Tunaomba fanya analysis pia kwa wadada wa JF,(wewe pia ukiwemo)
Unachopaswa kukumbuka ni kwamba,hao wanaume na wanawake wa JF ndiyo hao hao waliopo mtaani,hawa wa humu hawana dunia yao peke yao!
Kubwa zaidi ni kwamba,katika jamii yoyote,kuna watu wa aina mbali mbali,wapo wenye busara zao,na wapo wenye mizaha mingi,na wapo wajinga wajinga,lakini pia wapumbavu hawakosekani, na hii sio kwa wanaume tu,hata wanawake!
Kwa mfano,tazama mada za baadhi ya wanawake walio wake za watu hapa MMU,wanavyojiachia kuelezea nia au namna walivyotombwa na wanaume wasio waume zao,tena kwa kujisifia kabisa,(hayo ni maadili?)
Kikubwa si kuwalaumu wanaume,tuseme ukweli kwamba kizazi hiki kimepotoka,na shetani amefanikiwa sana kukiponda ponda, namna ya kutoka hapa sio nyepesi,inahitaji nguvu kubwa,ukatili kidogo,na uvumilivu wa hali ya juu sana, vinginevyo kwa siku za usoni,hali itakuwa mbaya zaidi!