nzalendo
JF-Expert Member
- May 26, 2009
- 12,733
- 14,160
Ina upana wake ndio maana wengine wanahamia Dodoma.Wapenzi wangu, habarini
Msemo huu unazidi kuwa maarufu siku baada ya siku. Mwanzoni sikuutilia maanani sana.
Juzi nilikuwa kijijini kwetu, kijijini kabisaa!! Nikamsikia kijana mmoja anamwambia mwenzake "... Mimi sio mwanaume wa Dar..."
Leo nikiwa katika daladala, yakatokea Majibizano kati ya Kondakta na abiria.
Pamoja na maneno mengi Kondakta aliyoongea, neno hili nililishika ipasavyo "... Mimi siwezi kujibizana na wanaume wa Dar.."
Swali langu, mwanaume wa Dar ni nani? Anatambulikaje?
Kazi kwa watakao baki.
