Kuna jinga moja lilikwiba pesa za umma akatiwa ndani gereza la keko, kufika jela akakuta kijana Mdogo anamiliki kimvuli, basi basi jamaa bila kujuwa akaenda kukakaa kimvulini, mwenye kimvuli chake aliporudi yule Boss alichezea makofi siyo ya dunia hii, kumbe kuna mshkaji wa mtaani yupo jela mule muda tu ndio akamuokowa na kuanzia hapo ndio alikuwa na maisha Salama jela mpaka anapata dhamana.
Humu kuna Watoto wamepata kazi juzi wa nadhani wasiokuwa na pesa ni wajinga.
Mimi weekend hizi kama mfuko inaruhusu mtaani hata laki mbili wana nawapiga chupa kama kawaida, ukiona mengi duniani huwezi kumdharau mtu hasa mwanaume.
Kama kuna watu wanazinguwa kwenye hizi bar tafuta namna bora ya kuwaepuka, lakini mjini jaribu kuheshimu watu.