Wanaume tupendane, tusiharibiane ndoa

Joel360

JF-Expert Member
Sep 21, 2013
981
631
Leo naomba niongee na wanaume wenzangu.

Kwanini sisi wanaume hatupendani?

Tunawalaumu wanawake kuwa hawapendani ilihali na sisi pia hatupendani. Nitaeleza kwanini nasema hivi.

Unakuta mtu kwa makusudi anafahamu kuwa huyu mwanamke ni mke wa mtu. Mwanaume mwenzangu kamtolea mahari, kajipiga piga kufanya sherehe na anafanya kazi kwa bidii ili kumtunza mkewe(japo maisha yana changamoto nyingi sana) lakini bado atamtongoza (mke wa mtu) na atalala nae.

Kwani mbona kuna watu hawana huruma na wanaume wenzao namna hii? Ina maana hawafahamu kuwa wanachokifanya ni kuharibu ndoa na nyumba ya mwanaume mwenzake?

Au ndio tumekosa upendo kiasi hicho? Ndugu zangu kama sisi wanaume tungekuwa tunapendana kusingekuwa na visa vya kufumaniana na wake za watu.

Tufikie hatua za kuwatakia heri wenzetu waliooa, tusiwe sehemu ya kuvuruga ndoa zao. Sikatai kuna baadhi ya wanawake ukiwa unamtongoza ukimuuliza ikiwa ameolewa anakataa, lakini mara nyingi wanawake huwa wawazi kuwa wameolewa.

Wanaume tupendane, tusiharibiane ndoa.

NB: Hakuna lolote lililonisibu, nimeandika kwa kuzingatia jinsi mambo yalivyo katika jamii.
 
Hivi wewe una akili sawa sawa kweli?! Sasa umeanza vipi kusema wanaume hatupendani kisha ukahusianisha na swala la mkeo kutoka nje ya ndoa?!

Unajua katika hali ya kawaida, inapotokea mkeo katoka nje ya ndoa unatakiwa kumuwajibisha mkeo kwa kuvunja kiapo cha ndoa na si mwanaume mwenzako kwani yeye hamkufunga ndoa.

Kwanza umshukuru mwanaume mwenzako anapokuonyesha madhaifu ya huyo unaemwita ni mkeo sababu ameamua kusaliti ndoa yenu. Unaanzaje kulaumu mwanaume mwenzako.

Umesahau ile kanuni ya 'Bros before whores'
 
Wanawake wenyewe ndio wanakuwaga na Shobo na wanaume unakuta mke wa mtu mara akutumie msg 'Mambo' au mara akupigie anachoongea hakieleweki sasa unadhani huyo anataka nn😠😠😠
 
Leo naomba niongee na wanaume wenzangu.

Kwanini sisi wanaume hatupendani?

Tunawalaumu wanawake kuwa hawapendani ilihali na sisi pia hatupendani. Nitaeleza kwanini nasema hivi.

Unakuta mtu kwa makusudi anafahamu kuwa huyu mwanamke ni mke wa mtu. Mwanaume mwenzangu kamtolea mahari, kajipiga piga kufanya sherehe na anafanya kazi kwa bidii ili kumtunza mkewe(japo maisha yana changamoto nyingi sana) lakini bado atamtongoza (mke wa mtu) na atalala nae.

Kwani mbona kuna watu hawana huruma na wanaume wenzao namna hii? Ina maana hawafahamu kuwa wanachokifanya ni kuharibu ndoa na nyumba ya mwanaume mwenzake?

Au ndio tumekosa upendo kiasi hicho? Ndugu zangu kama sisi wanaume tungekuwa tunapendana kusingekuwa na visa vya kufumaniana na wake za watu.

Tufikie hatua za kuwatakia heri wenzetu waliooa, tusiwe sehemu ya kuvuruga ndoa zao. Sikatai kuna baadhi ya wanawake ukiwa unamtongoza ukimuuliza ikiwa ameolewa anakataa, lakini mara nyingi wanawake huwa wawazi kuwa wameolewa.

Wanaume tupendane, tusiharibiane ndoa.

NB: Hakuna lolote lililonisibu, nimeandika kwa kuzingatia jinsi mambo yalivyo katika jamii.
Wewe endelea kuwaonea huruma wanaume wenzako wakati mke wako anagongelewa misuli bila huruma na hao wanaume.
 
Kwani amembaka?

Mwanamke ndiye mwenye nafasi ya kukataa au kukubali labda afanye kubakwa!

Ndiyo maana michepuko wanawake wanastahahili kuwajibishwa sababu pale wanapojua fika kuwa Mwanaume fulani ana mke tena wengine unakuta hata siku ya ndoa mchepuko alikuwepo lakini anashupaza shingo kwa kilanga na njaa na kuroga !

Mimi naona wanaume michepuko wala sio kivile lakini wanawake michepuko ndio waharibifu wa ndoa na madhara yao kwenye welfare ya ndoa ni makubwa na mabaya sana.

Mke wa ndoa akichepuka atapelekea cash inflows kwenye ndoa au hata akiliwa bure sawa iwapo wenyewe wanapendana
Kwa dhati ya moyo.

Lakini kwa Mwanaume wa ndoa kuchepuka ni hasara kwa familia coz inapelekea cash outflows kwa kwenda kumhonga mchepuko mwanamke nje !

Lipokuja swala la uchawi,

Mchepuko Mwanaume anayechukua mke wa mtu siyo rahisi atafute kumroga yule mume wa ndoa au kumroga mke wa mtu anayemchukua siyo rahisi na kwa hiyo madhara ya uharibifu kwenye ndoa huwa ni nadra sana.

Lakini kwa Mwanaume wa ndoa kuchepuka na mchepuko mwanamke nje ya ndoa huwa ni kinyume chake.

Ndo maana Imeandikwa asiachwe mwanamke mchawi kuishi.
 
Mpaka mwanamke kuchepuka ujue imerahisishwa sana na mwanamke mwenyewe kwa tamaa zake mwenyewe kutafuta pesa , au ni tabia alishazoea
Kubadili mabwana, au umemvuruga pengine alikuamini sana kisha ukam-disappoint mkeo
Sana sasa amegundua hujatulia unamdhalilisha kwenye jamii Kwa hiyo ana revenge kwa kuwa ujue kabla na baada ya kumuoa
Mke ujue kuna wanaomuimbishaga kumtaka sema aliamua kukutunzia
Heshima na kumuogopa Mungu .

Sasa akijakujua wewe unachepuka beyond reasonable mashaka basi jipange kukabiliana na kitakachofuata iTV.

Wanaume michepuko huwa hawanaga hila ya uharibifu.

Hawalengi kumchuna mkeo, hawahitaji kununuliwa gari na mkeo, hawalengi kusomeshewa watoto wao wa kufikia na mkeo,

Hawalengi kulipiwa kodi ya nyumba na mkeo,

Hawalengi kujengewa nyumba na mkeo,

Hawasingizii kufiwa au kuuguliwa ili wamchune mkeo hela, n.k

Ndiyo maana nakwambia hawanaga madhara ukilinganisha na kitendo cha mume kuchepuka ambao hupelekea kupoteza rasilimali za familia.
 
mkeo unakuta chura kubwa tandamu hasa, rangi imekubali, akitembea kiuno kinazunguka tu chenyewe na hana uchoyo, unataka sisi tufanye nini ndugu yangu?? eti? ata ingekua ni wewe ungefanyaje asee??
 
Back
Top Bottom