ERTUGRUL BEY
JF-Expert Member
- Aug 6, 2020
- 11,534
- 21,547
Huko nyuma wazazi wetu na wazee wetu waliishi na bibi zetu na mama zetu,hali ya kuwa wanaume ndio watafutaji na ilikuwa hivyo siku zote,wala hawakuhofia sijui sisi tukifa watoto wetu wataishi vipi?
Kwasababu anayetoa riziki ni Mungu,kwahiyo hata kama hao walipo kufa Mwenyezi Mungu aliendelea kuipa riziki familia kwa namna anayojua yeye,na watu waliendelea kuishi na watu wakakua vizuri tu
Kimekuja kizazi ambacho kina woga wa maisha,wakaanza kubadilisha nidhamu ya ulimwengu huu,maana hapo awali nidhamu ilikuwa baba au mwanaume ndio mtafutaji na mama au mke analea familia
Sasa kizazi hiki kikaona nidhamu hii imepitwa na wakati,wakahofia maisha na kuhisi kwamba wao wanaume wakifa basi familia zao zitapata shida,wakasahau kabisa kwamba riziki inatoka kwa Allah
Sasa wakaanza kuona mwanamke nae ajishughulishe achangie upatikane mkate wa familia,na kweli baada ya wanawake kuona wanashinikizwa wachangie kulisha nao wakaanza kufanya hivyo
Kama haitoshi kizazi hiki cha wanaume ambao ni waoga wa maisha,wakaona hapana kuoa mwanamke ambaye ni wa darasa la saba au ambaye hajasoma sio sawa,inabidi waoe wake wasomi,basi dada zetu wakaona isiwe tabu nao wakafungua vitabu na alhamdulillah wana stashahada zao,shahada na shahada za uzamivu
Sasa ambacho hawakujua hiki kizazi cha wanaume waoga wa maisha kuwa,mwanamke wa zamani alikuwa mtiifu kwa mumewe kwasababu alikuwa anamtegemea mumewe kwa kila kitu,ndio maana walikuwa wenye nidhamu na adabu
Hawakujua kwamba baada ya mwanamke kusoma na kuingiza kipato,itafika kipindi ataweza kujitegemea na hivyo hato muhimtaji mwanaume tena kama zamani,kwani nae anauwezo wa kupata mkate wake wa kila siku
Matokeo yake leo hii,walio oa wanawake walio soma wanalia na walioa wanawake wenye kipato pia wanalia,wamesahau kwamba haya mazingira wametengeneza wao wenyewe
Na riziki ndio imekuwa mtihani kweli kweli,kwa maana vipato havina baraka kwasababu hamu mtegemei Mwenyezi Mungu sasa ila mnategemea kazi zenu ndio zitaendesha maisha yenu,matokeo yake tunaenda resi sana lakini mwisho wa siku mishahara haikutani,yaani lazima utakuwa na madeni tu
Na mlibugi zaidi kwakutojua kwamba mwanamke ni malikia ameumbwa ili ahudumiwe na sio yeye ahudumie,ndio maana kutwa kuchwa mnalalamika mwanamke anakipato kikubwa lakini hakuna anachochangia ndani,hamjui kwamba mwanamke sio asili yake kuprovide bali tuna wafosi tu
Kwahiyo haya tuliyataka wenyewe,tumeoa wasomi wanatuendesha,na tumeoa wajasilia mali wanatuendesha,kwahiyo buddies tukae kwa kutulia na tunapambane na hali zetu
Haya hayakutokea kwa bahati mbaya ila tuliyatafuta wenyewe na sasa tuishi nayo
Na wanawake wakazidi kujiongeza kwa kutaka haki sawa zaidi kwahiyo yajayo yanafurahisha
Ni hayo tu!