Mtambuzi
Platinum Member
- Oct 29, 2008
- 8,810
- 15,398
Kama umeshawahi kufunga mbwa au kumchunguza, utagundua kwamba, mbwa dume ana kawaida ya kutoa sauti yenye kuonesha kuumia au kuhuzunika au kuomba hasa anapokutana na mbwa mwingine ambaye anajua wazi kuwa ana nguvu kuliko yeye. Lakini mbwa huyo huyo ataunguruma kwa sauti ya chini inayotoka ndani, kama vile amekasirika sana au anajitambulisha kwamba anajimudu pale anapokutana na mbwa ambaye anajua anaweza kupambana naye. Ukiwakagua mbwa utabaini sifa hiyo ya kuunguruma kwa namna tofauti kutoka mazingira flani hadi mengine. Pale ambapo anaona atashinda pambano, huwa ana mlio mmoja na pale anapoona atashindwa mlio huwa mwingine.Lakini je, hali kama hii iko kwa mbwa tu? Hapana, watafiti wanasema binadamu naye yuko hivyohivyo. Wanasema, linapokuja suala la namna tunavyojibu hali zenye kututisha, hatuna tofauti na mbwa.
Mbwa anashusha sauti na kuunguruma kutoka kooni kama anaamini kwamba, mbwa anayemkabili hamwezi. Mwanaume naye huwa na kawaida ya kushusha sauti yake na kuzungumza kama vile sauti yake ni mali sana, anapokuwa akizungumza na mtu ambaye anaamini anammudu kimwili. Kama ilivyo kwa mbwa, hata wanaume, hali hii hutokea bila wahusika kujua. Najua hata wewe mwanaume unayesoma hapa unaweza kutilia mashaka jambo hili, lakini kama ukianza kujiuliza sasa hivi ndipo ambapo utagundua kwamba, kwa wale watu ambao unaona kabisa unawamudu au ambao unaamini hawatishii usalama wako kimwili, utazungumza nao kwa sauti ya kutokea kooni au ndani, yenye kuonesha kujiamini.
Kwenye akili ya mwanaume tafsiri ya sauti hufanyika bila wenyewe kujua. Mwanaume anapomsikia mwenzake akizungumza kwa sauti iliyotulia na inayotoka ndani, huhisi kwamba, mtu huyo anayo nafasi kubwa zaidi kuliko yeye. Mwanaume humchukulia mwanaume mwenzao wa namna hiyo kama aliye na nafasi kubwa ya kumudu au kudhibiti. Kama umewahi kuchunguza utakubaliana name kwamba, wanaume huwa na kawaida ya kupandisha sauti na kuwa na sauti yenye mawimbi makali, pale wanapozungumza na mtu ambaye wanajua anawazidi hasa kimwili na kinguvu. Kama ni mtu ambaye wanaamini kwamba, wanamzidi, sauti zao huwa ni za kushiba na zinazotoka ndani.
Hii ina maana kwamba, bila wanaume wenyewe kujua, wanaposikia sauti iliyotulia, yaani inayotoka kwa wanaume wenzao huhisi kwamba, hao wenzao wanawamudu. Kumbuka hapa sizungumzii kupayuka au kuzungumza kwa kelele, bali nazungumzia utoaji wa sauti. Nikisema sauti kutoka kooni nina maana ya sauti nzito na yenye aina ya mamlaka (Vijana wa siku hizi huita Ki-besi) Lakini kwa sehemu kubwa, mamlaka au kummmudu mwanaume mwingine inapimwa zaidi kimwili kuliko madaraka au sifa nyingine. Hii ikiwa na maana kwamba, pale ambapo mwanaume anahisi kwamba, kimwili anamzidi au anaweza kumdhibiti mwingine, ndipo ambapo sauti yake huwa ni ile ya kutokea kooni. Haifahamiki ni kwa nini hasa wanaume hujikuta bila hiyari yao wakiwa na mabadiliko hayo ya sauti pale wanapokabiliana na wanaume wenzao, ambao ama wanajua kuwa wanawamudu au hawawamudu. Lakini wataalamu wanadhani, hali hiyo inatokana na maumbile ya wanaume kutaka kuoneshana tofauti zao. Bila shaka umeshawahi kuona hata kwenye sinema. Wale waigizaji ambao wanaamini kwamba, wanaweza kuwazidi nguvu adui zao, wanapozungumza nao, hutoa sauti zao kutokea kooni. Kuigiza kwa namna hii kunatokana na nadharia hii, kwamba, mwanaume mwenye nguvu hatoi sauti kali.
Mbwa anashusha sauti na kuunguruma kutoka kooni kama anaamini kwamba, mbwa anayemkabili hamwezi. Mwanaume naye huwa na kawaida ya kushusha sauti yake na kuzungumza kama vile sauti yake ni mali sana, anapokuwa akizungumza na mtu ambaye anaamini anammudu kimwili. Kama ilivyo kwa mbwa, hata wanaume, hali hii hutokea bila wahusika kujua. Najua hata wewe mwanaume unayesoma hapa unaweza kutilia mashaka jambo hili, lakini kama ukianza kujiuliza sasa hivi ndipo ambapo utagundua kwamba, kwa wale watu ambao unaona kabisa unawamudu au ambao unaamini hawatishii usalama wako kimwili, utazungumza nao kwa sauti ya kutokea kooni au ndani, yenye kuonesha kujiamini.
Kwenye akili ya mwanaume tafsiri ya sauti hufanyika bila wenyewe kujua. Mwanaume anapomsikia mwenzake akizungumza kwa sauti iliyotulia na inayotoka ndani, huhisi kwamba, mtu huyo anayo nafasi kubwa zaidi kuliko yeye. Mwanaume humchukulia mwanaume mwenzao wa namna hiyo kama aliye na nafasi kubwa ya kumudu au kudhibiti. Kama umewahi kuchunguza utakubaliana name kwamba, wanaume huwa na kawaida ya kupandisha sauti na kuwa na sauti yenye mawimbi makali, pale wanapozungumza na mtu ambaye wanajua anawazidi hasa kimwili na kinguvu. Kama ni mtu ambaye wanaamini kwamba, wanamzidi, sauti zao huwa ni za kushiba na zinazotoka ndani.
Hii ina maana kwamba, bila wanaume wenyewe kujua, wanaposikia sauti iliyotulia, yaani inayotoka kwa wanaume wenzao huhisi kwamba, hao wenzao wanawamudu. Kumbuka hapa sizungumzii kupayuka au kuzungumza kwa kelele, bali nazungumzia utoaji wa sauti. Nikisema sauti kutoka kooni nina maana ya sauti nzito na yenye aina ya mamlaka (Vijana wa siku hizi huita Ki-besi) Lakini kwa sehemu kubwa, mamlaka au kummmudu mwanaume mwingine inapimwa zaidi kimwili kuliko madaraka au sifa nyingine. Hii ikiwa na maana kwamba, pale ambapo mwanaume anahisi kwamba, kimwili anamzidi au anaweza kumdhibiti mwingine, ndipo ambapo sauti yake huwa ni ile ya kutokea kooni. Haifahamiki ni kwa nini hasa wanaume hujikuta bila hiyari yao wakiwa na mabadiliko hayo ya sauti pale wanapokabiliana na wanaume wenzao, ambao ama wanajua kuwa wanawamudu au hawawamudu. Lakini wataalamu wanadhani, hali hiyo inatokana na maumbile ya wanaume kutaka kuoneshana tofauti zao. Bila shaka umeshawahi kuona hata kwenye sinema. Wale waigizaji ambao wanaamini kwamba, wanaweza kuwazidi nguvu adui zao, wanapozungumza nao, hutoa sauti zao kutokea kooni. Kuigiza kwa namna hii kunatokana na nadharia hii, kwamba, mwanaume mwenye nguvu hatoi sauti kali.