kumshawishi mtu kwa namna yoyote ile, inabidi ujiandae kwa matokeo utakayoyapata! Usianze kulalamikia pesa au mali ulizotumia kwa ajili yake. Huo ni ukatili wa kihisia!

Mtu akishasema hataki unamshawishi kitu gani?
Kubembeleza bembeleza Sana nako NI kujivunjia tuu heshima.

Yaani unamtongoza Dada MTU mzima let say anamiaka 25+ alafu amekukatalia na ametoa sababu zake, bado uendelee kumshawishi😂😂 huo nao ni utoto.

Mambo hayo tuliyafanya tukiwa Sekondari,

Sisi wengine tunajua Mwanamke akisema hapana tunaamini na kuheshimu hapana yake, akisema ndio tunaamini na kuiheshimu ndio yake.

Vijana lazima wafundishwe, MTU mzima habembelezwi wala hashawishiwi tena kwenye ishu ya Ndoa ndio kabisa a
 
Mwanaume sio katili mwanaume ana msimamo hasa hasa pale mwanamke anapoleta ujinga ujinga.. mwanamke ni kiumbe hatari ewe mwanaume usimwonee mwanamke huruma.. ishi na mwanamke kwa akili tuu utakuja kushukuru sana
 
Back
Top Bottom